benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
Waandishi wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Fortune Francis, Sunday George na dereva wa kampuni hiyo, Omary Mhando wamejeruhiwa baada ya kupigwa na kundi la vijana ambao hawajafahamika wa chama gani wakati wakitekeleza majukumu ya katika Uwanja wa Buriaga, Temeke jijini Dar es Salaam.
Tukio hilo limetoekea leo Jumamosi, Julai 22, 2023 wakati walipokwenda kuangalia maandalizi ya mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chadema unaotarajia kufanyika kesho Jumapili.
Mbali na kujeruhiwa kwa waandishi hao na dereva, pia wameibiwa simu za mkononi pamoja na gari kuharibiwa kwa kuvunjwa vioo.
Tayari uongozi umeripoti tukio hilo Kituo cha Polisi cha Chang’ombe kama hatua ya awali wakati taratibu zingine za kiofisi zikiendelea.
Wameripoti Mwananchi
Tukio hilo limetoekea leo Jumamosi, Julai 22, 2023 wakati walipokwenda kuangalia maandalizi ya mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chadema unaotarajia kufanyika kesho Jumapili.
Mbali na kujeruhiwa kwa waandishi hao na dereva, pia wameibiwa simu za mkononi pamoja na gari kuharibiwa kwa kuvunjwa vioo.
Tayari uongozi umeripoti tukio hilo Kituo cha Polisi cha Chang’ombe kama hatua ya awali wakati taratibu zingine za kiofisi zikiendelea.
Wameripoti Mwananchi