Waandishi wa kitabu cha Zaburi

Waandishi wa kitabu cha Zaburi

Umejuaje kama hajui maana yake

Naona ulilokuwa unaliwaza wakati unaniambia nikuletee maana ya Zabur limeenda vibaya🤣🤣🤣
Niambie basi wewe mwenye Quran ,

Hilo neno la Zaburi ndani ya Quran maana yake ni nini?
 
Umejuaje kama hajui asili yake?

Maana ya Zabur umeletewa uliza sasa maswali sio kuonyesha masikitiko yako
Neno “Zaburi” umetoa wapi?

Je, ni Kiarabu au Kiebrania?

Kama ni Kiebrania, kwa nini Qur’an itumie neno la dini nyingine kama ni ufunuo kamili wa mwisho?
 
Neno “Zaburi” umetoa wapi?

Je, ni Kiarabu au Kiebrania?

Kama ni Kiebrania, kwa nini Qur’an itumie neno la dini nyingine kama ni ufunuo kamili wa mwisho?

Umeuliza: Neno “Zaburi” umetoa wapi?​

Majibu:

Neno Zaburi limetajwa moja kwa moja ndani ya Qur’an:


“Na tulimpa Daud Zaburi.” (Qur’an 4:163)

Kwa hiyo, chanzo chake kwa Muislamu ni Qur’an, si Mkristo wala Myahudi.

Ukauliza : Je, “Zaburi” ni Kiarabu au Kiebrania?​

Majibu:

Ndiyo, kihistoria:

Asili ya neno liko karibu na Kiebrania “Tehillim”
Au Kisyria/Aramu “Zabura” (maandiko, nyimbo)

Lakini Qur’an haikanushi kutumia maneno yasiyo ya asili ya Kiarabu.

Waarabu wa zama za Mtume ﷺ tayari walitumia maneno mengi ya kigeni:

Injil,Taurat ,Fir’aun , Iblis ,Sijjil

Maneno haya yalikuwa yamearabiishwa na yakawa sehemu ya lugha ya Kiarabu.

Ukauliza: Kwa nini Qur’an itumie neno la “dini nyingine”?

Majibu:

Hapa kuna kutokufahamu ki msingi.

Zaburi si ya dini nyingine

Zaburi ni ufunuo wa Mwenyezi Mungu kwa Nabii Daud (alayhi salam)


Uislamu unaamini: Musa → Taurat, Daud → Zaburi , Isa → Injil , Muhammad ﷺ → Qur’an

KUMBUKA : Mungu ni Mmoja, dini ni moja (Uislamu), Mitume ni wengi.


Qur’an inasema:

“…Amewawekea nyinyi, enyi watu, Sheria ya Dini tuliyokuletea kwa njia ya wahyi, ewe Mtume, nayo ni Uislamu, na ile Aliyomuusia Nūḥ aifuate kivitendo na aifikishe kwa watu, na ile aliyowausia Ibrāhīm, Mūsā na Īsā (Watano hawa ndio Ulū al- 'azm [wenye hima] miongoni mwa Mitume kulingana na kauli iliyo mashuhuri) kwamba msimamishe Dini kwa kumpwekesha Mwenyezi Mungu, kumtii na kumuabudu Yeye na sio mwingine, na msitafautiane katika Dini ambayo nimewaamrisha muifuate. Ni kubwa mno juu ya washirikina lile mnalowalingania la kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kumtakasia ibada. Mwenyezi Mungu Anamchagua Anayemtaka miongoni mwa viumbe Vyake awe ni mwenye kumpwekesha na Anamuongoza yule anayerejea Kwake afanye matendo ya utiifu Kwake” (Qur’an 42:13)

Kwa hiyo:

Qur’an haitumii “neno la dini nyingine”

Inathibitisha ufunuo ule ule wa Mungu kwa Mitume waliotangulia

Kwa kumalizia:

“Zaburi si ya Ukristo, ni ufunuo wa Mungu kwa Nabii Daud. Qur’an haitumii neno la dini nyingine, bali inathibitisha ufunuo ule ule wa Mungu. Na kutumia neno lenye asili ya kale hakupunguzi ufunuo wa Qur’an, kwani lugha hubeba maneno kutoka tamaduni tofauti.”


 
Jibu basi Neno ZABURI ndani ya Quran ,maana yake ipi ? Muhammad alilitoa wapi au halina maana ?

Zaburi ndani ya Qur’an lina maana: ni ufunuo wa Mungu kwa Nabii Daud. Muhammad ﷺ hakulitoa kwa nafsi yake bali kwa wahyi. Kutumia jina lile lile si kukopa, ni kuthibitisha ufunuo ule ule wa Mungu.
 
dini ya kiislam imejaa vitu ambavyo hata mungu mwenyewe huenda anavishangaa. Unamlazisha Mungu kwamba ameshusha kitabu cha zaburi wakati walioandika waliwahi ishi hapa duniani, halafu huyo mungu ashushe kitu watu wachakachue awatazame tu kwani hao watu ndo wanao mwamulia Mungu cha kufanya?, Ile zuburi iliyochakachuliwa na hao watu iko wapi.
Yaani mtu anabishia biblia halafu anafanyareference quran. Unambishia myahudi unafanya reference kwa mwarabu watu wenye tofauti kabisa, au unambishia mkerewe na mambo ya mila zake kwa kufanyarefrence kwa mmakonde!
We ukiamini Mohamad ndo mtakatifu wako, usimbishie mtu anaye amini yesu ndo mtakatifu wake. Eti unachoamini wewe sio ila ninachoamini ndio. Ukiuliza kwanini unaambiwa quran imesema, kwani huyo Mungu ambaye wengine tunaamini kwamba ananguvu kuliko kitu chochote ulimwenguni alishindwaje kuhifadhi kitabu chake kisichakachuliwe badala yake akiache alete kitabu kingine! Kama mungu alishindwa kuwadhibiti wachakachuaji zaburi unajuaje kwamba amewadhibiti wasichakachue quran, kwa sababu wanaotumia biblia ni binadamu walewale kama wanaotumia quran.


Uislamu haumfundishi Mungu ashindwe. Biblia yenu inakiri Zaburi ni ufunuo kwa Daud, na wanazuoni wa Biblia wanakiri maandiko yalipitia mikono ya wanadamu.

Hilo si tusi, ni historia. Mungu kwa hikima yake aliacha hilo litokee, kisha akateremsha Qur’an kama kigezo cha mwisho na akaahidi mwenyewe kukihifadhi (Qur’an 15:9). Kila dini hurejea kitabu chake—sio ajabu Muislamu kurejea Qur’an.”

Kama Mungu alishindwa kuhifadhi Zaburi, kwa nini Yesu na Mitume waliendelea kuzinukuu kama Neno la Mungu, ilhali tayari zilikuwa zimeandikwa na wanadamu?

Wewe unarejea Biblia kwa imani yako, mimi narejea Qur’an kwa imani yangu. Lengo si kumlazimisha Mungu wala kumdharau Mtume wa mtu mwingine, bali kueleza msimamo wa imani yetu. Tukiheshimiana, mjadala unabaki wa maana.
 
Kwahiyo Covax Jagina hata chat gpt wameshindwa kujibu hili.

Je kuna sehem ambayo Quran inasema Tourat au Injili imeandikwa kwa maneno yasiyo ya allah?.

Qur’an haikanushi asili ya Zaburi, lakini inakanusha usalama wa maandiko ya awali kwa ujumla. Na historia yenyewe inaonyesha Zaburi hazikubaki katika toleo moja. Kwa hiyo hoja si “Zaburi ni uongo”, bali “Zaburi ya leo haiwezi kuthibitishwa kuwa ile ile ya Daudi.”
 
Qur’an haikanushi asili ya Zaburi, lakini inakanusha usalama wa maandiko ya awali kwa ujumla. Na historia yenyewe inaonyesha Zaburi hazikubaki katika toleo moja. Kwa hiyo hoja si “Zaburi ni uongo”, bali “Zaburi ya leo haiwezi kuthibitishwa kuwa ile ile ya Daudi.”
Sawa. Je

Zaburi ya leo haiwezi kuthibitishwa kuwa ile ile ya Daudi.”

Haya kaongea Mohamed au nani?.
 
Zaburi ndani ya Qur’an lina maana: ni ufunuo wa Mungu kwa Nabii Daud. Muhammad ﷺ hakulitoa kwa nafsi yake bali kwa wahyi. Kutumia jina lile lile si kukopa, ni kuthibitisha ufunuo ule ule wa Mungu.
Chagua moja tu,

Qur’an ikikiri neno Zaburi ni nyimbo basi Uislamu unapingana na Zaburi
Kama Zaburi si nyimbo basi Qur’an imetumia neno vibaya,imeiba neno la watu bila kujua maana yake

Muhammad hakujua maana halisi ya Zaburi

Qur’an ilinakili kutoka vyanzo vya Kiyahudi bila uhakiki

Ni lipi unalichagua, na kwa nini?
 

Umeuliza: Neno “Zaburi” umetoa wapi?​

Majibu:

Neno Zaburi limetajwa moja kwa moja ndani ya Qur’an:




Kwa hiyo, chanzo chake kwa Muislamu ni Qur’an, si Mkristo wala Myahudi.

Ukauliza : Je, “Zaburi” ni Kiarabu au Kiebrania?​

Majibu:

Ndiyo, kihistoria:

Asili ya neno liko karibu na Kiebrania “Tehillim”
Au Kisyria/Aramu “Zabura” (maandiko, nyimbo)

Lakini Qur’an haikanushi kutumia maneno yasiyo ya asili ya Kiarabu.

Waarabu wa zama za Mtume ﷺ tayari walitumia maneno mengi ya kigeni:

Injil,Taurat ,Fir’aun , Iblis ,Sijjil

Maneno haya yalikuwa yamearabiishwa na yakawa sehemu ya lugha ya Kiarabu.

Ukauliza: Kwa nini Qur’an itumie neno la “dini nyingine”?

Majibu:

Hapa kuna kutokufahamu ki msingi.

Zaburi si ya dini nyingine

Zaburi ni ufunuo wa Mwenyezi Mungu kwa Nabii Daud (alayhi salam)


Uislamu unaamini: Musa → Taurat, Daud → Zaburi , Isa → Injil , Muhammad ﷺ → Qur’an

KUMBUKA : Mungu ni Mmoja, dini ni moja (Uislamu), Mitume ni wengi.


Qur’an inasema:



Kwa hiyo:

Qur’an haitumii “neno la dini nyingine”

Inathibitisha ufunuo ule ule wa Mungu kwa Mitume waliotangulia

Kwa kumalizia:




Hivi hayo unakopi kwa CHATGPT unayosoma au unakopi tu,?

Tatizo si Daudi, tatizo si Zaburi tatizo ni Qur’an kutumia neno lenye historia, lugha, na maana iliyo wazi, kisha kuliacha ligongane na mafundisho yake yenyewe.

Mimi nauliza maswali katika
lugha
historia
mantiki
consistency ya ufunuo

Kwa nini Qur’an itumie maneno ya vitabu vya awali bila kuyarekebisha kimaudhui kama yalikuwa yamepotoshwa?
 
Neno “Zaburi” umetoa wapi?

Je, ni Kiarabu au Kiebrania?

Kama ni Kiebrania, kwa nini Qur’an itumie neno la dini nyingine kama ni ufunuo kamili wa mwisho?
Ila wewe unafurahisha kweli🤣🤣🤣
Aliyekwambia kuwa neno likiwa la lugha fulani basi ni la dini fulani ni nani???
 
Hebu tuambie. Je Kuna kitabu cha allah ambacho hakijaandikwa kwa mikono ya Binadamu?.
Hao waandishi wa Qur’an wamenakili na hawajatumia maneno yao kuandika Qur’an tofauti na vitabu vyenu ambavyo wenyewe mnakiri kuwa ni maneno ya watu
 
Hebu tuambie. Je Kuna kitabu cha allah ambacho hakijaandikwa kwa mikono ya Binadamu?.

Hakuna kitabu cha Mungu kilichoandikwa bila binadamu, lakini tofauti ni hili:
Qur’an iliandikwa na kuhifadhiwa chini ya ulinzi wa Mungu dhidi ya mabadiliko, Torati, Injili na Zaburi hazina ulinzi huo.

Kuandikwa na binadamu si tatizo; tatizo ni kubadilishwa na binadamu bila uhakika wa ulinzi wa Mungu
 
kaongea huyo aliyeleta mada

Waislam wanaamini Quran na Mohamed.
Kama hakuna sehem Mohamed au Quran imeonyesha. Unapata wap ujasiri wa kusema Zaburi iliyopo sio ile aliyopewa Daudi..

Hauoni kuwa ni ubishan wa kijinga ambao hauna support evidence kwenye source zinazoaminika na jamii.

Ukiwa hata na akili tu ndogo unaweza kujua tu hilo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom