Waagizaji mafuta: Kwanini Wahindi na Waarabu peke yao?!

Waarabu wa zamani hapa Tanzania walikuwa na biashara za maduka ya rejareja, karibu yote Dar.

Wamepand kidogo kidogo mpaka sasa wana hayo makampuni makubwa makubwa, sasa wewe unataka uanze kukimbia hata kutambaa hujaanza?

Wachaga ni mfano mzuri wa biashara (wana ila moja tu, ambayo waarabu hawana), wanaanza kibanda cha sigara, mara viwili, mara vitatu, mara wanaenda Dubai mara wanashindana na AM.
Faiza,
Umenichekesha sana. Nilipokuwa mdogo kuna huyu Mwarabu akiitwa mshiiri. Yeye alikuwa anauza kanga, nguo za akina mama, etc. etc. Sasa kitu cha ajabu, akikuta hauna hela, mathalani kaja kule kwetu bara mwezi April, atakuuzia nguo bila kukutoza kitu. Anajua kuwa mwezi wa saba nane ni wakati wa kuvuna pamba maeneo ya kwetu na watu wana hela. Utamkuta anapita kila nyumba aliyotoa nguo na kanga za mkopo kukusanya hela zake. Hii ilikuwa inatokea karibu kila msimu wa pamba. Na alikuwa hasahau!
 
Faiza,
Umenichekesha sana. Nilipokuwa mdogo kuna huyu Mwarabu akiitwa mshiiri. Yeye alikuwa anauza kanga, nguo za akina mama, etc. etc. Sasa kitu cha ajabu, akikuta hauna hela, mathalani kaja kule kwetu bara mwezi April, atakuuzia nguo bila kukutoza kitu. Anajua kuwa mwezi wa saba nane ni wakati wa kuvuna pamba maeneo ya kwetu na watu wana hela. Utamkuta anapita kila nyumba aliyotoa nguo na kanga za mkopo kukusanya hela zake. Hii ilikuwa inatokea karibu kila msimu wa pamba. Na alikuwa hasahau!


Kweli nawakumbuka kabisa hapa Dar. walikuwa wakiitwa "guoguo" na Haki ya Mungu nawajua ambao wametajirika sana baada ya hapo, au watoto zao, mfano mzuri ni huyu Mwarabu mwenye Kariakoo Bazaar sasa hivi, alianza kuwa mteja hapo Kariakoo Bazaar (wenyewe orijini walikuwa wahindi) akawa anatembeza nyumba kwa nyumba mpaka akainunua hiyo Kariakoo Bazaar na sasa ana viwanda.

Mfano mwingine ni huyu S. S. Bakhresa, alianza na duka la kutengeneza viatu vya mikanda pale mtaa wa Uhuru, sasa ni one of the richest man in Africa.

Mifano ipo mingi tu, hawa Oilcom, walikuwa na duka la vyakula huko Morogoro wakapate tenda ya kuwalisha wanajeshi Ngerengere, sasa ni wasambazaji wakubwa wa mafuta Tanzania na nchi za jirani.

Habari za matajiri wa Dar. Wa asili yoyote ile, tuulize sisi tuliokuwa nao, tumesoma nao, tumecheza nao, tumekula nao, tumesota nao, Tunawajuwa vizuri sana.
 
Aaaah mkuu wangu wakati mwingine tukubali Hekma ya Mwenyezi Mungu alowaumba Waarabu na Wahindi kwa kipaji cha wafanya biashara (merchant) kabla hata mzungu hajajua biashara ya kununua na kuuza. Na pengine ni ktk kutazama uasilia huo huo ndio maana sisi tunalima sana mazao ya chakula na kuuza wakati hakuna mhindi wala mwarabu anayeshika jembe kulima!...

Mkandara,

Sikubaliani na mawazo ya namna hii hata kidogo. Kuwaza namna hii kunaendeleza utumwa wa kifikra ambao ndiyo sababu kuu ya umaskini wa waafrika kwa ujumla.
Viongozi wetu tunaowachagua wenyewe wanawapa fursa za kutuibia na pia wanawalinda dhidi ya mkono wa sheria hata pale ushahidi unapokuwa dhahiri.(mfano EPA)
Viongozi wengi ni vibaraka wa hao wafanya biashara kwa kupewa vizawadi vidogo vidogo au kushirikiana nao kuibiia uma kwa makubaliano ya kupewa share kidogo.
Maadui wa kiuchumi wa mtu mweusi ni weusi wenzake, jaribu kufanya uchunguzi kidogo tu katika ofisi za serikali na sehemu nyingine za huduma namna ambavyo mtoa huduma mweusi anavyorespond kwa mweusi mwenzake na kwa mtu wa rangi nyingine.
Ukombozi wa kweli wa kiuchumi kwa weusi utapatikana tu pale ambapo fikra zao zitakuwa huru kwa maslahi yao wenyewe.
Angalia hata hotuba za viongozi weusi kwa wageni wa rangi nyingine, utafikiri viongozi hao wanatoa ripoti kwa wakubwa zao kikazi.
Tukipata viongozi wa kisiasa watakaopenda uchumi wetu uwe mikononi mwa weusi, itawezekana hivyo lakini kwa hali kama ilivyo sasa, mabadiliko makubwa ya fikra za viongozi pamoja na wananchi wenyewe yanahitajika.
Fikra za viongozi wengi weusi ni za kitumwa na ndiyo sababu wanawaza kuombaomba kimataifa, wanawaogopa mafisadi, wanasaini mikataba mibovu (unilateral) baadaye wanabaki kulalamika n.k.
Kwa Mungu binadamu wote ni sawa na wanaweza kufanya chochote kwa kiwango kinacholingana ila ujinga, woga , uzembe na vinavyofanana na ndivyo vinavyowatofautisha.
 
Kweli nawakumbuka kabisa hapa Dar. walikuwa wakiitwa ;guoguot; na Haki ya Mungu nawajua ambao wametajirika sana baada ya hapo, au watoto zao, mfano mzuri ni huyu Mwarabu mwenye Kariakoo Bazaar sasa hivi, alianza kuwa mteja hapo Kariakoo Bazaar (wenyewe orijini walikuwa wahindi) akawa anatembeza nyumba kwa nyumba mpaka akainunua hiyo Kariakoo Bazaar na sasa ana viwanda.
Mfano mwingine ni huyu S. S. Bakhresa, alianza na duka la kutengeneza viatu vya mikanda pale mtaa wa Uhuru, sasa ni one of the richest man in Africa.
Mifano ipo mingi tu, hawa Oilcom, walikuwa na duka la vyakula huko Morogoro wakapate tenda ya kuwalisha wanajeshi Ngerengere, sasa ni wasambazaji wakubwa wa mafuta Tanzania na nchi za jirani.
Habari za matajiri wa Dar. Wa asili yoyote ile, tuulize sisi tuliokuwa nao, tumesoma nao, tumecheza nao, tumekula nao, tumesota nao, Tunawajuwa vizuri sana.
Faiza, uwewasahau kina Goro Store, Ahmed Bashuani na mzee wao (Big Bon)
 
Kweli nawakumbuka kabisa hapa Dar. walikuwa wakiitwa "guoguo" na Haki ya Mungu nawajua ambao wametajirika sana baada ya hapo, au watoto zao, mfano mzuri ni huyu Mwarabu mwenye Kariakoo Bazaar sasa hivi, alianza kuwa mteja hapo Kariakoo Bazaar (wenyewe orijini walikuwa wahindi) akawa anatembeza nyumba kwa nyumba mpaka akainunua hiyo Kariakoo Bazaar na sasa ana viwanda.

Mfano mwingine ni huyu S. S. Bakhresa, alianza na duka la kutengeneza viatu vya mikanda pale mtaa wa Uhuru, sasa ni one of the richest man in Africa.

Mifano ipo mingi tu, hawa Oilcom, walikuwa na duka la vyakula huko Morogoro wakapate tenda ya kuwalisha wanajeshi Ngerengere, sasa ni wasambazaji wakubwa wa mafuta Tanzania na nchi za jirani.

Habari za matajiri wa Dar. Wa asili yoyote ile, tuulize sisi tuliokuwa nao, tumesoma nao, tumecheza nao, tumekula nao, tumesota nao, Tunawajuwa vizuri sana.

Oyaa, kumbe na wewe kakijeba flani maana "guoguo" ni ya loooooong tyme!!!! haha ahahaha!
 
are they (localpetroleum companies owned by arabs) doing clean business??
 
View attachment 34907

..nimepita kule michuzi blog nikashtuka kuona picha ya waagizaji wa mafuta nchini.

..jamani sijawahi kuona ktk nchi yoyote ile wananchi wake wakiwa under-represented kiasi hiki.

..kwanini hakuna watanzania halisi ktk biashara hii?

..hivi serikali imeridhika na hali ilivyo kwamba biashara hii iwe monopoly ya wahindi na waarabu tu?

..call me mbaguzi or whatever you want, but we need to africanize this business without any delay or excuses.

joka kuu hujafanya utafiti wa kutosha......na chuki zako ni za wazi japo umemalizia kwa kujikinga tusikuite mbaguzi....kweli sio mbaguzi ila una donge la tumbo.....uchoyo dhidi ya waarabu na wahindi as wazungu mabwana zako hukuwataja....ukweli kuna wenye vituo vya mafuta na waigizaji....sasa wewe labda hao ulio waona kwenye picha ni wenye vituo vya mafuta. Waagizaji wakubwa wa mafuata ni kama ifutavo..the big one on top
  • bp......ya waingereza
  • gapco...nayo ilikua ya waingereza
  • oryx..ya makaburu
  • kobil .....
  • national oil...
kampuni kubwa za warabu ni
  • oil com
  • camel oil
wahindi labda ni mogas na gbp.
Lakini yuna makampuni makubwa ya wabongo kama
  • world oil ....huyu nimbongo na ameinvest sana katika mafuta..in fact facility yake ni kubwa na ya kisasa kule vijibweni kigamboni
  • yupo zakaria nae ni mzambazaji mkubwa...na yeye ni mwafrika (lakini ana rangi rangi aliyopata kutoka kwa babu yakee mjerumani) sasa labda kwa kigezo chako hayumo katika africanasation!!!1
tanzania ni nchi pekee katika east africa ambayo serikali yake ni 100% africanised. Mhindi ama mwarabu hata kama atakua ana vigezo gani hapati kazi ya serikalini hivi sasa ...serikali ya tanzania in fact sio equal opportunity employer!!! Tofauti na wenzetu wa kenya wao elimu na ujuzi ndio unaoangaliwa na rangi ya mtu...alimradi wewe ni mkenya basi nafasi unayo.....ubaguzi huu ndio umetufikisha hapa gizani.......
 
Mkandara,

Sikubaliani na mawazo ya namna hii hata kidogo. Kuwaza namna hii kunaendeleza utumwa wa kifikra ambao ndiyo sababu kuu ya umaskini wa waafrika kwa ujumla.
Viongozi wetu tunaowachagua wenyewe wanawapa fursa za kutuibia na pia wanawalinda dhidi ya mkono wa sheria hata pale ushahidi unapokuwa dhahiri.(mfano EPA)
Viongozi wengi ni vibaraka wa hao wafanya biashara kwa kupewa vizawadi vidogo vidogo au kushirikiana nao kuibiia uma kwa makubaliano ya kupewa share kidogo.
Maadui wa kiuchumi wa mtu mweusi ni weusi wenzake, jaribu kufanya uchunguzi kidogo tu katika ofisi za serikali na sehemu nyingine za huduma namna ambavyo mtoa huduma mweusi anavyorespond kwa mweusi mwenzake na kwa mtu wa rangi nyingine.
Ukombozi wa kweli wa kiuchumi kwa weusi utapatikana tu pale ambapo fikra zao zitakuwa huru kwa maslahi yao wenyewe.
Angalia hata hotuba za viongozi weusi kwa wageni wa rangi nyingine, utafikiri viongozi hao wanatoa ripoti kwa wakubwa zao kikazi.
Tukipata viongozi wa kisiasa watakaopenda uchumi wetu uwe mikononi mwa weusi, itawezekana hivyo lakini kwa hali kama ilivyo sasa, mabadiliko makubwa ya fikra za viongozi pamoja na wananchi wenyewe yanahitajika.
Fikra za viongozi wengi weusi ni za kitumwa na ndiyo sababu wanawaza kuombaomba kimataifa, wanawaogopa mafisadi, wanasaini mikataba mibovu (unilateral) baadaye wanabaki kulalamika n.k.
Kwa Mungu binadamu wote ni sawa na wanaweza kufanya chochote kwa kiwango kinacholingana ila ujinga, woga , uzembe na vinavyofanana na ndivyo vinavyowatofautisha.
Najua sana na nakubali sana pengine napingana na imani zetu au kisayansi lakini ukweli upo kwamba kila race iimebarikiwa kwa jambo fulani zaidi ya race nyinginezo. Kama ile sinema ya - White man can't jump ni sinema lakini upo ukweli fulani kwamba mzungu hawezi kuruka kama mtu mweusi ktk mchezo wa Basketball.. as to say hivi ni lini mara ya mwisho mzungu aliwahi kushinda dunk competition?..

Hivyo hivyo ktk kukubali ukweli kama huu, waarabu na wahindi ni wafanyabiashara toka enzi (merchant) kabla hata wazungu hawajafahamu biashara za uchuuzi. Na kifupi msingi wa somo la biashara limetokana na mfumo wa kibiashara ambao waarabu na wahindi waliufanya bila kwenda darasani. mambo mengi yamechukuliwa toka ktk mfumo wao na kuuweka ktk vitabu.. Hivyo biashara sio somo la kuvumbuliwa na wala sio sayansi. Ni sawa na Mbatu aloweza kulima na kuvuna kwa kufuata majira ya masika na kiangazi bila kwenda shule au Nilotics kama Wajaluo kuvua samaki kwa mikuki na matenga bila nyavu..Na bila kusahau Wamasai na uchungaji mtu mmoja aweza kuchunga ng'ombe 300..

Kwa hiyo, swala la kujaaliwa lipo na tunaliweka pembeni na ndio maana ya hoja yangu kwa sababu hakuna sababu yoyote inayotufanya sisi tushindwe kuagiza mafuta. Mtasema kibali basi agiza mafuta peleka Kongo, Burundi au Uganda kote wanahitaji mafuta na sii lazima upate kibali cha TZ.. Kusita kote tulokuwa nako ni kutokana na utamaduni wa mtu.. Biashara sii utamaduni wetu na kwa yule aliyeweza kufanya basi kavuka mipaka yake kama vile Mmasai kuvua samaki au mwarabu kulima shamba la mahindi..

Mwisho labda wewe nambie kwa nini Wamasai hawavui samaki au waarabu/wahindi hawalimi mahindi..
 
Nimesikia watu wakiongea pale kariakoo eti biashara ya mafuta ni alqaida ndio wawekezaji wakuu hapa bongo.....ndio sababu wengi ni waarabu......sina uhakika lakini
 
Hamna cha ajabu hapo. Nenda Muhimbili ukaone jinsi Madaktari wa Kihindi walivyo zagaa mawodini, achilia mbali Mahospitali na Kliniki za Wahindi na Wageni wengine zenye viwango vya juu zilivyozagaa nchi nzima, pamoja na mashule, mahoteli, magereji, building and road contractors, you name it...ni Wahindi na Waarabu. Ukweli ni kwamba viwango vya kazi na huduma zao, ukilinganisha na Wazawa vipo juu zaidi. Tukubali, tusikubali, Watanzania wote, na haswa economic and social elites, wanawategemea sana Wahindi na Waarabu. Bila wao, nchi itasimama. And that's the hard truth...
 
Faiza, uwewasahau kina Goro Store, Ahmed Bashuani na mzee wao (Big Bon)

Huyo alianza kwa bucha ya nyama pale mtaa wa Jamhuri, karibu na Naaz Hotel enzi hizo, siku hizi kuna Chinese Restaurant. Si unaona katokea wapi? kwenye bucha ya nyama!
 
Miafrika ndivyo tulivyo, kubwabwaja tu lakini hamna chochote cha maana. Ngozi nyeupe ni nyeupe tu.

Ukweli hubaki kuwa ukweli.

Leo tunalalamika wakati tunajijua wazi kabisa kuwa hata makazini hatuishi:

Kufiwa: Leo mjomba kesho anti, kesho kutwa bibi, mpaka wengine wanasahau leo sijui waseme wamefiwa na nani. Kuumwa, kwenda kunywa chai saa za ofisi, masababu kibaao.

Hatujui kuwajibika kabisa, kila kitu baadae, njoo kesho, leo hayupo kenda kuzika, ametoka kwenda kula, atarudi sasa hivi msubiri kidogo.

Nenda kwenye biashara za wahindi na waarabu, hukuti kitu kama hicho. Akiumwa anaumwa kweli, akifiwa kafiwa kweli. Halafu tunataka kushinda nao?
 
Huyo alianza kwa bucha ya nyama pale mtaa wa Jamhuri, karibu na Naaz Hotel enzi hizo, siku hizi kuna Chinese Restaurant. Si unaona katokea wapi? kwenye bucha ya nyama!

Wewe kujifanya unajua kila kitu!? Hebu tuelezee basi historia nzima ya Ahmed Bahashwan kuanzia "bucha ya nyama" unayodai alianzia, huku ukitaja maduka na aina zote za biashara alizowaki kufanya hadi hivi leo, na sasa hivi biashara zake zinaendeleaje...
 
Wewe kujifanya unajua kila kitu!? Hebu tuelezee basi historia nzima ya Ahmed Bahashwan kuanzia "bucha ya nyama" unayodai alianzia, ukitaja maduka na aina zote za biashara alizofanya.

Samahani sana, sizijui zote lakini najuwa kabla ya kuwa na kituo cha mafuta alikuwa na bucha na nimekutajia mpaka ilipokuwepo. Na ndugu yake (Marehem Abdallah Bahashwan) alikuwa na duka la kuuza viungo (spices) ambalo mbaka sasa linaendelezwa na wanawe, huko uhindini.

Tafadhali usinishobokee, watu wa Dar nawajua vizuri sana, ni kwetu. Kujuana haina maana mjuane kila kitu, tunavijua tuvijuavyo na tusivyovijuwa tunawaachia wenyewe.

Sasa wewe kutaka nikutajie toka alipozaliwa kauza bajia, maandazi, aaahhhhh? unanini weyee? Unanshangaza!
 
Samahani sana, sizijui zote lakini najuwa kabla ya kuwa na kituo cha mafuta alikuwa na bucha na nimekutajia mpaka ilipokuwepo. Na ndugu yake (Abdallah) alikuwa na duka la kuuza viungo (spices) ambalo mbaka sasa linaendelezwa na wanawe, huko uhindini.

Tafadhali usinishobokee, watu wa Dar nawajua vizuri sana, ni kwetu. Kujuana haiana maana mjuane kila kitu tunavijua tuvijuavyo na tusivyovijuwa tunawaachia wenyewe.

Sasa wewe kutaka nikutajie toka alipozaliwa kauza bajia, maandazi, aaahhhhh? unanini weyee? Unanshangaza!

Kwa hiyo, kutoka "bucha ya nyama" hadi "kituo cha mafuta" hujui alifikaje, si ndiyo? Na hilo "duka la kuuza viungo" unalodai lipo hadi hivi leo linaitwaje, lipo mtaa gani, na linaendesha na "wanawe" wenye majina gani? Iweje mtu ufikie kiwango cha kufanya biashara ya "kituo cha mafuta" halafu bado ung'ang'anie kuendesha "duka la viungo"?
 
Kwa hiyo, kutoka "bucha ya nyama" hadi "kituo cha mafuta" hujui alifikaje, si ndiyo? Na hilo "duka la kuuza viungo" unalodai lipo hadi hivi leo linaitwaje, lipo mtaa gani, na linaendesha na "wanawe" wenye majina gani? Iweje mtu ufikie kiwango cha kufanya biashara ya "kituo cha mafuta" halafu bado ung'ang'anie kuendesha "duka la viungo"?

Wewe kama unayakubali yakubali kama unayakataa yakatae, sipo hapa kuulizwa maswali ya kitoto. Duka la viungo kwa sasa linaendshwa na "Buye" na hilo ni la Marehem Mzee Abdallah Bahshwan ambae kaka yake (Marehem pia) ndio alikuwa na Bucha na baadae akawa na hicho kituo cha mafuta cha Msimbazi ambacho sasa vyote, duka na kituo vinaendeshwa na watoto tu, pengine hao watoto hata hiyo bucha hawajawahi kuiona.

Unalo?
 
Back
Top Bottom