Mbona sasa mnataka kwenda personal?
Welcome to IQTest.com, home of the original online IQ test.
Click here to take our free, private, and fun IQ test.
Our original IQ test is the most scientifically valid IQ test available on the web today. Previously offered only to corporations, schools, and in certified professional applications, it is now available to you. In addition to measuring your general IQ, our exclusive test assesses your performance in 13 different areas of intelligence, revealing your key cognizant strengths and weaknesses.
Developed by PhDs and statistically sound, our test reflects the best research available.
Click to begin.
What is an IQ?
An Intelligence Quotient indicates a person's mental abilities relative to others of approximately the same age. Everyone has hundreds of specific mental abilities--some can be measured accurately and are reliable predictors of academic and financial success.
It is my understanding that the preponderance of evidence points to nurture rather than nature as the main contributor to IQ.
Augustine Moshi
Kichuguu umesahau kwamba ni sisi wenyewe tunaowapigia kura hao viongozi kwa hiyo ni reflection YETU SISI. Wengi humu ni ukweli usiopingika haya maneno ya Watson yanatuuma and we are trying to be apologetic-but hata kama na yeye ameapologise-but message delivered!, ohh, Roman empire ilikwisha, wazungu wanahistoria chafu etc! Well yote ni kweli lakini kama jamaa alivyosema hatuna ingenuity katika lolote! Iweje Profesor awe mkali Harvard au MIT akirudi kwao iwe zero? ok you say mazingira? kwa nini asiyabadirishe unafikiri yale ya Harvard au MIT yalijileta? yalitafutwa!
We angalia, kikubwa katika elimu ni kutumia hiyo elimu KUBADILI mazingira ya muhusika, baada ya vita ya pili ya dunia Japani, Korea Germany zilikuwa grounded to the ashes, leo wako wapi? unafikiri USA waliweka marshall plan kusudi waendelee na kuwazidi? Kamwe msaada hauwezi kukuendeleza..China leo inapiga hatua na tuinaangalia hivi hivi, tuko nao kitandani tukiwapa raslimali zetu kama madini na mafuta kwa peremende, kesho wakiwa superpower wakaanza kudictate terms tutaanza kulalamika hivi hivi! Leo Tanzania tunapewa misaada kibao lakini utakuta zaidi ya 60% ya bajeti ni administration kununua magari nk, JK juzi alikuwa na suprus expenditure Ikulu, ulizia ni ngapi na hizo hela zimekwenda wapi? I mean mi mpaka nachoka when I happen to think of Africa. Tutajaza visingizo lukuki, ila ukweli upo pale pale. WE ARE NOT SERIOUS tunaamini uzalendo ni kuishangilia timu ya taifa na kuvaa bendera ya taifa!!
Ushauri wangu, tukubali hali halisi na tuanze moja, tujue jukumu la kuiendeleza Africa na watu wake ni letu sisi waafrikca. Leo mpaka kijiko anacholia President kinatoka Ulaya, hata wembe anaotumia babu yangu kunyoa ndevu unatoka ulaya, jamani hiyo shule inatusaidia vipi? Hata wadogo zenu huku bongo wakisikia unakuja watakwambia "mzee niletee raba kutoka mtoni" Yes, thats the truth!
Its sad kusema kwamba race yetu ni inferior lakini zama hizi tunaishi ulimwengu wa kikatili mno, hakuna kuoneana huruma! Juzi nimeattend conference moja ya WTO ungesikia fugures katika nyanja za innovation na Africa iko wapi, ungelia. na imagine wakati delegation ya Korea ina wataalamu kama ishirini na wanasisa kama wawili, ya Tanzania ilikuwa na wanasisa kama kumi na technocrats wawili! talk of seriousness! what will you negotiate?
Mwanamaulindi,
Unaongea Bologna, kwa taarifa yako university ya Timbuktu (west afrika)inaizidi hizo zote za ulaya kwa miaka.Kama nilivyosema, mzungu ameanza juzi tu,na sayansi na falsafa amechukua kutoka kwa mwafrika,ni kweli afrika sasa hivi ina matatizo, but it was not always so, ulaya vilevile, walikuwa chini hata kushinda Afrika!Na ni mwafrika ndiye aliyemtoa mzungu katika ujinga!
Tatizo kubwa la waafrika ni kwamba tumegawanyika mno(kutokana na diversity yet, na dynamics nyingi sio IQ! kwahiyo ni rahisi maadui kututwanga.Tunachoitaji ni umoja zaidi.Lakini usidanganywe na mtu yoyote kwamba 'afrika haijawahi kuwa na university n.k' huo ndio uogo unaoloishwa na mzungu huyo unayemsujudia!!!
Nyani, tatizo haliko kwenye kusema kitu ambacho ni dhahiri, tatizo liko kwenye kanuni na msingi wa kile unachosema. Nikiamka asubuhi na kusema kuwa Mungu ameniambia kuwa Wanyakyusa wote ni nusu binadamu, watu lazima wahoji kama nilichokisema kinaendana na akili na msingi wa madai yangu (huyo Mungu wa ndotoni) kina mantiki yoyote.
Inapokuja kwenye maoni ya kisayansi, mwanasayansi hasemi kitu kisichona uhakika na hawezi kutoa kauli iliyohukumu pasipo kuonesha msingi wa hukumu hiyo. Mwanasayansi akisema tofauti ya mtu mweupe na mweusi ni kiasi cha melanin na mtu ambaye hana kabisa melanin au ana upungufu mkubwa aw melanini anaitwa albino, basi Madai ya mwanasayansi huyo yanaweza kupimwa na kuoneshwa ukweli wake.
Lakini Mwanasayansi huyo huyo anapokuja na kusema kwa vile watu weupe na weusi wanatofautiana kiasi cha melanin kwenye ngozi zao basi wale ambao wana melanin kidogo (weupe) wana akili zaidi na wale wenye melanin nyingi (weusi) wana akili kidogo inabidi aoneshe msingi wa madai hayo ya kuvuka toka tofauti ya melanin na kufikia tofauti ya akili.
Sasa yawezekena anasema kweli, lakini msingi wa ukweli huo ni nini?
A. Awe amefanya utafiti wa kundi kubwa la watu wenye rangi tofauti na mahali tofauti (wakiwemo Wahindi, Wachina, Wajapani n.k ) na kupima viinihai vyao vyote vinavyohusiana na akili.
B. Ahakikishe kuwa amecontrol factors nyingine zote anapofanya vipimo hivyo
C. Awe na kundi la kulinganishia (Control group) ambalo ingawa lina rangi zile zile lakini halipatiwi vitu fulani fulani.
D. Halafu apime aone tofauti ya akili.
Atangaze matokeo ya uchunguzi wake huo kwenye chombo kinachokubalika katika suala hilo e.g The Journal of Nature, American Medical Association Journal, The Jornal on Human Genetics etc
Akifanya hivyo basi aandike mbinu, taratibu, na njia alizotumia kufuatilia utafiti huo na kuweka wazi nadharia anayotaka kuthibitisha (he must provide all the data, methodology, and necessary information) kwa wanazuoni wengine ili waweze kurudia majaribio hayo (to repeat the experiment) na wakosoe mbinu zilizotumika (kama kuna ulazima) na waboreshe mchakato mzima wa kutafuta ukweli wa nadharia yake.
Sasa, endapo wanasayansi wengine duniani wakaurudia utafiti ule ule kwa kutumia sampuli kubwa zaidi na njia zilizoboreshwa zaidi, basi ile nadharia yake inakuwa zaidi ya nadharia na inaanza kukubalika kama msimamo wa kisayansi.
Sasa, Bw. Waston anaweza kuushawishi umma wa ulimwengu kama amefanya hivyo. So far, he hasn't and that renders his conclusion baseless, his theory unfounded and at best prejudicial if not an outright absurdity!!
Yeye kasema hivi:
The 79-year-old geneticist reopened the explosive debate about race and science in a newspaper interview in which he said Western policies towards African countries were wrongly based on an assumption that black people were as clever as their white counterparts when "testing" suggested the contrary. He claimed genes responsible for creating differences in human intelligence could be found within a decade.
Sasa inavyoonekana kuna watu wanalifanyia kazi hilo swala ktk angle ya sayansi. Tusubiri tuone. Lakini mimi nasema hivi, mtu huhitaji kuwa mwanasayansi kutambua kwamba wazungu wametuzidi ktk mambo fulani fulani hasa ikija kwenye kutawala na kuyamudu mazingira tunayoishi. Na wala huhitaji kufanya utafiti wa kina kujua mtu/ watu fulani haku/hawakujaliwa kuwa na kipawa fulani. Unachohitaji ni macho na akili ya kawaida tu. Wewe mwenyewe hapo nadhani una uwezo wa kutambua mtu mwenye akili nyingi sana na mtu mwenye akili za kawaida bila ya kutumia vipimo vya sayansi na utafiti wowote ule wa kina. Kila siku hapa unammiminia sifa Nyerere kwa kuwa mtu mwenye upeo mkubwa sana. Je ulimpima akili yake kisayansi na kubainisha alikuwa na kiwango gani cha akili? Si ulitumia macho, masikio, na akili yako tu ya kuzaliwa kulitambua hilo?
Wewe mwenyewe huoni kama wazungu wametuzidi kwenye baadhi ya mambo? Afrika nzima kusini mwa jangwa la sahara (ukiondoa Afrika Kusini) ni maskini ya kutupwa. Je, umaskini huo ni wa akili au maliasili? Yaani mnataka kuniambia imetokea tu kama bahati mbaya kwamba Nchi zote hizo ziwe maskini...lakini Afrika Kusini ikaendelea sana.
Mambo mengine sio lazima uwe mwanasayansi kuyatambua. Na huyo huyo Watson angesema kwamba watu weusi wana nguvu zaidi ya watu weupe na ndio maana wanafanya vizuri sana ktk mambo ya michezo wala msingedai atuonyeshe utafiti alioufanya....Ni kweli hakuna mtu ambaye anapenda aonekane au ajulikane kuwa ni mjinga na hana akili na ndio maana wengi wanaona kama aliyoyasema ni ya kipumbavu lakini sijaona hata mmoja aliyekuja na findings za kudis-prove madai yake zaidi ya dismissal kama 'unfounded' , 'baseless', 'absurd' n.k.
Ndugu yangu Makanyanga unapoteza muda wako wewe una akili sana na wala usijisumbue kujibishana nao unaona sasa hakuna mtu alijibu ujumbe wako, hao hawataki kuelewa na hawajui nini maana ya intelijensia nigekushauri usiendelee kuchangia hii mada manake upeo wako unaonekana ni mkubwa sana ukilinganishwa na wengi humu, mimi nimechemsha....Intelligence I, is a function dependent on several variables, largely the environment E in which one was raised/brought up. The well upbringing of a child W, is a variable dependent on the same E plus the family capacity to live either poor P, good G, better B, very good VG, or Ececellent life El!
Using a mathemetical equation therefore;
I=f(E,W,....) and also W(E,G,B,VG,....,El), implying that f is a function-of-a-function (composite function). It is therefore hard to support or refute the argument on the basis of scientific evidence. However, on the social or human rights and sense of humour perspective, the evidence is 100% refutable.
Kwani source yta akili ni nini? Si ni training? Mtoto aliyekua kwenye familia maskini isiyokuwa na gari, huwezi ukamlaumu kuwa hajui kuendesha gari au ukasema kuwa haitatokea AKAWEZA kuendesha gari! Ni kwamba hajawahi kuwa trained, meaning that UKIMTRAIN, anaweza kuendesha gari.
Katika similar analog,huwezi ukasema mzungu asiyejua jina la tembo katika lugha ya kiswahili ni mjinga, au mwafrika asiyejua jina la nyoka kwa kiingereza ni mjinga pia! Nadhan tukiendelea kujadili hapa tutakuwa tuna-commit fallacy moja inaitwa ARGUMENTUM-AD-IGNORANTIUM, argument to ignorance.
Mind u, "FEELINGS OF INFERIORITY AND SUPERIORITY COMPLEX ARE THE SAME, THEY (BOTH) ORIGINATE FROM FEAR! Goodluck wana JF, kazi kwenu!
..... Mtoto aliyekua kwenye familia maskini isiyokuwa na gari, huwezi ukamlaumu kuwa hajui kuendesha gari au ukasema kuwa haitatokea AKAWEZA kuendesha gari! Ni kwamba hajawahi kuwa trained, meaning that UKIMTRAIN, anaweza kuendesha gari.
Ndugu yangu Makanyanga unapoteza muda wako wewe una akili sana na wala usijisumbue kujibishana nao unaona sasa hakuna mtu alijibu ujumbe wako, hao hawataki kuelewa na hawajui nini maana ya intelijensia nigekushauri usiendelee kuchangia hii mada manake upeo wako unaonekana ni mkubwa sana ukilinganishwa na wengi humu, mimi nimechemsha....