Wa mwisho ndiyo mshindi

Habari wanaJF,

Nnaomba tucheze mchezo unaitwa "wa mwisho ndo mshindi"......... Ni mchezo rahisi sana, unaanzisha sentensi kwenye neno la mwisho la sentensi aloandika mwenzako.

Mfano:

Ualimu Tanzania ni kazi ngumu kiasi

Kiasi ambacho kama hukuzoea maisha ya tabu, utalalama kila siku

Siku uianze vizuri bwana, ukiianza vibaya lazima utukane mwenzio

Mwenzio ni mtu ambaye mnaweka hisia zenu pamoja bila kusalitiana kama dr. Ulimboka na madkatari

Madaktari wa Tanzania wanahitaji kulipwa zaidi........ (tuendelee kwa mtindo huo wanaJF, wa mwisho ndo winner.. Karibuni sana)
zaidi ya mimi hakuna mwingine aliyepita hapa
 
Back
Top Bottom