Vyuo vikuu nchini haviwatendei haki wasabato??

Vyuo vikuu nchini haviwatendei haki wasabato??

Siyo siri, wasababto wanajifanya wana imani sana. Siku tulikuwa msafara wa viongozi kadhaa ktk wilaya yetu. Ilikuwa ijumaa. Ilipofika saa 12 jioni, mmoja wetu akasema sabato imefika hawezi kuendelea na safari, tulale hapo tulipo. Dereva akasema hakuagizwa hivyo na TO. Anatakiwa arudishe gari ofisini lina kazi nyingine jumamosi asubuhi.
Yule mwenzetu akashuka kutoka garini akatuacha tuendelee na safari. Alisafiri jumapili kwa gharama zake.
Palikuwa na ulazima kiasi kutoendelea na safari wakati ilibaki kama saa moja tu kufika nyumbani?
Imani ya kusonga ugali kwa msalaba.
IMEANDIKWA

IMETUPASA KUMTII MUNGU KULIKO WANADAMU
 
Mbona Ijumaa kuna shughuli nyingi tu hufanyika na waislam hawalalamiki?
Kwasababu QURAN inasema siku ya ijumaa ni siku ya kazi

Na hiyo hiyo Quran inasema siku ya sabato ni siku ya ibada na waliowahi kuigeuza siku ya kazi WALIGEUZWA MANYANI
 
Mungu atatumia AMRI ZAKE KUMI kuuhukumu ulimwengu huu Usemao AMRI KUMI hazina kazi, AKIFIKA KWENYE AMRI YA 4 INAYOHUSU SABATO ATAWAFYEKA TU PIA


. "Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe UZISHIKE AMRI ZAKE, Maana kwa JUMLA ndiyo IMPASAYO [WAJIBU WAKE] MTU. Kwa maana Mungu ataleta HUKUMUNI kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya." "Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. Kwa maana yeye aliyesema,
Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria [mwenye dhambi]. Semeni ninyi na kutenda kama watu WATAKAOHUKUMIWA KWA SHERIA YA UHURU Mhubiri 12:13,14; Yakobo 2:10-12.

FB_IMG_1541697525881.jpeg
 
Ila kuna baadhi ya wasabato wanafki sana.
Tulisoma na mtu chuo, ijumaa kulikua na kipindi mpaka saa moja na nusu usiku,,ikifika saa kumi na mbili kamili anatoka darasani,ila ijumaa ndo mpenzi wake ndo alikua anaenda kulala kwake anaondoka j2.

Tulikua tunamshangaa sana,
 
Siku ya Sabato ni Mali ya BWANA hatupaswi kufanya chochote ila kinacholeta Utukufu kwa Muumbaji wetu. Kwa nionavyo Graduation haileti Utukufu wowote kwa Mungu zaidi ni kwa ajiri kujifurahisha sisi wenyewe.
'"lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako"" Kut.20:10.
Mbona umeacha usitoke nje yamtupo wa jiwe
 
Pia haviwatendei haki Waislamu kwa kuendelea na shughuli zake kama kawaida siku za Ijumaa??

Tume ya uchaguzi pia haiwatendei haki wakristo kwa kufanya uchaguzi siku za Jumapili?

Kwahiyo Serikali pia haitutendei haki wanandoa maana tulipaswa tupumzike siku ya Jumatatu??

Visabato masalia vina lalamika kama makalio ya konki konki...
Si ndio nyie mnaolilia katiba mpya???
Sasa hii tuliyonayo inampa mtu nafasi ya kuabudu so inategemea wewe umemuweka mbele Mungu kiasi gani katika maisha yako.

Mi binafsi ni Msabato tangu tumboni mwa mama yangu sijaivunja sabato, shuleni, vyuoni, kazini hata kwenye biashara zangu na nimekua nikiheshimika saana kwa sababu ya uchaji Mungu wangj na kuitunza sabato katika mazingira yoote.

Tambua ukiwa na Hofu ya Mungu popote atakupigania.
 
Hao wasabato waanzishe chuo chao kikuu wawewanafundisha jumapili ijumaa na jumamosi wawe wanapumzika, hao jamaa ni wanafiki sana wenyewe wanafanyaga uovu siku hio ya jumamosi
Chuo wanacho
 
M dini haya bado siku chache niachanane nayo
 
Si ndio nyie mnaolilia katiba mpya???
Sasa hii tuliyonayo inampa mtu nafasi ya kuabudu so inategemea wewe umemuweka mbele Mungu kiasi gani katika maisha yako.

Mi binafsi ni Msabato tangu tumboni mwa mama yangu sijaivunja sabato, shuleni, vyuoni, kazini hata kwenye biashara zangu na nimekua nikiheshimika saana kwa sababu ya uchaji Mungu wangj na kuitunza sabato katika mazingira yoote.

Tambua ukiwa na Hofu ya Mungu popote atakupigania.
Amina! Wewe sasa ndo msabato wa kweli...

Msabato wa kweli huitunza sabato kwa gharama yoyote... sio kulialia na kulaumu binadamu wenzie...
 
Hawalalamiki maana dini yao inasema BAADA YA IBADA YA IJUMAA KILA MTU AENDELEE KUFANYA KAZI,

ILA WASABATO NA WAYAHUDI WANAOFATA biblia na maandiko ya MUNGU WANAAMBIWA HIVI

Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi na kutenda mambo yako yote, lakini SIKU YA SABA NI SABATO YA BWANA, MUNGU WAKO. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, … maana kwa siku siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari na vyote vilivyomo, lakini AKAPUMZKA siku ya saba. Kwa hiyo BWANA AKAIBARIKI siku ya Sabato AKAITAKASA" - Kutoka 20:8-11.
Serikali haina dini, mfano dini yangu inasema nile bata 24/7, sasa huoni nami nanyimwa haki yangu? Tuache kulia lia
 
Siyo siri, wasababto wanajifanya wana imani sana. Siku tulikuwa msafara wa viongozi kadhaa ktk wilaya yetu. Ilikuwa ijumaa. Ilipofika saa 12 jioni, mmoja wetu akasema sabato imefika hawezi kuendelea na safari, tulale hapo tulipo. Dereva akasema hakuagizwa hivyo na TO. Anatakiwa arudishe gari ofisini lina kazi nyingine jumamosi asubuhi.
Yule mwenzetu akashuka kutoka garini akatuacha tuendelee na safari. Alisafiri jumapili kwa gharama zake.
Palikuwa na ulazima kiasi kutoendelea na safari wakati ilibaki kama saa moja tu kufika nyumbani?
Imani ya kusonga ugali kwa msalaba.
Bt imam ya mtu isiwe kigezo cha kumtukana sasa
 
Back
Top Bottom