Katika ile amri ya nne Mungu anatuagiza sisi anasema:
"Ikumbeke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi na kutenda mambo yako yote, lakini SIKU YA SABA NI SABATO YA BWANA, MUNGU WAKO. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, … maana kwa siku siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari na vyote vilivyomo, lakini AKAPUMZKA siku ya saba. Kwa hiyo BWANA AKAIBARIKI siku ya Sabato AKAITAKASA" - Kutoka 20:8-11.
Mungu alipowapa watu wake zile Amri kumi, pia alieleza wazi kwamba maagizo yale yaliyotoka kinywani mwake asiwepo mwanadamu yeyote wa kuyafanyia marekebisho yeyote ili kuyafanya yawe bora zaidi au kuondoa maneno yake yeyote anapofanya uhariri wake.
"MSIONGEZE neno lolote katika yale niwaamuruyo, wala MSIPUNGUZE neno lolote, bali zishikeni amri (kumi) za BWANA, Mungu wenu ninazowapa ninyi" - (Kumbukumbu la Torati 4:2).
Mungu mwenyewe anatoa ahadi kwamba hawezi kuzibadili amri zake [kumi]:
"MIMI SITALIVUNJA agano langu, wala SITABADILI NENO LILILOTOKA MIDOMONI (MWANGU) - (Zaburi 89:34).
Biblia inaeleza waziwazi kwamba Mungu hakubadili Sabato kutoka siku ya saba kwenda ile ya kwanza ya juma.
View attachment 928000