Mkiambiwa ukweli mnadai mmetukanwa
BASI MTU WA KWANZA KUWATUKANA NI MUNGU MWENYEWE
HALAFU HAKUNA HATA AYA MOJA HAPO INAYOTOA KIBALI CHA IBADA YA JUMAPILI
UMEENDA UMEKOPI UMEPEST HATA KUPITIA UMESHINDWA
Uchunguzi wa ushahidi wa maandiko unaoonyesha wazi kwamba wale mitume hawakufanya jaribio lolote la kuibadili siku ya Mungu ya mapumziko kutoka siku ya saba kwenda ile siku ya kwanza ya juma. Agano jipya, linaitaja siku hiyo ya kwanza ya juma mara nane tu. Katika mifano hiyo yote hakuna ambapo siku ya kwanza ya juma inatajwa kuwa ni takatifu, wala hata kudokezwa kuwa tunapaswa kuitenga kama siku ya ibada. Uchunguzi uliofanywa kwa makini sana wa hayo mafungu manane yanayoitaja siku ya kwanza ya juma huonyesha matukio haya yaliyotokea Jumapili:
(1) Wanawake walikwenda kaburini siku ile ya kwanza ya juma (Mathayo 28:1).
(2) "Hata Sabato ilipokwisha" wanawake wakaanza tena kufanya shughuli zao za kidunia katika siku ile ya kwanza ya juma (Marko 16:1,2).
(3) Yesu alimtokea kwanza Mariamu Magdalena mapema siku ile kwanza ya juma (Marko 16:9).
(4) Wafuasi wa Yesu walianza tena kufanya shughuli zao katika ile siku ya kwanza juma (Luka 24:1).
(5) Mariamu alikwenda kwenye kaburi lile la Yesu na kulikuta kaburi liko tupu katika ile siku ya kwanza (Yohana 20:1).
(6) Wanafunzi wale walikusanyika mahali pamoja "kwa hofu ya Wayahudi" (si kwa ajili ya kuendesha ibada ) Katika ile siku ya kwanza ya juma (Yohana 20:19).
(7) Paulo aliwaomba washiriki wa kanisa kufanya mahesabu ya fedha zao walizopata katika ile siku ya kwanza ya juma, na "kuweka kando kiasi fulani cha fedha" kwa ajili ya maskini kule Yerusalemu (I Wakorintho 16:1,2). Kifungu hicho hakitaji mkutano wowote wa dini ambao ulifanyika.
(8) Katika Matendo 20:7 Luka anaongea habari za hotuba (mahubiri) ya Paulo aliyoitoa katika ile siku ya kwanza ya juma wakati wa mkutano ule wa kuagana ambao haukutazamiwa kufanyika. Kusema kweli, Paulo alihubiri kila siku, na mitume wale walimega mkate kila siku (Matendo 2:46).
Hakuna hata moja kati ya mafungu hayo linalodokeza ya kwamba wale mitume waliazimu kuacha kuitunza Sabato ya siku ya saba. Mitume wale hawakulitaja badiliko lolote la Sabato kutoka siku ya saba kwenda ile ya
kwanza ya juma. Hakuna ushahidi wowote ulio wazi katika Agano Jipya unaoonyesha badiliko hilo la Sabato kutoka Jumamosi, siku ya saba ya juma, kwenda Jumapili, siku ya kwanza ya juma. Badiliko hilo lilikuja baada ya siku zile za Yesu na mitume wake, kwa hiyo, yatupasa sisi kuigeukia historia ili kuona ni lini na kwa jinsi gani badiliko hilo lilitokea.
HAYA LETA ANDIKO MOJA TU LINALOONYESHA HATA MTUME WA YESU ALIFANYA IBADA SIKU YA KWANZA YA JUMA
View attachment 928067