Vyuo vikuu binafsi taabani kifedha

Japo umeweka na mzaha kwenye huu uzi ukweli ni kuwa vyuo vina hali mbaya. Na wakulaumiwa ni wamiliki wa vyuo. Pale Tumaini Iringa wamefanya ufisadi usio na mfano na sasa nadhani ni mwaka wafanyakazi hawajalipwa salary. Waliofisadi hawajashitakiwa hata kwa balozi. Ovyo sana na misalaba yao vifuani
 
Hujajibu swali, (narudia) nitajie wanasayansi wawili tu waliosoma kwenye vyuo vya kanisa katoliki. Hilo tu
 
SAUT wamefyatua vyuo kama matembele. Sipati picha pale Chuo cha msamvu itakuaje.?
Kwa kweli hata mimi sijafurahishwa na kanisa kufungua matawi kama uyoga. Sijui hapa kanisa walikosea wapi. Chuo cha SAUT mwanza kilikuwa na nguvu sana. Angalau wangeishia matawi mawili tu nchi nzima ingeeleweka. Sasa matawi karibu kila mkoa mkubwa wa Tanzania? Hapana!!!!!
 
Brother if your first degree results match to GPA of 3.8 standard going up, sidhani kama ungekuwa unalalama kuwa hupati ajira UDSM, OUT, SUA, Mzumbe na kwingineko kule kwenye taasisi za serikali. Nafasi za ajira ziko bwerere ila ufaulu mbovu sana kwa watahiniwa wengi nchini. Someni kwa bidii na focus ya field sahihi ya kupita.
 
Kila Baba Mhashamu Askofu anataka Chuo Kikuu jimboni mwake. Fikiria Jimbo la Mbinga nao wanataka Chuo Kikuu Cha Mtakatifu Kizito Litumbandyoso - Mbinga.
 
Undergraduate admission mwaka huu wa masomo 2019/2020/sijui itakuaje. Maana mitoto inakimbilia UDOM tu
 
St john dodoma mbona ipo safi tuu. Naona mwaka jana na mwaka huu admission wanajaza na wapo vizuri wewe unakwama wapi[emoji23]
Saut Arusha ni chuo cha kipuuzi sana....Imagine chuo kipo kilombero,makelele asubuhi mpk jioni,hakuna hostel rafiki zaidi ya vile vyumba vya kanisa pale havitoshi hata watu hamsini,........hamna hata kiwanja cha mchezo mmoja hapa hata kurefresh mind ni shida,mpaka wanachuo wakapigane huko mjini wapate pa kuchezea michezo trna kwa taaabu,....saut arusha inamfaa sana mtu anayesoma evening classes sio full time...even though nawasifu pia kitaaluma wapo vizuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…