Vyombo vya dola vimeipora Ikulu kutoka kwa wananchi

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,606
29,755
Nikiwasalimu itikieni

Enzi za Mwalimu, Ikulu ya Dar ilikuwa na uzio wa michongoma na maua sambamba na uzio wa wavu eneo lenye wanyamapori wanaofugwa Ikulu. Enzi hizo tuliweza kuona uzuri na umaridadi wa Ikulu yetu. Wapita njia hususan wageni waliweza kutembea pembeni ya uzio wa Ikulu bila kusumbuliwa

Alipokuja mzee Mwinyi alijenga ukuta kuzunguka ikulu, lakini haukuwa ukuta wa kumnyima mpitanjia kujionea umaridadi wa jengo letu linaloendeshwa na kutunzwa na kodi zetu.

Alikuja mzee Mkapa ambaye hakukuwa na heka heka nyingi bali aliruhusu wapitanjia kutembea pembezoni mwa uzio huku wakijionea ufahari wa Ikulu yetu.

Ukarabati mkubwa wa Ikulu (badala ya kuanza ujenzi wa Dodoma) ulifanyika chini ya Jakaya, tukaanza kuona mabadiluko machache, upande wa barabara ya Barack Obama ilianza kufungwa usiku kuzuia magari kupita. Lakini wapitanjia waliruhusiwa kupita. Upande wa Wanyama wanaofugwa Ikulu ukawekwa Uzio kuziba wanyama wasionekane na wapitanjia. Tulianza kupata mashaka labda wameuzwa kwa sababu wale wanyama walipungua sana kabla hakujazibwa kabisa wasionekane....

Kasheshe alipokuja mpendwa wetu JPM, barabara ya Barack Obama ikafungwa kabisa hakuna raia kupita, na hata wapita njia walizuiwa, kibaya zaidi hadi sasa raia anayetembea nje ya ukuta wa Ikulu anashughulikiwa kikatili na wale walinzi waliovaa makirikiri. Hali hii imedumu hadi kwa rais wa sasa. Tunachojiuliza Watanzania kadhaa ni kwamba, kuna tishio gani la usalama kiasi ya kuwekwa makatazo hayo? Au kuna biashara gani zinaendelea Ikulu kiasi kwamba wapitanjia wanaweza kuiba siri?

Inaonesha kuwa Serikali imeweka alert dhidi ya raia wake na haina imani nao na kibaya zaidi, vyombo vya dola vimejimilikisha jengo na mandhari ya Ikulu huku vikijua wazi kabisa kuwa ile ni kodi za wananchi.

Kama endapo lengo ni ulinzi. Watafakari uwezo wao wa kulinda lile jengo bila kujenga hofu kwa wapitanjia .

Lakini, kitu muhimu ni kwamba, kadiri wanavyoiweka Ikulu mbali na wananchi ndivyo wwnavyomjengea mazingira magumu sana mkazi namba moja pale Ikulu hadi kupelekea kupoteza umaarufu. Kusimika mabango na public mentioning ya rais ni utamaduni uliobuniwa kuhakikisha anapata umaarufu wa LAZIMA badala ya kufanya mambo ya msingi zaidi.

Natoa rai kwa wwhusika, wasipore ama kuitenganisha Ikulu na Tanzania. Kama wanaona ni muhimu kufanya hivyo basi wabuni miradi ya uwekezaji ya kuiendesha Ikulu na wasitegemee kodi zetu.

Jambo la kuzingatia. Ikulu ya Chamwino ina privacy nzuri na maridhawa kwa rais, itoshe kwa yeye kufanyiakazi na kuishi kule na aruhusu barabara zilizokuwa zinapitika zamani kuelekea na kutoka Kivukoni kutumika.
 
Nikiwasalimu itikieni

Enzi za Mwalimu, Ikulu ya Dar ilikuwa na uzio wa michongoma na maua sambamba na uzio wa wavu eneo lenye wanyamapori wanaofugwa Ikulu. Enzi hizo tuliweza kuona uzuri na umaridadi wa Ikulu yetu. Wapita njia hususan wageni waliweza kutembea pembeni ya uzio wa Ikulu bila kusumbuliwa

Alipokuja mzee Mwinyi alijenga ukuta kuzunguka ikulu, lakini haukuwa ukuta wa kumnyima mpitanjia kujionea umaridadi wa jengonletu linaloendeshwa na kutunzwa na kodi zetu.

Alikuja mzee Mkapa ambaye hakukuwa na heka heka nyingi bali aliruhusu wapitanjia kutembea pembezoni mwa uzio huku wakijionea ufahari wa Ikulu yetu.


Ukarabati mkubwa wa Ikulu (badala ya kuanza ujenzi wa Dodoma) ulifanyika chini ya Jakaya, tukaanza kuona mabadiluko machache, upande wa barabara ya Barack Obama ilianza kufungwa usiku kuzuia magari kupita. Lakini wapitanjia waliruhusiwa kupita. Upande wa Wanyama wanaofugwa Ikulu ukawekwa Uzio kuziba wanyama wasionekane na wapitanjia. Tulianza kupata mashaka labda wameuzwa kwa sababu wale wanyama walipungua sana kabla hakujazibwa kabisa wasionekane....

Kasheshe alipokuja mpendwa wetu JPM, barabara ya Barack Obama ikafungwa kabisa hakuna raia kupita, na hata wapita njia walizuiwa, kibaya zaidi hadi sasa raia anayetembea nje ya ukuta wa Ikulu anashughulikiwa kikatili na wale walinzi waliovaa makirikiri. Hali hii imedumu hadi kwa rais wa sasa. Tunachojiuliza Watanzania kadhaa ni kwamba, kuna tishio gani la usalama kiasi ya kuwekwa makatazo hayo? Au kuna biashara gani zinaendelea Ikulu kiasi kwamba wapitanjia wanaweza kuiba siri?

Inaonesha kuwa Serikali imeweka alert dhidi ya raia wake na haina imani nao na kibaya zaidi, vyombo vya dola vimejimilikisha jengo na mandhari ya Ikulu huku vikijua wazi kabisa kuwa ile ni kodi za wananchi.

Kama endapo lengo ni ulinzi. Watafakari uwezo wao wa kulinda lile jengo bila kujenga hofu kwa wapitanjia .

Lakini, kitu muhimu ni kwamba, kadiri wanavyoiweka Ikulu mbali na wananchi ndivyo wwnavyomjengea mazingira magumu sana mkazi namba moja pale Ikulu hadi kupelekea kupoteza umaarufu. Kusimika mabango na public mentioning ya rais ni utamaduni uliobuniwa kuhakikisha anapata umaarufu wa LAZIMA badala ya kufanya mambo ya msingi zaidi.

Natoa rai kwa wwhusika, wasipore ama kuitenganisha Ikulu na Tanzania. Kama wanaona ni muhimu kufanya hivyo basi wabuni miradi ya uwekezaji ya kuiendesha Ikulu na wasitegemee kodi zetu.

Jambo la kuzingatia. Ikulu ya Chamwino ina privacy nzuri na maridhawa kwa rais, itoshe kwa yeye kufanyiakazi na kuishi kule na aruhusu barabara zilizokuwa zinapitika zamani kuelekea na kutoka Kivukoni kutumika.
huo utabaki kuwa mtazamo na nadharia za wanataluma na wadadisi wa masuala ya kisiasa.

Lakini ukweli utabaki palepale, dola, ikulu na vyote vilivyomo ndani yake ni mali ya wananchi na umma wa waTanzania wote.
 
huo utabaki kuwa mtazamo na nadharia za wanataluma na wadadisi wa masuala ya kisiasa.

Lakini ukweli utabaki palepale, dola, ikulu na vyote vilivyomo ndani yake ni mali ya wananchi na umma wa waTanzania wote.
Sasa si uende uingie ndugu kuliko kulialia hapa!! Mbona mnatetea mada za kijinga namna hii?

Hivi hamjui kuwa baada ya Septermber 11, security ya nchi na viongizi wa dunia ilibadilika by 360°?
 
Sasa si uende uingie ndugu kuliko kulialia hapa!! Mbona mnatetea mada za kijinga namna hii?

Hivi hamjui kuwa baada ya Septermber 11, security ya nchi na viongizi wa dunia ilibadilika by 360°?
Mkapa akiwa bado raisi wakati sept 11 inatokea hakujifungia hivyo, na aliyefuata bwana Kikwete naye hakufanya hivyo.
Huko ambapo sept 11 ilitokea bado watu wanaingia ikulu hadi kupiga picha ni kama utalii fulani.

Sijui kwanini viongozi wa kiafrika wanaona ufahari kujitenga na wananchi.

Sisemi watu waingie hovyo hovyo, ila sasa kapuku mie kupita nje barabarani kuna shida gani hadi wanidunde
 
Sasa si uende uingie ndugu kuliko kulialia hapa!! Mbona mnatetea mada za kijinga namna hii?

Hivi hamjui kuwa baada ya Septermber 11, security ya nchi na viongizi wa dunia ilibadilika by 360°?
niikaingie mara ngap,
mimi naieleza nionavyo mimi na wew unaeleza udhanivyo.

na by the way huu ni mtazamo wangu binafsi.
hiyo habari ya mbona mnatetea au hivi hamjui n.k si sawa usiwahusishe wasiohusika kwenye mawazo yangu.

ni address mimi pekee.

Dollar, Ikulu na vyote vilivyomo ndani yake ni mali ya wananchi na waTanzania wote.
 
niikaingie mara ngap,
mimi naieleza nionavyo mimi na wew unaeleza udhanivyo.

na by the way huu ni mtazamo wangu binafsi.
hiyo habari ya mbona mnatetea au hivi hamjui n.k si sawa usiwahusishe wasiohusika kwenye mawazo yangu.

ni address mimi pekee.

Dollar, Ikulu na vyote vilivyomo ndani yake ni mali ya wananchi na waTanzania wote.
Hii mada haina hadhi ya kuwa JF, mambo ya Facebook haya. I logoff
 
Yes mkuu wakati TISS ina heshima na adabu, ikulu ilikua sehemu ya kawaida kuitembelea, eneo mbele ya ikulu wananchi waliruhusiwa kupunga upepo, Ile barabara ilikua wazi 24 hrs, walivyoingia madikiteta ikulu imebadilika sana, tuelewe TISS ile ilimpeleka president Nyerere karibu kabisa na makaburu (mazishi ya president Khama) na kumrudisha salama president wetu Tanzania, hawa TISS wa sasa wamejaa vitisho kwa waoga waliojaa sasa Tanzania
 
Nikiwasalimu itikieni

Enzi za Mwalimu, Ikulu ya Dar ilikuwa na uzio wa michongoma na maua sambamba na uzio wa wavu eneo lenye wanyamapori wanaofugwa Ikulu. Enzi hizo tuliweza kuona uzuri na umaridadi wa Ikulu yetu. Wapita njia hususan wageni waliweza kutembea pembeni ya uzio wa Ikulu bila kusumbuliwa

Alipokuja mzee Mwinyi alijenga ukuta kuzunguka ikulu, lakini haukuwa ukuta wa kumnyima mpitanjia kujionea umaridadi wa jengonletu linaloendeshwa na kutunzwa na kodi zetu.

Alikuja mzee Mkapa ambaye hakukuwa na heka heka nyingi bali aliruhusu wapitanjia kutembea pembezoni mwa uzio huku wakijionea ufahari wa Ikulu yetu.


Ukarabati mkubwa wa Ikulu (badala ya kuanza ujenzi wa Dodoma) ulifanyika chini ya Jakaya, tukaanza kuona mabadiluko machache, upande wa barabara ya Barack Obama ilianza kufungwa usiku kuzuia magari kupita. Lakini wapitanjia waliruhusiwa kupita. Upande wa Wanyama wanaofugwa Ikulu ukawekwa Uzio kuziba wanyama wasionekane na wapitanjia. Tulianza kupata mashaka labda wameuzwa kwa sababu wale wanyama walipungua sana kabla hakujazibwa kabisa wasionekane....

Kasheshe alipokuja mpendwa wetu JPM, barabara ya Barack Obama ikafungwa kabisa hakuna raia kupita, na hata wapita njia walizuiwa, kibaya zaidi hadi sasa raia anayetembea nje ya ukuta wa Ikulu anashughulikiwa kikatili na wale walinzi waliovaa makirikiri. Hali hii imedumu hadi kwa rais wa sasa. Tunachojiuliza Watanzania kadhaa ni kwamba, kuna tishio gani la usalama kiasi ya kuwekwa makatazo hayo? Au kuna biashara gani zinaendelea Ikulu kiasi kwamba wapitanjia wanaweza kuiba siri?

Inaonesha kuwa Serikali imeweka alert dhidi ya raia wake na haina imani nao na kibaya zaidi, vyombo vya dola vimejimilikisha jengo na mandhari ya Ikulu huku vikijua wazi kabisa kuwa ile ni kodi za wananchi.

Kama endapo lengo ni ulinzi. Watafakari uwezo wao wa kulinda lile jengo bila kujenga hofu kwa wapitanjia .

Lakini, kitu muhimu ni kwamba, kadiri wanavyoiweka Ikulu mbali na wananchi ndivyo wwnavyomjengea mazingira magumu sana mkazi namba moja pale Ikulu hadi kupelekea kupoteza umaarufu. Kusimika mabango na public mentioning ya rais ni utamaduni uliobuniwa kuhakikisha anapata umaarufu wa LAZIMA badala ya kufanya mambo ya msingi zaidi.

Natoa rai kwa wwhusika, wasipore ama kuitenganisha Ikulu na Tanzania. Kama wanaona ni muhimu kufanya hivyo basi wabuni miradi ya uwekezaji ya kuiendesha Ikulu na wasitegemee kodi zetu.

Jambo la kuzingatia. Ikulu ya Chamwino ina privacy nzuri na maridhawa kwa rais, itoshe kwa yeye kufanyiakazi na kuishi kule na aruhusu barabara zilizokuwa zinapitika zamani kuelekea na kutoka Kivukoni kutumika.
NYERERE ALIWEKA WANYAMA IKULU ILI ANGALAU WANANCHI WA DAR WAWAONE LAKINI ALIPOINGIA YULE MZEE KATILI AKAREFUSHA UKUTA NA KUHAMISHA WANYAMA
 
Yes mkuu wakati tiss ina heshima na adabu, ikulu ilikua sehemu ya kawaida kuitembelea, eneo mbele ya ikulu wananchi waliruhusiwa kupunga upepo, Ile barabara ilikua wazi 24 hrs, walivyoingia madikiteta ikulu imebadilika sana,tuelewe tiss ile ilimpeleka president Nyerere karibu kabisa na makaburu (mazishi ya president Khama)na kumrudisha salama president wetu Tanzania, hawa TISS wa sasa wamejaa vitisho kwa waoga waliojaa sasa Tanzania
Sereste Ian Khama. Kumbe kuna kisa cha mwalimu sijakijua. Aisee. Mkuu em tupe kisa hicho aisee. I once saw a movie ya sir Sereste Ian Khama jinsi alivyopambana kuoa mke UK huku ndugu wa ukoo wakawa wanagoma.

Pale white house upande fulani nadhan wamegawanya kwa wings kuna sehem wing fulan is open to public kupiga picha. As we know social media zinasaidia sana kupromote kitu.
 
Mbona hawa viongozi wakienda Ulaya Na Marekani ulinzi wao huwa si mkali sana Kama wanaoupataga Tanzania?
Je hatari zaidi ya usalama wao huwa ipo Ndani ya nchi au nje ya nchi?
Huwa naona wanajiachia tu Na kujichanganya Na akina Mambe Kimbambi Na wako simple Kabisa... iweje wahofie sana usalama wao ndani ya nchi kuliko nje ya nchi?
Ndani ya nchi msafara zaidi ya Magari 50, nje ya nchi msafara si zaidi ya magari matatu... Hii imekaaje?
 
Yes mkuu wakati tiss ina heshima na adabu, ikulu ilikua sehemu ya kawaida kuitembelea, eneo mbele ya ikulu wananchi waliruhusiwa kupunga upepo, Ile barabara ilikua wazi 24 hrs, walivyoingia madikiteta ikulu imebadilika sana,tuelewe tiss ile ilimpeleka president Nyerere karibu kabisa na makaburu (mazishi ya president Khama)na kumrudisha salama president wetu Tanzania, hawa tiss wapumbavu wa sasa wamejaa vitisho kwa waoga waliojaa sasa Tanzania
Mkuu umetema madini ya Tanzanite bigly bigly

Unclassify the classfied pls
 
Mbona hawa viongozi wakienda Ulaya Na Marekani ulinzi wao huwa si mkali sana Kama wanaoupataga Tanzania?
Je hatari zaidi ya usalama wao huwa ipo Ndani ya nchi au nje ya nchi?
Huwa naona wanajiachia tu Na kujichanganya Na akina Mambe Kimbambi Na wako simple Kabisa... iweje wahofie sana usalama wao ndani ya nchi kuliko nje ya nchi?
Ndani ya nchi msafara zaidi ya Magari 50, nje ya nchi msafara si zaidi ya magari matatu... Hii imekaaje?
Ukiwa president Tanzania unageuka kuwa mungu mtu. Na mungu huyo lazima alindwe sana dhidi ya pepo wachafu wanaoonekana wakirandaranda karibu yake🤣
 
Sasa si uende uingie ndugu kuliko kulialia hapa!! Mbona mnatetea mada za kijinga namna hii?

Hivi hamjui kuwa baada ya Septermber 11, security ya nchi na viongizi wa dunia ilibadilika by 360°?
Marekani penyewe waliposhambuliwa hiyo Sept 11, hamna uzio Hadi Leo,

Ninyi ndio walinzi mnaozuga lindoni Kwa mkwara mkali boss akiwa hajalala,ikifika mida flani usiku mzito, mnarudi kulala Kwa wake zenu!!
 
Mkapa akiwa bado raisi wakati sept 11 inatokea hakujifungia hivyo, na aliyefuata bwana Kikwete naye hakufanya hivyo.
Huko ambapo sept 11 ilitokea bado watu wanaingia ikulu hadi kupiga picha ni kama utalii fulani.

Sijui kwanini viongozi wa kiafrika wanaona ufahari kujitenga na wananchi.

Sisemi watu waingie hovyo hovyo, ila sasa kapuku mie kupita nje barabarani kuna shida gani hadi wanidunde
Ukiona hivyo ujue huo ni ushahidi kuwa viongozi hao wanaingia madarakani bila ridhaa ya wananchi, hivyo wanahofu nao maana wako madarakani bila ridhaa Yao.
 
Mkuu umetema madini ya Tanzanite bigly bigly

Unclassify the classfied pls
Yeah mkuu,facts lazima zibakie hivyo, uoga gani uliompata mpangaji mkuu wa magogoni kuamua kuifunga ile barabara mbele ya ikulu?,mimi ninayetoka kinondoni kwenda ferry lazima nifanye twist n turn kuifikia ferry, kisa dikiteta mmoja kaamua ya kuamua!!,wote tutakufa tu
 
Back
Top Bottom