Imefika mahali tujadili mambo bila kuweka vyama vyetu mbele,
CAG ndiye mwenye jukumu la ukaguzi na kimsingi amekwisha toa sababu za kushindwa kukagua ambayo ni kutopewa fungu la ukaguzi wa vyama vya siasa.
Binafsi nimemuunga mkono
Zitto katika harakati za kuhakikisha ukaguzi unafanyika na ukweli unajulikana lakini wakati tunaunga mkono hili swala mwanzoni kabisa hapa hapa JF tukiamini ni swala jema kiuwajibikaji siku zinavyokwenda linaanza kuleta sura za kisiasa na hili ndio tatizo nchi hii.
Tatizo liko wazi na kimsingi CAG ametoa sababu na ilipaswa tujue hatua gani zichukuliwe kurekebisha huu udhaifu lakini naona kuna taswira inajengwa kutuhumu vyama hasa kuna chama kimelengwa very specific.
Lazima vyama vikaguliwe na CAG na tuache siasa kwenye mambo ya msingi maana tuna sheria na miongozo inayotosha kuongea na si kuanza kutuhumu tu na kuishia kuchanganya wananchi wasioelewa ukweli halisi.