Vyama vya siasa vipewe muda vikamilishe Mahesabu-PAC

Vyama vya siasa vipewe muda vikamilishe Mahesabu-PAC

Kuna uzi mwingine hapa JF unasema kuwa Msajili wa vyama vya siasa amesema ataendelea kutoa ruzuku. Sasa hawa mwananchi wanatuambia PAC 'imemtaka' Msajili aendelee kuvipitia ruzuku vyama vya siasa!

Nani alimuwahi mwenziwe?

Awali PAC ilikurupuka kwa kutoa "maelekezo" kwa msajili kusitisha ruzuku kwa vyama.

Baada ya wadau kuielimisha PAC juu ya mipaka ya madaraka Yao,na baada ya kubaini kwamba msajili alikuwa Makini sana kabla ya kuitikia wito wa kusitisha ruzuku,ndipo sasa PAC ilatambua kuwa ilikuwa imepiga wrong number!

Katika kujikosha na kutaka kufuta madhambi iliyokuwa imeyafanya,PAC imeluja sasa na kauli mpya ya kumtaka msajili aendelee kuvipatia vyama ruzuku.

Kimsingi bado PAC imechemka tena kwaluwa mamlaka Yao yanaishia kwenye kuvipa muda vyama ili viwe vimekaguliwa hadi hiyo January 2014
Suala la kuendelea au kutokuendelea kupata ruzuku linabaki chini ya mamlaka ya msajili,na PAC wasiendelee kujifanya wao wana mamlaka hayo.

Jambo la msingi ambalo mimi nilitarajia kulisikia Leo kutoka PAC ni namna ya kuiwezesha ofisi ya CAG kifedha ili iweze kufanya ukaguzi wa mahesabu ya vyama kwakuwa imeelezwa tangu awali kuwa ofisi ya CAG imeshindwa kufanya ukaguzi wa mahesabu ya vyama kwakuwa hawana bajeti ya kazi hiyo. Lakini naona Hilo hawajalizungumza,na hapo ndipo nataka kulibaliana na wadau kuwa PAC inafanya siasa badala ya kazi za kitaalamu na kisheria.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Ninngemshangaa Jaji Mutungi angekubali harakati za watu binfs kwenye mambo ya kikanuni na sheria,aibu sasa kwa waliotayari kunyongwa ktk kutetea mambo Yao binafsi.
 
Dr. Slaa amepotea mitandaoni kwa sababu yuko busy kurekebisha mahesabu yaonekane safi!!!

Uzalendo mgumu...

.....Ama kweli "mti wenye matunda ndio hurushiwa mawe" yaani Magamba hayaongelewi kabisa na yametulia kimya utadhani hayapo.
1. yamekula zaidi ya Bil 50 wakati CHADEMA hata bil 10 hazifiki.
2. Hayajakaguliwa wala kupeleka taarifa ya mahesabu yao kwa msajili wa vyama.
3. Hawajamtaarifu mapato yeyote nje ya ruzuku kutoka kwa marafiki zao au EPA, MEREMETA, KAGODA, DEEPGREEN nk.
Lakini ajabu wote humu habari ni juu ya CHADEMA na PAC tu! chama ambacho angalau kimewasilisha mahesabu yaliyokaguliwa (japo si na CAG kutokana na ukapa wa ofisi ya CAG) na chama ambacho kimeshatoa tamko kuwa kipo tayari kukaguliwa na CAG tena si kwa pesa za ruzuku tu, bali hata kinazopata kutokana na vyanzo vingine.
Hii ni uthibitisho kwamba tumaini la watanzania wote including akina ZeMarcopolo kwa sasa ni CHADEMA.
 
Kamati ya Bunge ya Mahesabu ya serikali PAC imetoa tamko la kuridhia vyama kukamilisha taarifa za fedha na kukabidhi kwa CAG ifikapo Januari 2014.

Hii ni baada ya Kamati hiyo kukutana na msajili wa vyama vya siasa Jaji Francis Mutungi leo jijini Dar es Salaam.

Pia kamati hiyo imemtaka msajili wa vyama kuendelea kuvipatia Ruzuku vyama hivyo.

Source:Mwananchi Breaking News
ACHA KUPOTOSHA Umma PAC haijaagiza kitu kama hicho..Najua ww upo CHADEMA unaumia sana kuona zitto anawatwanga wazimawazima.Wezi wakubwa nyie.
 
Kuna uzi mwingine hapa JF unasema kuwa Msajili wa vyama vya siasa amesema ataendelea kutoa ruzuku. Sasa hawa mwananchi wanatuambia PAC 'imemtaka' Msajili aendelee kuvipitia ruzuku vyama vya siasa!

Nani alimuwahi mwenziwe?

Mkuu FJM Nadhani kamati imefanya hivi kuweka kumbukumbu sawa kwa sababu siku ile tulimsikia Zitto akisema ameamuru kuzuiliwa Ruzuku kwa vyama vyote!

Nadhani hapa Zitto alikosea na kamati yote kuonekana inakurupuka bila kufuata sheria.
 
Last edited by a moderator:
Kamati ya PAC ilikurupuka tangu mwanzo na ilipaswa kukaa kimya na kuacha ngonjera zenye kauli gongana kwenye media.

Kwa nini.

1. Kamati ilipaswa kumbana CAG kukagua mahesabu ya vyama na si kumuagiza msajili kuzuia ruzuku eti kwa kuwa vyama havija kaguliwa mahesabu yao. Msajili wa vyama na mkaguzi mkuu wa serikali ni mamlaka mbili tofauti. Ili kupata uhalali wa kuzuia ruzuku kupitia ofisi ya msajili ni lazima ujue kuwa mahesabu yamekaguliwa na CAG na si kukurupuka.

2. Ilikuwa si sahihi kwa kamati ya PAC labda kwa malengo maalumu kuwatishia makatibu wa vyama kuwa itawaita kwenye kamati na kuwahoji kuhusu matumizi ya ruzuku za vyama au hata kuwapeleka selo kwa siku 7. Chadema kwa mfano, mwenye mamlaka ya kuhojiwa kuhusu ruzuku ya chama ni baraza la wadhamini wa chama na sio katibu mkuu Slaa.

3. Kamati inaonekana kabisa kuwa ilikuwa na ajenda yake juu ya ruzuku, na ajenda hiyo needless to say haikuwa ajenda ya kamati bali ajenda ya mtu binafsi mwenye remote control ya kamati ndio maana hata target ya kamati nzima ikawa butu.

Kuna haja ya kamati kujitafakari upya na kuiga mbinu ya wawindaji mahiri wa ndege mwitu. Kulenga shabaha kwa umakini kisha kuachia mpira wa manati; sio kuachia mpira wa manati kisha unalenga shabaha.
 
ACHA KUPOTOSHA Umma PAC haijaagiza kitu kama hicho..Najua ww upo CHADEMA unaumia sana kuona zitto anawatwanga wazimawazima.Wezi wakubwa nyie.

Wewe kijana huna hadhi ya kubishana na mimi.
Na wala usijifanye una haki ya kutoa habari kuliko watu wengine.

Ninachokushauri nenda katubu kwa watu uliowalipua Arusha!
 
Ukweli ni kwamba KAMATI YA PAC inayoendeshwa na Zitto imemtaka CAG kuhakikisha anavifanyia ukaguzi wa kina vyama vyote kwa muda wa miaka minne yote vinavyodaiwa kutofanyiwa mahesabu ya mapato yao.
CAG akishakagua kufikia January ahakikishe anakabidhi ripoti kwa kamati ya zitto PAC.
SWala analoliongelea molemo hapa ni uongo na unafiki mkubwa.CHADEMA mbona mnalialia sana?Zitto nyonga hao
 
Wewe kijana huna hadhi ya kubishana na mimi.
Na wala usijifanye una haki ya kutoa habari kuliko watu wengine.

Ninachokushauri nenda katubu kwa watu uliowalipua Arusha!
wewe mtoto nenda kavar nepi huko.Mbona unapotosha umma hivyo?Zitto kawashika patamu nyie wote wauza madawa lazima make.
PAC inadeal na chadema mwanzo mwisho kwa sababu ndio mnaongoza kulialia hapa Tanzania kumbe wezi wakubwa wa Ruzuku.
 
mbona kuna sehemu inaonesha jaji mtungi hana mawasiliano na CAG? MAANA ANASEMA ANA SUBIRI RIPORT ZA VYAMA WALIZO WASILISHA KWA CAG?

LAKINI TUTAPIGA KELELE BURE KAMA TUTAENDELEA KU AUDIT WATU TUSIO WAPANGIA MATUMIZI?
 
Kwa mtazamo wangu Zitto na PAC hawakukurupuka na wanajua matokeo ya kauli zao.

Baada ya lile tamko, kila aliyekuwa akihusika alitoa kauli na public ikajua kuwa hakuna chama kilichokaguliwa na CAG hadi sasa. Wote hesabu zao zimekaguliwa na auditors ambao hata independence yao hakuna anaejua hadi sasa.

Big up Zitto na kamati yako, fruits tunaanza kuziona, deadline is already set na CAG huenda akawa asign independent auditors going forward.

Ukisiakia paaaaaaaaa, ujue limempata! Acha wabwabwaje sasa!
 
Mkuu kuna mahali nimesema:


Wakurupukaji wajifunze.Tulisema PAC ilitakiwa ku-deal na CAG na Ofisi ya Msajili kwanza.

Hizi tabia za kukurupuka kama chafya ndizo zinazoharibu na kushusha kiwango cha siasa zetu

Ilimradi mtu una ajenda yako binafsi na mapovu ya kutosha basi unaitumia fursa kwa namna yoyote ile.

Hoja hazijengwi kisomi bali kwa jazba na chuki binafsi tu.Mbaya zaidi inapofanywa na wanasiasa wasomi

Haya sasa nashauri turudi kwenye mada za msingi.Katiba Mpya!
muuza sumu na mtembea na tindikali naona unatetea buku tatu zako hapa za Slaa
 
Imefika mahali tujadili mambo bila kuweka vyama vyetu mbele,

CAG ndiye mwenye jukumu la ukaguzi na kimsingi amekwisha toa sababu za kushindwa kukagua ambayo ni kutopewa fungu la ukaguzi wa vyama vya siasa.

Binafsi nimemuunga mkono Zitto katika harakati za kuhakikisha ukaguzi unafanyika na ukweli unajulikana lakini wakati tunaunga mkono hili swala mwanzoni kabisa hapa hapa JF tukiamini ni swala jema kiuwajibikaji siku zinavyokwenda linaanza kuleta sura za kisiasa na hili ndio tatizo nchi hii.

Tatizo liko wazi na kimsingi CAG ametoa sababu na ilipaswa tujue hatua gani zichukuliwe kurekebisha huu udhaifu lakini naona kuna taswira inajengwa kutuhumu vyama hasa kuna chama kimelengwa very specific.

Lazima vyama vikaguliwe na CAG na tuache siasa kwenye mambo ya msingi maana tuna sheria na miongozo inayotosha kuongea na si kuanza kutuhumu tu na kuishia kuchanganya wananchi wasioelewa ukweli halisi.
...mkuu hicho ndicho chama pekee kilicho Tumaini la watanzania wote. Nani wa kukizungumzia kile chama cha MIHADARATI tena? We huoni hata akina ZeMarcopolo hawana time nacho tena? kila wakilala wakiamka ni Dr Slaa, CHADEMA hawana kingine kwenye ubongo wao kwa sasa.
 
Huo ndio ukweli na sio upotoshaji wa Akina Molemo na Ben saanane vijana wa bukutatu tatu za Slaa ma Mbowe
Kwa mtazamo wangu Zitto na PAC hawakukurupuka na wanajua matokeo ya kauli zao.kk

Baada ya lile tamko, kila aliyekuwa akihusika alitoa kauli na public ikajua kuwa hakuna chama kilichokaguliwa na CAG hadi sasa. Wote hesabu zao zimekaguliwa na auditors ambao hata independence yao hakuna anaejua hadi sasa.

Big up Zitto na kamati yako, fruits tunaanza kuziona, deadline is already set na CAG huenda akawa asign independent auditors going forward.

Ukisiakia paaaaaaaaa, ujue limempata! Acha wabwabwaje sasa!
 
chadema wanahaha na zitto as if kaua,Kumbe wanatambua kuwa ni wezi wakubwa na wamekuwa wakikwepa kufajyiwa mahesabu.
...mkuu hicho ndicho chama pekee kilicho Tumaini la watanzania wote. Nani wa kukizungumzia kile chama cha MIHADARATI tenaq? We huoni hata akina ZeMarcopolo hawana time nacho tena? kila wakilala wakiamka ni Dr Slaa, CHADEMA hawana kingine kwenye ubongo wao kwa sasa.
 
Kamati ya PAC ilikurupuka tangu mwanzo na ilipaswa kukaa kimya na kuacha ngonjera zenye kauli gongana kwenye media.

Kwa nini.

1. Kamati ilipaswa kumbana CAG kukagua mahesabu ya vyama na si kumuagiza msajili kuzuia ruzuku eti kwa kuwa vyama havija kaguliwa mahesabu yao. Msajili wa vyama na mkaguzi mkuu wa serikali ni mamlaka mbili tofauti. Ili kupata uhalali wa kuzuia ruzuku kupitia ofisi ya msajili ni lazima ujue kuwa mahesabu yamekaguliwa na CAG na si kukurupuka.

2. Ilikuwa si sahihi kwa kamati ya PAC labda kwa malengo maalumu kuwatishia makatibu wa vyama kuwa itawaita kwenye kamati na kuwahoji kuhusu matumizi ya ruzuku za vyama au hata kuwapeleka selo kwa siku 7. Chadema kwa mfano, mwenye mamlaka ya kuhojiwa kuhusu ruzuku ya chama ni baraza la wadhamini wa chama na sio katibu mkuu Slaa.

3. Kamati inaonekana kabisa kuwa ilikuwa na ajenda yake juu ya ruzuku, na ajenda hiyo needless to say haikuwa ajenda ya kamati bali ajenda ya mtu binafsi mwenye remote control ya kamati ndio maana hata target ya kamati nzima ikawa butu.

Kuna haja ya kamati kujitafakari upya na kuiga mbinu ya wawindaji mahiri wa ndege mwitu. Kulenga shabaha kwa umakini kisha kuachia mpira wa manati; sio kuachia mpira wa manati kisha unalenga shabaha.

PAC inatimiza wajibu wake wa kuhakikisha fedha za umma zinakaguliwa. Agizo la kusitisha ruzuku lilitolewa na kamati wala halikuwa agizo la mtu binafsi ndio maana lilikwenda kwa maandishi. Msajili kaiomba kamati kwa maandishi kuwapa vyama muda wa kujirekebisha ili hesabu zao zikaguliwe. Kwa vyovyote vile kusitisha ruzuku kungeumiza sana CCM na nashangaa sana kuona vya upinzani vinashabikia jambo hili.
PAC Leo imeamua vyama vyote kupeleka mahesabu yao kwa CAG yakaguliwe. Hivyo ni dhahiri hayakuwa yanakaguliwa. Hakuna haja ya kulambana kwani tayari tumepata uthibitisho kwamba hesabu hazijakaguliwa na sasa zitakaguliwa.
Kuhusu fedha za kukaguq PAC imeagiza hazina watoe fedha za ukaguzi huo maalumu wa kuanzia 2009/2010, 2010/2011 na 2012/2013.
Mimi binafsi sina maslahi binafsi ya zoezi hili. Napenda tu kuona kuwa fedha za umma zinakaguliwa. Sasa zitakaguliwa na kumaliza tatizo.
Wenye kutaka kuonyesha wameshinda ni juu yao. Muhimu ni kwamba kuanzia sasa fedha za umma zitakaguliwa na CAG kama matakwa ya sheria yanavyotaka. Ni ushindi kwa watanzania wenye fedha zao.
 
Tatizo hii issue inapokelewa kisiasa zaidi na nadhani kama chama kimoja tu kingekuwa hakijapeleka hesabu nadhani kauli ya zito ingeonekana lulu kwani hata humu jamvini naona tunaipokea kisiasa tu, haiingii akilini chama cha siasa ambacho ndio tunategemea kitaunda serikali alafu kikawa hakina utaratibu wa kukagua mahesabu yake, nadhani wamewapa muda wa kutosha ku-balance mambo yao kwani kanuni ya hela ni unafanya retirement then unapewa hela nyingine but ajabu kwa vyama vya siasa vyenyewe vinachukua hela tu mahesabu baadae
Wala haiingii akilini, vyama vyote vilidai mahesabu yao yako tayari na vingine yameshakakuguliwa, sasa miezi yote hiyo ya nini? Kwa nini wasiambiwe tu wakayakabidhi mara moja kwa CAG kwa ukaguzi. Wanawapa mad ili wayatengeneze!
 
Back
Top Bottom