Vyama vya siasa vipewe muda vikamilishe Mahesabu-PAC

Vyama vya siasa vipewe muda vikamilishe Mahesabu-PAC

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Kamati ya Bunge ya Mahesabu ya serikali PAC imetoa tamko la kuridhia vyama kukamilisha taarifa za fedha na kukabidhi kwa CAG ifikapo Januari 2014.

Hii ni baada ya Kamati hiyo kukutana na msajili wa vyama vya siasa Jaji Francis Mutungi leo jijini Dar es Salaam.

Pia kamati hiyo imemtaka msajili wa vyama kuendelea kuvipatia Ruzuku vyama hivyo.

Source:Mwananchi Breaking News
 
Ngoja buku7 waje na boss wao hapa,maana yule hana dogo anaweza itisha press tena na kutoa tamko kuwa ccm ishamaliza mahesabu yote ya toka 1961-2014
 
cc zitto kabwela


Ha ha ha yule hana lolote ni njaa tu ya madaraka inamsumbu ndio maana hata msajili kasema hawezi kusitisha ruzuku bila upembuzi yakinifu, akitilia mashaka uamuzi wa zitto kuwa alitaka kujijenga yeye mwenyewr
 
kuna kamati ya PAC na kamati ya Zitto!hizi directives za Kamati ya PAC,sasa tunangoja maagizo ya kamati ya Zitto.yale maagizo ya 'Nipo tayari kufa'
 
Dr. Slaa amepotea mitandaoni kwa sababu yuko busy kurekebisha mahesabu yaonekane safi!!!

Uzalendo mgumu...
 
kuna kamati ya PAC na kamati ya Zitto!hizi directives za Kamati ya PAC,sasa tunangoja maagizo ya kamati ya Zitto.yale maagizo ya 'Nipo tayari kufa'

Mkuu kuna mahali nimesema:


Wakurupukaji wajifunze.Tulisema PAC ilitakiwa ku-deal na CAG na Ofisi ya Msajili kwanza.

Hizi tabia za kukurupuka kama chafya ndizo zinazoharibu na kushusha kiwango cha siasa zetu

Ilimradi mtu una ajenda yako binafsi na mapovu ya kutosha basi unaitumia fursa kwa namna yoyote ile.

Hoja hazijengwi kisomi bali kwa jazba na chuki binafsi tu.Mbaya zaidi inapofanywa na wanasiasa wasomi

Haya sasa nashauri turudi kwenye mada za msingi.Katiba Mpya!
 
...Inaonekana msajili alikuwa na kazi ya kuwaelimisha akina Zito hadi wakaelewa walichopaswa kukifanya. Tatizo walibeba ajenda zao wakamiss target na sasa msajili kawarudisha kwenye target stahili na kuwatoa kwenye ajenda zao za kipuuzi.
 
Kamati ya Bunge ya Mahesabu ya serikali PAC imetoa tamko la kuridhia vyama kukamilisha taarifa za fedha na kukabidhi kwa CAG ifikapo Januari 2014.

Hii ni baada ya Kamati hiyo kukutana na msajili wa vyama vya siasa Jaji Francis Mutungi leo jijini Dar es Salaam.

Pia kamati hiyo imemtaka msajili wa vyama kuendelea kuvipatia Ruzuku vyama hivyo.

Source:Mwananchi Breaking News
aaaaaah! hivi sheria inaruhusu hii kitu kweli?
 
Ha ha ha yule hana lolote ni njaa tu ya madaraka inamsumbu ndio maana hata msajili kasema hawezi kusitisha ruzuku bila upembuzi yakinifu, akitilia mashaka uamuzi wa zitto kuwa alitaka kujijenga yeye mwenyewr

Lakini kwa kauli zake za njaa njaa mwisho wa siku January 2014 mahesabu yanatakiwa yapelekwe nadhani kama asingeitoa hiyo kauli ya njaa mahesanu yasingepelekwa mpaka uchaguzi mguu utakapokaribia
 
Nahisi kuna sehemu zito hakuwa sahihi.
 
Kamati ya Bunge ya Mahesabu ya serikali PAC imetoa tamko la kuridhia vyama kukamilisha taarifa za fedha na kukabidhi kwa CAG ifikapo Januari 2014.

Hii ni baada ya Kamati hiyo kukutana na msajili wa vyama vya siasa Jaji Francis Mutungi leo jijini Dar es Salaam.

Pia kamati hiyo imemtaka msajili wa vyama kuendelea kuvipatia Ruzuku vyama hivyo.

Source:Mwananchi Breaking News

Kuna uzi mwingine hapa JF unasema kuwa Msajili wa vyama vya siasa amesema ataendelea kutoa ruzuku. Sasa hawa mwananchi wanatuambia PAC 'imemtaka' Msajili aendelee kuvipitia ruzuku vyama vya siasa!

Nani alimuwahi mwenziwe?
 
aaaaaah! hivi sheria inaruhusu hii kitu kweli?

Tatizo hii issue inapokelewa kisiasa zaidi na nadhani kama chama kimoja tu kingekuwa hakijapeleka hesabu nadhani kauli ya zito ingeonekana lulu kwani hata humu jamvini naona tunaipokea kisiasa tu, haiingii akilini chama cha siasa ambacho ndio tunategemea kitaunda serikali alafu kikawa hakina utaratibu wa kukagua mahesabu yake, nadhani wamewapa muda wa kutosha ku-balance mambo yao kwani kanuni ya hela ni unafanya retirement then unapewa hela nyingine but ajabu kwa vyama vya siasa vyenyewe vinachukua hela tu mahesabu baadae
 
Mkuu kuna mahali nimesema:


Wakurupukaji wajifunze.Tulisema PAC ilitakiwa ku-deal na CAG na Ofisi ya Msajili kwanza.

Hizi tabia za kukurupuka kama chafya ndizo zinazoharibu na kushusha kiwango cha siasa zetu

Ilimradi mtu una ajenda yako binafsi na mapovu ya kutosha basi unaitumia fursa kwa namna yoyote ile.

Hoja hazijengwi kisomi bali kwa jazba na chuki binafsi tu.Mbaya zaidi inapofanywa na wanasiasa wasomi

Haya sasa nashauri turudi kwenye mada za msingi.Katiba Mpya!

nilitaka kushangaa mzee wa sum asimtetee dr slaa, yeye na wenzake 4 wanalipwa kwa kumwangamiza Zitto kisiasa na wako ladhi ata kumwondolea maisha yake. huo kikwetu tunakufananisha na SHOGA.
 
...Inaonekana msajili alikuwa na kazi ya kuwaelimisha akina Zito hadi wakaelewa walichopaswa kukifanya. Tatizo walibeba ajenda zao wakamiss target na sasa msajili kawarudisha kwenye target stahili na kuwatoa kwenye ajenda zao za kipuuzi.
Angekuwa Tendwa sasa tungekuwa tunaongea mengine... ha ha ha haaa! mafao mwema, mzee sharo baro!
 
Mkuu kuna mahali nimesema:


Wakurupukaji wajifunze.Tulisema PAC ilitakiwa ku-deal na CAG na Ofisi ya Msajili kwanza.

Hizi tabia za kukurupuka kama chafya ndizo zinazoharibu na kushusha kiwango cha siasa zetu

Ilimradi mtu una ajenda yako binafsi na mapovu ya kutosha basi unaitumia fursa kwa namna yoyote ile.

Hoja hazijengwi kisomi bali kwa jazba na chuki binafsi tu.Mbaya zaidi inapofanywa na wanasiasa wasomi

Haya sasa nashauri turudi kwenye mada za msingi.Katiba Mpya!

Atakuja hapa, atatema povu halafu utashangaa buku 7 fc wote wanavamia thread kumsapoti. Yule jamaa wanamvumilia sana wenzake chamani!
 
Kamati ya Bunge ya Mahesabu ya serikali PAC imetoa tamko la kuridhia vyama kukamilisha taarifa za fedha na kukabidhi kwa CAG ifikapo Januari 2014.

Hii ni baada ya Kamati hiyo kukutana na msajili wa vyama vya siasa Jaji Francis Mutungi leo jijini Dar es Salaam.

Pia kamati hiyo imemtaka msajili wa vyama kuendelea kuvipatia Ruzuku vyama hivyo.

Source:Mwananchi Breaking News
msajiri alisema hawezi kusitisha ruzuku kwa vyama hadi ajiridhishe.
 
Lakini kwa kauli zake za njaa njaa mwisho wa siku January 2014 mahesabu yanatakiwa yapelekwe nadhani kama asingeitoa hiyo kauli ya njaa mahesanu yasingepelekwa mpaka uchaguzi mguu utakapokaribia

Usiwe msukule wa viwango hivyo. Ni sheria ipi ya fedha ambayo ikikiukwa haitoi adhabu ina compromise na mkiuka sheria? Zitto alisema sheria imekiukwa. Sasa kama hakupiga siasa kwa nini hawajatoa adhabu kwa vyama vilivyokiuka sheria badala yake vinaongezewa muda?
 
Imefika mahali tujadili mambo bila kuweka vyama vyetu mbele,

CAG ndiye mwenye jukumu la ukaguzi na kimsingi amekwisha toa sababu za kushindwa kukagua ambayo ni kutopewa fungu la ukaguzi wa vyama vya siasa.

Binafsi nimemuunga mkono Zitto katika harakati za kuhakikisha ukaguzi unafanyika na ukweli unajulikana lakini wakati tunaunga mkono hili swala mwanzoni kabisa hapa hapa JF tukiamini ni swala jema kiuwajibikaji siku zinavyokwenda linaanza kuleta sura za kisiasa na hili ndio tatizo nchi hii.

Tatizo liko wazi na kimsingi CAG ametoa sababu na ilipaswa tujue hatua gani zichukuliwe kurekebisha huu udhaifu lakini naona kuna taswira inajengwa kutuhumu vyama hasa kuna chama kimelengwa very specific.

Lazima vyama vikaguliwe na CAG na tuache siasa kwenye mambo ya msingi maana tuna sheria na miongozo inayotosha kuongea na si kuanza kutuhumu tu na kuishia kuchanganya wananchi wasioelewa ukweli halisi.
 
Back
Top Bottom