Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

In principle hakuna ubaya kwa watu kushiriki katika mchakato wa siasa wa nyumbani kutoka ughaibuni, ningependa kuona hata kura tunaenda kupiga ubalozini na kwenye consulate zetu mbali mbali.

Lakini kinachoendelea sasa hivi ni kama members walivyosema hapo juu.Matawi haya yanaonekana kuwa ni "dili la ulaji" tu. Ukifuatilia kinachoendelea jumuiya ya CCM London sasa hivi ni aibu tupu.

As stated, I am not entirely against the idea of having these branches, but I would like to see them run in a more politically savvy way and taking a bigger socio-economic role.I frankly see a bigger role to be played by non-partisan Tanzania development associations zitakazosaidia kutuma hela nyumbani, kufanya biashara na nyumbani, kusaidia wakati wa misiba na sherehe nk kuliko haya mambo ya kushabikia vyama, hususan kwa chama kilichokuwa established kama CCM.

The way things are going now mimi naona wana promote idling, embezzlement na division tu.

I think division is wot's gonna happen here..watanzania tukikutana huwa tuna umoja sana na tukiongea siasa tunajadili na kuwa wazi kwa matatizo ya nyumbani bila kujali nani ni nani nyumbani..sasa limekuja hili group ambalo kama ni viziwi..propaganda kibao..they end up making a fool of themselves and the tanzanian community as a whole..untill they give us legitimate reasons to why they are doing this..i will personally keep on critising (keep in mind mimi sio CUF, SIO CHADEMA SIO NCCR..mzalendo tuu)..im jus shocked at how some of our brothers and sisters (ambao wamepata bahati ya kuwa nje kujionea systems of accountability na kuona tanzania from a different angle) but they are still so ignorant of the situation back home utafikiri hawana ndugu vijijini wanaotaabika..inauma sana!

Je kwa kufungua haya matawi wanatuambia tulio huku kwamba wamefurahishwa na yanayotokea nyumbani chini ya uongozi wa CCM??
 
Hawa watu wa UK na Asia wanaofungua haya mashina ya CCM wanaboa kweli. I'll put em on blast this coming sunday. I just can't stand them grrrrrrrrrr.

Namna mojawapo ya kushughulikia hawa jamaa wanaofungua matawi kwa ajili ya kulinda status quo ama kama vitega uchumi vyao ama njia ya kujipenyeza kwenye system ni kuwashambulia kama wengine wanavyofanya hapa. Lakini namna nyingine ni kufungua matawi ya vyama mbadala; kuendeleza mapambano ya fikra. Kama wao nafungua matawi ya fikra za kifisadi bila matawi ya fikra nyingine hapawezi kuwa na vitovu organized vya mapambano ya fikra.

Huko tunapoelekea sheria za uchaguzi zitaruhusu watanzania walioko nje kupiga kura; how will political mobilization be done kama hakuna matawi?

Hivi karibuni tulikuwa na mazungumzo na msajili wa vyama vya siasa; na moja ya maeneo ni sheria zetu kueleza bayana kuhusu taratibu za ufunguaji wa matawi nje ya nchi. Kwa sasa sheria iko kimya; kuna mwanya wa matawi kufunguliwa kama affilliates wa vyama vya siasa nje ya nchi.

Pamoja na kujadili jinsi ya kuwapinga wanaofungua matawi kwa nia za kifisadi tujadili pia matawi genuine yafunguliwaje? Kwa nini? Yawe na muundo gani? Malengo gani?

Kikwazo kikubwa ni kuwa kuna matabaka katika watanzania walio nje ya nchi. Wengi ya watu wanaokerwa na yayofanywa na siasa za kifisadi, wengi wao pia wako nje ya nchi kwa njia za mkato- hivyo wakati mwingine wao kujitokeza kufungua matawi na kufanya siasa za upinzani nje ya nchi ni hatari kwa survival yao. Lakini kwa upande mwingine, wengi ya waliokwenda kwa njia iliyonyooka ni hao hao ambao ni wapenzi wa kulinda status quo na baadhi yao ni wanufaika wa ufisadi.

Lakini bado naamini kwamba wako watanzania wengi tu wenye uwezo wa kufungua matawi ya upinzani nje ya nchi, ambao wametimiza taratibu zote za kuwa nje; ambao hawahitaji kujipendekeza kwa Balozi za Tanzania nje ya nchi. Ni wakati wa kusimama na kuhesabiwa.

Nitafurahi siku moja- kukawa na mabalozi mbadala katika nchi mbalimbali; watakaoweza kuzikosoa hata balozi zetu nje ya nchi kama zikishindwa kutimiza wajibu wake kwa raia wa Tanzania walioko nchi hizo na hata kwa malengo ya kitaifa yaliyowapeleka huko. Nitafurahi siku hiyo! Nitafurahi kwa kuwa tutakuwa na mifumo mbadala ya kutoa hata sera mbadala za mambo ya nje kuhusiana na mahusiano yetu na nchi hizo. Lakini ili hili litokee, linahitaji wewe uliyeko huko; sio sisi viongozi wa kisiasa tulioko huku nyumbani.

Natambua kwamba kuna vyama vya watanzania walioko nchi hizo- wakati mwingine zinafanya malengo yanafanana kidogo na hayo- lakini hizi ni non partisan civil society; bado political activism inahitajika ili mradi tumeamua ku-organize vyama vyetu katika model ya matawi.

Otherwise; kwa wale ambao dhana ya matawi inawachefua; bado wananafasi ya kufanya siasa mbadala, siasa za upinzani nje ya nchi- kwa mtindo wa vuguvugu(movement). Chama cha siasa si lazima muundo pekee; hata mawazo tu yanayoratibiwa chini chini kwa vuguvugu yanaweza kuleta mabadiliko. Hayakamatiki; hayaonekani- lakini yana nguvu kubwa ya kuushinda mfumo wa kifisadi; madikteta kote duniani wanajua jinsi vuguvugu linavyoweza kuangusha tawala zinazominya demokrasia. Tujaribu, tutaweza!

JJ
 
Nakubaliana kuwa ni muhimu watu kupiga kura wakiwa nje lakini sioni kwa nini lianzishwe tawi la chama cha siasa ili kutimiza hilo.
Katika hali ya sasa, kila chama kipo huru kuendesha harakati zake nchini hivyoi hakuna sababu ya kuwa na tawi nje ya nchi. Kama chama kinashindwa kufanya siasa nchini katika mazingira ya sasa, sijui kama kitafanikiwa kwa kuanzisha tawi nje ya nchi.
Huko nje sanasana wanaweza kuwa wanatafuta fedha tu au kama ilivyodokezwa ni opportunity ya baadhi ya watu kutafuta namna ya kuingia kwenye system.
Hata hivyo, kama wanatafuta fedha inapaswa wawe makini isije wakatumbukiziwa fedha za mazabe kwenye vyama vyao wakajikuta katika hali mbaya zaidi
 
Nilitegemea wabongo wa ughaibuni kutokana na exposure na elimu watakuwa watu wa kwanza kuongoza mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa kule nchini lakini ndio kwanza wanaongoza kupiga vigeregere na kushangilia uchafu wa CCM kama wanavijiji mbalimbali pale Bongo wanaopewa pilau na khanga za bure wakati wa upigaji kura. MNABOA SANA GRRRRRRRRR.
 
Mnyika nadhani sikubaliani nawe kuhusiana na kufungua matawi mbalimbali ya vyama vya siasa ughaibuni, nadhani kitu muhimu kwetu ni kufungua Jumuiya mbalimbali ambazo zitakuwa na malengo ya kufungua vitega uchumi au kuwainua kiuchumi watanzania walio katika nchi hizo. Watu hawatoishia kufungua matawi ya CCM,Chadema,CUF,TLP na vyama vingine, mwisho wake wataanza kuanzisha vyama vyao vya kikabila na hapo ndio itakuwa mwanza wa kuanzisha makundi katika jamii hizo. Watanzania hawako wengi ughaibuni kwa hiyo ni bora kushikamana katika jumuiya za kawaida kuliko vyama vya Siasa.

MLIOANZISHA MATAWI YA CCM KULE LONDON NA ASIA MNABOA SANA, Y'ALL SUCK !!
 
Geeque,

Nilitegemea wabongo wa ughaibuni kutokana na exposure na elimu watakuwa watu wa kwanza kuongoza mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa kule nchini lakini ndio kwanza wanaongoza kupiga vigeregere na kushangilia uchafu wa CCM kama wanavijiji mbalimbali pale Bongo wanaopewa pilau na khanga za bure wakati wa upigaji kura. MNABOA SANA GRRRRRRRRR.

Very important point on the role of Tanzanian intellectuals in the diaspora on political change at home.

Ingawa proportionally inawezekana kuna wabongo wengi walio college educated ughaibuni kuliko bongo, hili halimaanishi kwamba.

1.Walio "college educated" ndiyo walioelimika.Kuna watu wamepitia vyuo na hawajaelimika.

2.Walio ughaibuni ndiyo wana exposure zaidi.Kuna watu wamepata exposure wakarudi bongo wakati wengine wamebaki ughaibuni mpaka kesho hawana exposure, wanakumbatia vi clique vyao -mwanzo wa kutafuta security in numbers na deals za ajabu katika matawi ya vyama vya siasa-. Kuna watu hawajatoka bongo wana subcribe kila kitu muhimu na wanaelewa dunia kuliko watu walio ughaibuni.Admittedly this is not a sizable proportion though.

3.Wanaoendesha huu upuuzi wa vyama vya siasa ni wabongo walioelimika.Kuna watu wengi wasio na shughuli au prospects za siku za usoni wameshindwa mikakati ya elimu na career ughaibuni wanaona njia rahisi ya kutafuta maisha ni ukajanja wa vyama vya siasa.

Tatizo linakuja wabongo wengi walioelimika wanajua how pathetic system yetu ilivyo na wameamua kufanya mambo yao tu.This is sad kwa sababu kama unavyosema walitakiwa kuwa mstari wa mbele kuchochea mabadiliko lakini ni vigumu kumwambia Professor wa Kibongo mwenye residency USA na anayekimbiza miaka michache tu kupata tenure ashiriki siasa za bongo.It takes a person of great conviction and patriotism.Furthermore the available vehicles for this enterprise are seriously limited.

Kwa hiyo wale wanaoweza kufanya vuguvugu la kweli, kwa kuwa wanaelewa sacrifice inayotakiwa na challenge zilizo mbele,in a Socratic reluctance if not due to selfish awareness, wanaamua kuacha kujishughulisha, wale wanaojishughulisha hawana ajenda yoyote zaidi ya ukajanja.

It is pretty much the same at home
 

..ni ujinga na na uroho wa madaraka ndio unaofanya watu kujipendekeza na kuanzisha vyama ughaibuni,kwa kifupi ni kama vile watu huwa wana-regret kuishi ughaibuni na at the same time wanataka kuvuna nyumbani, so kwa kujigawa ndo idea ya kuanzisha tawi nje ya nchi linapokuja ili ata later mtu atakapokuja kuomba dhamana ya wananchi(ubunge!!) aseme eti alikuwa mwanachama wa chama fulani tokea nje ya nchi kwa miaka kadhaa!! ni ulafi mtupu!! Lets not get fooled na hii scam!!This government led by J.Kikwete ni corrupt and ignorant government, inabidi ipingwe kama inavyopingwa China ktk olympics over Tibet!! Yes we can, tuanze vijijini! huko ndipo kwenye mizizi achilia mbali matawi!!...lets make a move!!

Wanatengeneza CV zao kwani mtu anaweza kuwa anafanya kazi Care ya kuosha wazungu kwa miaka saba na ana MBA hivyo akirudi nyumbani CV yake hawezi kuandika kuwa alikuwa mchambishaji wa wazungu ni bora awe na tittle ya Mwenyekiti/katibu wa CCM UK .

hapa Reading kuna msiba hatujawaona kuja kusaidia msiba, na kwa sasa kuna misiba mitatu huwezi kuwaona wanachama wa Vyama wako kwenye misiba. sasa imekuwa kama Kitchen Party kila wiki linafunguliwa tawi na huwezi kuona wanachama wapya zaidi ya viongozi wawili wakiongoza na mbunge wa Singida.

Hawa wa India wame graduate siku moja kabla ya kufungua tawi la chama unaona kabisa kuwa wameGraduate na sasa wana waza kazi watapata vipi? bora wapitie upenyo wa siasa.

Hawa watu hawajui chama wala siasa na sasa kumekuwa na group la watu wa kasikazini kujifanya ndio wamehodhi kila kitu.

Mimi siungi mkono matawi ya Ughaibuni watu kama CUF wakipewa upenyo huu watautumia kupanga mikakati mibaya kwani hakuna wa kuwazuia.
 
Mnyika nadhani sikubaliani nawe kuhusiana na kufungua matawi mbalimbali ya vyama vya siasa ughaibuni, nadhani kitu muhimu kwetu ni kufungua Jumuiya mbalimbali ambazo zitakuwa na malengo ya kufungua vitega uchumi au kuwainua kiuchumi watanzania walio katika nchi hizo. Watu hawatoishia kufungua matawi ya CCM,Chadema,CUF,TLP na vyama vingine, mwisho wake wataanza kuanzisha vyama vyao vya kikabila na hapo ndio itakuwa mwanza wa kuanzisha makundi katika jamii hizo. Watanzania hawako wengi ughaibuni kwa hiyo ni bora kushikamana katika jumuiya za kawaida kuliko vyama vya Siasa.

MLIOANZISHA MATAWI YA CCM KULE LONDON NA ASIA MNABOA SANA, Y'ALL SUCK !!

Geeque

Rudia tena kusoma post yangu mkuu. Nimetoa menu kwa watu wote- mwenye kutaka kufangua tawi afanye hivyo; na asiyetaka aache. Ndio maana ya demokrasia.

Ama kama uwepo wa matawi unawagawa watanzania basi ni ishara kwamba watanzania hawaelewi maana ya siasa za mfumo wa vyama vingi. Sasa tusivunje sahani kwa kuwa ni chafu; tuisafishe.

Inabidi tujiulize; tawi nini- ni kijiwe na bendera ama ni jumuia ya watu wenye kukubaliana katika itikadi ya chama fulani kwa malengo ya kisiasa? Sasa kama kuna waCHADEMA wako nchi fulani- kuna ubaya gani watu hao kufahamiana na kukutana?

Kusema kwamba wakishajuana kwa misingi ya vyama vyao hawatazikana; ni kama kusema sisi huku nyumbani tunaojuana kwa misingi ya vyama fulani basi hatuzikani.

Kusema kwamba kwa uchache wao watanzania wa nje hawawezi si vyema wakagawanyika kiitikadi ni kama kusema watu wachache hawana haki ya kuwa na itikadi tofauti. Ni kunyima uhuru wa fikra.

Lakini kusema hayo- sipingi hoja yako ya jumuia za kiuchumi na kusiadiana- hizi ziwepo tu na zitimize malengo uliyoyataja; na ziundwe na watanzania wote bila kujali itikadi. Lakini uwepo wa jumuia za kiuchumi au kijamii hauzuii uwepo wa jumuia za kisiasa.

na kama siasa inawagawa wananchi na kuondoa umoja wao popote pale walipo- iwe ni Zanzibar ama ughaibuni; basi siasa hiyo ina walakini. Na ni wajibu wetu kuundoa huo walakini; na kama walakini huo hauwezi kuondoka; basi siasa hiyo ya vyama vingi yenye kuleta mgawanyiko haina maana kuwepo, tuiache na kurudi kwenye chama kimoja!

JJ
 
Matawi haya mengi ni ubabaishaji watu wa UK wamesikia kuwa JK anakuja mwezi wa nne(April) basi mwezi march wote umetumika kufungua matawi zaidi ya manne,Mwaka jana waliposikia JK anaingia UK wakaanzisha Tawi ili ili kujijenga kwake.

India nao wamesikia JK anapita wiki hii basi nako matawi yamefunguliwa mwisho wa wiki ya jana.huu ndio unafiki dhamira zao za siri ni kuwa karibu na JK na si chama.Mbona hawakufungua kipindi cha Mkapa ambaye hakuwa na utaratibu wa kuonana na WaTanzania akiwa Ughaibuni.

wanachama wa India

http://issamichuzi.blogspot.com/2008/04/mysore-wafungua-tawi-la-ccm.html#comments
 
am aware that kikwete atakua UK kwenye tarehe 16 april, kusudi la kuwepo UK, kama tulivyoelezwa na Ikulu, ni zuri na ni kwa ajili ya watanzania wote, regardless political stand.Ila am very much sure kuna watu wasiojua mipaka ya chama na serikali watafanya ujio wa kikwete ni wa kichama!! sitashangaa kuona kumbi imepambwa na bendera za CCM na kumbi kurembeshwa kwa kijani na njano!!
 
Hawa wa India wame graduate siku moja kabla ya kufungua tawi la chama unaona kabisa kuwa wameGraduate na sasa wana waza kazi watapata vipi? bora wapitie upenyo wa siasa.
Inawezekanaje wagraduate na kufungua tawi, Sidhani kama ni ukweli
Kama ni mgawanyiko sidhani, kwani hawa si watoto wadogo hawezi kutengana kwa ajili ya itikadi ya chama.
Mbona nyumbani watu wanavyama tofauti, lazima tuelewe kuwa siasa ni siasa na utu ni kitu kingine.
Tusiwe na mawazo mgando, niwakati wa vyama vingine tufungue matawi kuleta more challenges,kwani hapo ndipo democrasia itakuwa.
Ikumbukwe kuwa ccm wanaanza kuwaandaa vijana wadogo kwa kuwajaza itkadi zao,wakirudi watu hawa itakuwa vigumu mno kuwabadilisha mawazo
 
Inawezekanaje wagraduate na kufungua tawi, Sidhani kama ni ukweli
Kama ni mgawanyiko sidhani, kwani hawa si watoto wadogo hawezi kutengana kwa ajili ya itikadi ya chama.
Mbona nyumbani watu wanavyama tofauti, lazima tuelewe kuwa siasa ni siasa na utu ni kitu kingine.
Tusiwe na mawazo mgando, niwakati wa vyama vingine tufungue matawi kuleta more challenges,kwani hapo ndipo democrasia itakuwa.
Ikumbukwe kuwa ccm wanaanza kuwaandaa vijana wadogo kwa kuwajaza itkadi zao,wakirudi watu hawa itakuwa vigumu mno kuwabadilisha mawazo

PITIA MICHUZI BLOG KUNA HABARI YA WAO KU GRADUATE NA PICHA ZAO.TUSIANDIKIE MATE NA WINO UPO.
 
kwa hali ilivyo sasa nchini kwetu huku, halafu uone eti watu wakubwa kabisa wanapiga na picha eti, ni tawi la ccm linafunguliwa sijui London, sijui India, heri na sisi tulioko hukuhuku nchini...

Wakati huu ambao tunaunganisha nguvu pamoja kupambana na mafisadi, ni kichefuchefu kusoma habari hizi...! basi tu.

Na wao wanafanya makusudi kuutetea ufalme uliopo ili waendelee kubakia na hali nzuri...
Nasema iko siku... Nani angejua Sadamu angebebwa kama nyau... aliyeiba mayai siku moja.

lakini hawa ndio walewale!

Hiyo Londoni hiyo jamani tusaidieni kuelimisha, kila la huko ukiliona kwenye blogs yeyote... sio wamemkaribisha, sio tawi. sio salamu, sio pongezi... unajiuliza hawa wazungu au waafrika wenzetu.. hawana ndugu tz kweli hawa wanaoteseka...
au ndio wale waliokuwa wazungu?

ungekuwa na viboko ni kuwatandadika tu...!
 
kwa hali ilivyo sasa nchini kwetu huku, halafu uone eti watu wakubwa kabisa wanapiga na picha eti, ni tawi la ccm linafunguliwa sijui London, sijui India, heri na sisi tulioko hukuhuku nchini...

Wakati huu ambao tunaunganisha nguvu pamoja kupambana na mafisadi, ni kichefuchefu kusoma habari hizi...! basi tu.

Na wao wanafanya makusudi kuutetea ufalme uliopo ili waendelee kubakia na hali nzuri...
Nasema iko siku... Nani angejua Sadamu angebebwa kama nyau... aliyeiba mayai siku moja.

lakini hawa ndio walewale!

Hiyo Londoni hiyo jamani tusaidieni kuelimisha, kila la huko ukiliona kwenye blogs yeyote... sio wamemkaribisha, sio tawi. sio salamu, sio pongezi... unajiuliza hawa wazungu au waafrika wenzetu.. hawana ndugu tz kweli hawa wanaoteseka...
au ndio wale waliokuwa wazungu?

ungekuwa na viboko ni kuwatandadika tu...!

Hawa dawa yao ni kuwapiga picha ndugu zao vijijini na kuwatumia..naona wamepoteza mwelekeo...sijui ndo kukaa sana ulaya..au ndo gear ya kurudia bongo! Naona elimu ya ulaya siku hizi haitoshi lazma na kadi ya CCM au??
 
Manufaa ya matawi kwa sasa si faida kwa Nchi bali wajanja kutumia nafasi kujitangaza na biashara zao na kupata tender na si zaidi ya hapo

Hili nalo sasa linataka kuwa tatizo kubwa sana, na limeanzia London, kuna watu pale wenye nia njema, lakini kuna wanaotaka kujipatia ujiko, nina wasi wasi kuwa balozi wa pale ni naive sana, au na yeye anafikiri ni ujiko ku-entertain huu ujanja ujanja,

I mean nina heshima sana na mama Balozi, lakini hili la matawi ya CCM, halijakaa sawa, labda watoe maelezo zaidi, otherwise ninakubaliana na wachangiaji wengi hapa kuwa ni ujanja wa baadhi ya wananchi kujaribu kujisogeza na the powers! Sasa tatizo litakuja kwa wale wasiojihusisha je itakuwaje?
 
................... lakini hili la matawi ya CCM, halijakaa sawa, labda watoe maelezo zaidi, otherwise ninakubaliana na wachangiaji wengi hapa kuwa ni ujanja wa baadhi ya wananchi kujaribu kujisogeza na the powers! Sasa tatizo litakuja kwa wale wasiojihusisha je itakuwaje?

....watabakia kuwa...........huyu ni rafiki yangu........na siyo rafiki yetu.......!!!
 
Kule kwa Michuzi na Haki niliuliza ni kwanini haya matawai yanazagaa sana Asia and UK? Hakuna aliyenijibu, but i still believe there is something behind this CCM global Invasion.

There is nothing wrong kuanzisha tawi la CCM, lakini inatia mashaka kuona haya matawi yanayofunguliwa kila kukicha pasipo agenda. Swali linakuja jee kuna baadhi ya watu wanataka kufaidikika kwa njia moja au nyingine?

Nimeona hasa UK ufunguzi unaenda sambamba na balozi wa Tanzania hapo UK. Jee huyu balozi ni political figure au neutral? Jee what is the common purpose za yeye kualikwa kwenye ufunguzi wa haya matawi? Swali gumu ninalo jiuliza ni " is this movement affiliate with CCM network expansion"?

Jee Watanzania member wa haya matawi wanabefit vipi? Maana pale UK kuna jamaa mmoja nasikia yeye ndie anaenzisha hizi movement na kisha yeye ndie anapata check kutoka makao makuu, jee swala zima ni kutanua ufusadi?
 
Back
Top Bottom