Vurugu mitaani Mwanza kati ya wamachinga na polisi

Vurugu mitaani Mwanza kati ya wamachinga na polisi

hivi hiyo makoroboi inashida gani!kila kukiwa na fujo mwanza zinaanzia hapo!!!kwa nn wasiwaache vijana wachape kazi bila bugudha!!


yaan hii serikali taabu tupu, watu wakijiajiri napo shida.............pale wala hapana tatizo kwsbb watu wanafanya biashara zao kwa utulivu sasa sijui serikali inakereka nn, na sijui waende wapi sasa hawa watu.
 
Wapigwe tu, hao ni wakwepa kodi. Kwanini mimi nilipe kodi wengine wasilipe kupitia umachinga? Hao ni wahujumu uchumi. Mnataka uchumi wa nchi uteketezwe na machinga badala ya kuwa na investments kubwa mijini? Hivi kila kijana akiwaza umachinga, tutakuwa na taifa la aina gani?
 
Tupia picha za zile screen za mtaani ka bdo zipo hai.

Ngoja nijaribu kuweka... IMG_20140611_103146.jpg

Hapo ni askari wa FFU wakiwa barabara ya Karuta tayari kwa kupiga mabomu
 
Dah hata mimi nimeongea na mtu toka Rock City alikuwa ofisini kwake ikabidi ghafla iwe unplan public holiday.Hatariiii
 
Machinga wanathaminiwa wakati wa uchaguzi tu, baada ya hapo ni maji ya kuwasha, mabomu ya machozi na virungu vya polis kwa kwenda mbele...
 
charminglady mpenzi usitoke ofisini kabisa maana huku tu tayari nasikia sauti za mabomu yani sijui tunatokaje
 
Last edited by a moderator:
Habari zilizonifikia punde zinasema kuwa kuna vurugu zinaendelea katikati ya jiji la Mwanza kati ya Machinga na Polisi wa kutuliza ghasia

Vurugu hizo zimeelezwa kutokea eneo la Makoroboi ambapo Machinga hufanyia biashara zao baada ya Halmashauri ya jiji la Mwanza kuwapa eneo hilo wafanyie biashara

Habari zinasema kuwa mabomu yamerindima eneo hilo na shughuli simesimama

Mbunge wa Nyamagana Ezekia Wenje yupo Bungeni na nimepewa taarifa kuwa ameomba muongozo wa Spika kuhusiana na suala hilo na spika amemuomba Mh Lukuvi ajibu kwa niaba ya Waziri Mkuu na Kukuvi amesema Mh Wenje asubiri hadi ofisi ya Waziri mkuu ijiridhishe na taarifa hizo na kisha kumjibu

Tunasubiria taarifa zaidi!
 
Mjini kumenishinda, nimeamua kurudi hotelini. Hawa askari wanatia hasira sana. Waswahili walisema "mzaha mzaha hutumbua usaha" siku moja tutajutia jaya maamuzi ya viongozi wetu.
 
  • Thanks
Reactions: ram
ni kweli nimeongea na katibu wa wamachinga akathbitsha 0759213469
 
Back
Top Bottom