Wakazi wa eneo la Lupaso, Vikawe wilayani Kibaha mkoani Pwani wameingiwa na hofu baada ya watu wanaodaiwa kujitambulisha kuwa polisi kufanya operesheni ya usiku na kuwakamata baadhi ya wananchi, siku nane tangu kutokee vurugu zilizohusishwa na mgogoro wa ardhi katika eneo hilo.
Tukio hilo limetokea majira ya saa 8 usiku kuamkia leo Mei 14, 2026 ambapo watu kadhaa walichukuliwa bila maelezo ya wazi kuhusu wanakopelekwa.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Vikawe, Shaban Ally Shaban, amesema jumla ya watu 13 walikamatwa katika operesheni hiyo, lakini baadaye watu 10 waliachiwa huku watatu wakichukuliwa na watu hao bila taarifa rasmi.
Amesema hadi sasa uongozi wa mtaa haujui sababu za kukamatwa kwao wala walikopelekwa, jambo lililoibua taharuki kwa wananchi wa eneo hilo.
Akizungumzia hali ya usalama baada ya vurugu za Mei 6, 2026, mwenyekiti huyo amesema wananchi walikuwa wamejipanga kuimarisha ulinzi wa maeneo yao kufuatia mgogoro wa muda mrefu wa ardhi kati ya wakazi wa Vikawe na familia ya Juma Ngololo inayodaiwa kumiliki eneo hilo kihalali.
Uongozi wa mtaa sasa unapanga kwenda Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Pwani ili kupata taarifa rasmi kuhusu watu hao watatu walioondolewa wakati wa operesheni hiyo.
Juhudi za kulitafuta Jeshi la polisi zinaendelea, kupata undani wa taarifa hii
Chanzo: EATV
Tukio hilo limetokea majira ya saa 8 usiku kuamkia leo Mei 14, 2026 ambapo watu kadhaa walichukuliwa bila maelezo ya wazi kuhusu wanakopelekwa.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Vikawe, Shaban Ally Shaban, amesema jumla ya watu 13 walikamatwa katika operesheni hiyo, lakini baadaye watu 10 waliachiwa huku watatu wakichukuliwa na watu hao bila taarifa rasmi.
Amesema hadi sasa uongozi wa mtaa haujui sababu za kukamatwa kwao wala walikopelekwa, jambo lililoibua taharuki kwa wananchi wa eneo hilo.
Akizungumzia hali ya usalama baada ya vurugu za Mei 6, 2026, mwenyekiti huyo amesema wananchi walikuwa wamejipanga kuimarisha ulinzi wa maeneo yao kufuatia mgogoro wa muda mrefu wa ardhi kati ya wakazi wa Vikawe na familia ya Juma Ngololo inayodaiwa kumiliki eneo hilo kihalali.
Uongozi wa mtaa sasa unapanga kwenda Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Pwani ili kupata taarifa rasmi kuhusu watu hao watatu walioondolewa wakati wa operesheni hiyo.
Juhudi za kulitafuta Jeshi la polisi zinaendelea, kupata undani wa taarifa hii
Chanzo: EATV