Mu-Israeli
JF-Expert Member
- Mar 21, 2012
- 2,454
- 975
Mwanza kuna vurugu kati ya wamachinga wa soko la Makoroboi na polisi.
Mabomu ya machozi yanapigwa sasa.
======Updates======
Mabomu ya machozi yanapigwa sasa.
======Updates======
Mh. Wenje akiwa bungeni ameuliza swali la dharura na amesema kuwa sasa hivi Mwanza hali sio shwari tena maana mabomu nayapigwa kila sehemu.Maduka jijini Mwanza yamefungwa kwa siku ya leo katika operesheni ya kuondoa machinga mtaa wa Makoroboi.
Ameomba pia serikali kuweka mipango madhubuti kwa wafanyabishara ndogo ndogo (Machinga) ili wapate sehemu ya kufanyia biashara.
Ameomba serikali kusitisha hiyo operesheni mara moja na muafaka wa swala hilo upatiwe ufumbuzi na wizara husika ya viwanda na biashara.
Mh. Lukuvi amejibu swali la dharura kwa kusema, Amesema ni kweli jambo hili limetolewa humu ndani na bado serikali inakusudia kutoa taarifa, anasema mh waziri mkuu alitoka bungeni na kwenda kuongea na wahusika na watachukua hatua kwa ishu ya Mwanza kutafta ukweli wa hali halisi na pia hawawezi kusimamisha operesheni hiyo kwa kauli wakiwa bungeni.Mhe Amekuja bungeni kupiga kura na anaendelea kushughulikia hili jambo.
![]()
![]()
![]()