Nimeishi kusini miaka 10 na lindi mjini ndiyo nimeishi zaidi nikiwa nafanya kazi katika mashirika ya kimataifa vijijini. Nilishuhudia umaskini wa kutisha na mawazo mgando yaliyolalamika daima "sisi watu wa kusini tumeachwa, kuanzia kung'oa reli" hadi ukosefu wa barabara. Nimeshuhudia wanafunzi wa shule wasiovaa viatu na wasichana wamejifunga vipande vya kaniki wakiimba tuna imani na Mwinyi, Nyerere, CCM huku viganja vikilenga mapaji ya uso salamu ya chipukizi wa TANU youth league!!Nikitinga mitaa ya Mtanda, Jamhuri, Mitwelo, Kariakoo, Mikumbi, Mpilipili, Sabasaba; Manispaa ya Lindi imepambwa na bendera za CCM kukiwa na uchache wa bendera za Chadema. Wananchi wa Lindi wamesikika wakinena hawatadanganyika na kujiunga na chama cha Kaskazini, wao sio watu wa kufanywa wa mwisho. Hawatafanya kosa kuiacha CCM iliyoiunua maisha ya Lindi kuipitia sera nzuri mfano ujenzi wa barabara na mashule ya kumwaga.
Nimeshuhudia watu wakila mbegu za miti zenye sumu sana wengine wakifa!! na hata majani!!
Ndugu yangu kusini ni mtaji mkuu wa CCMAGAMBA yaani UMASKINI. Sasa kudanganywa kunatokana na ahueni ndogo!! ambayo wameipata au ni ujumbe kutoka kwa SALMA JK (First lady) mwenye uenyeji wa hapo MIKUMBI?
Simba wa Nachunyu vipi?? wamethibitiwa?
Ming'oko vipi bado inaliwa? Huo utajiri mlioletewa na CCM ni upi?