watu wa lindi amkeni
ungesema walindi chagueni suti ya kuvaa safari ndo imeshaanza! Tayari walishaamka 2010, si unamjua mbunge wa lindi mjini hivi ni wa chama gani vile?
watu wa lindi amkeni
Watu wa Lindi si wajinga ni wapole na waungwana si kama watu wa Kilimanjaro na Arusha,mimi nimefanya kazi Railways Moshi na Arusha nawafahamu sana nyie ndugu zetu na hulka zenu za ubinafsi,uwiano wa shule za msingi na upili katika maeneo mengi Tanzania unatofautiana na hilo si jambo la kuwalaumu wakazi wa sehemu husika pia suala la utajiri wa watu nalo pia linategemea kwa mfano maeneo mengi ya Kusini kuna Gesi Asili,mafuta,chuma,maka ya mawe,uranium vitu ambavyo si rahisi kwa wachimbaji wadogo kuchimba kama vile Tanzanite tunakiri wazi kuwa maeneo ya kusini yaliachwa nyuma kimaendeleo lakini Serikali ilifanya makusudi,siku za karibuni nimetembelea maeneo mengi ya wilaya ya Monduli,Ngorongoro bado pia umasikini wa kutupwa upo tena sana tu ila ukifananisha Makao makuu ya Mkoa wa Arusha na Makao Makuu ya Mkoa wa Lindi Mkoa wa Lindi uko nyuma kiasi si sawa na Arusha ila umasikini kote upo!Wananchi wa Lindi wanahitaji ukombozi wa fikra kwanza kabla ya mambo mengine. CDM wanayo kazi kuwaelimisha, ukizingatia mtaji wa ccm ni wajinga.
Wananchi wa Lindi wanahitaji ukombozi wa fikra kwanza kabla ya mambo mengine. CDM wanayo kazi kuwaelimisha, ukizingatia mtaji wa ccm ni wajinga.
Nimeishi kusini miaka 10 na lindi mjini ndiyo nimeishi zaidi nikiwa nafanya kazi katika mashirika ya kimataifa vijijini. Nilishuhudia umaskini wa kutisha na mawazo mgando yaliyolalamika daima "sisi watu wa kusini tumeachwa, kuanzia kung'oa reli" hadi ukosefu wa barabara. Nimeshuhudia wanafunzi wa shule wasiovaa viatu na wasichana wamejifunga vipande vya kaniki wakiimba tuna imani na Mwinyi, Nyerere, CCM huku viganja vikilenga mapaji ya uso salamu ya chipukizi wa TANU youth league!!
Nimeshuhudia watu wakila mbegu za miti zenye sumu sana wengine wakifa!! na hata majani!!
Ndugu yangu kusini ni mtaji mkuu wa CCMAGAMBA yaani UMASKINI. Sasa kudanganywa kunatokana na ahueni ndogo!! ambayo wameipata au ni ujumbe kutoka kwa SALMA JK (First lady) mwenye uenyeji wa hapo MIKUMBI?
Simba wa Nachunyu vipi?? wamethibitiwa?
Ming'oko vipi bado inaliwa? Huo utajiri mlioletewa na CCM ni upi?
Nikitinga mitaa ya Mtanda, Jamhuri, Mitwelo, Kariakoo, Mikumbi, Mpilipili, Sabasaba; Manispaa ya Lindi imepambwa na bendera za CCM kukiwa na uchache wa bendera za Chadema. Wananchi wa Lindi wamesikika wakinena hawatadanganyika na kujiunga na chama cha Kaskazini, wao sio watu wa kufanywa wa mwisho. Hawatafanya kosa kuiacha CCM iliyoiunua maisha ya Lindi kuipitia sera nzuri mfano ujenzi wa barabara na mashule ya kumwaga.
hivi LINDI iko kwenye orodha ya mikoa ILIYOENDELEA au MASKINI?