Mimi ni customer care mstaafu ktk hii kampuni ya Vodacom uliyoituhumu kabla ya kupata mchongo government, naomba kuchangia kwa ufupi hii hoja yako.
Kuna kitu wanaita "FAIR USAGE POLICY"
"Fair usage policy" imejikita katika suala la kuwa "fair" ktk matumizi yako usije kuchukulia "ubwete" kwamba kwa Tsh 25,000 or whatever amount you paid udownload kitu hata cha Telabyte (TB)moja au mbili....hii inakuwa haiko "fair" kwa mtoa huduma kwani na yeye analipia hizo MB/GB/TB
Utofauti wa Unlimited bundles na zile ambazo ni "limited" ni kwamba Unlimited bundles ziko "capped" kwa 700mb (daily) 2GB (weekly) na 5GB (monthly) ambazo unaweza kuzitumia kwa high speed.
Endapo utafikia hyo "cap" iliyowekwa kabla ya muda wa bundle yako kuexpire hutokatiwa Huduma ya internet bali speed ndiyo itapungua.
Tofauti na limited bundles ambazo ukishafikia ukomo wa zile MB/GB ulizopewa basi net inakata kabisa.
Kuhusu speed, maeneo mengi ya TZ Vodacom wana tumia technology ya 3G ambayo kasi yake ya juu kabisa ya kubrowse iko 3.75mb/sec
Endapo unabrowse kwa slow speed (kama umeshafikia ukomo wa zile "capped" volumes zilizo ktk unlimited bundles inashuka hadi 0.2kb/sec.. Hicho ni kiwango cha chini kabisa kutegemea na network strength ya eneo ulilopo.. Ila huwa inapanda hadi 254kb/sec haizidi hapo.
Naamini utakuwa umeelewa japo kidogo, nakaribisha wengine wajuvi zaidi yangu wakuongezee.
Asante.