Kampuni ya Vodacom ni moja ya kampuni ya sim ambayo ilikuja na vifurushi vya chuo kwa wanachuo wanaotumia mtandao huo
Cha kusikitisha ni kuwa ghafla wamepandisha gharama za vifurushi kutoka 500 hadi 1000 pindua pindua,na mbs 500 kwa 1000 kwa saa 24 na kile cha wiki kutoka 1500 hadi elfu 2000 dk 150 na 1 GB
Vodacom wanapaswa kujua wanafunzi wanaotumia mtandao huo wanatoka familia za kimasikini hivyo wanapaswa vifurushi vyao viwe vya chini ili wanafunzi waweze kutafuta material bila shida
Vodacom hatukubaliani na mlichokifanya kwa wanafunzi wa kimasikini
Vodacom rudisheni gharama za mwanzoni za vifurushi vya chuo
Kama mnataka mfidie hela mliotoa kwenye rambi rambi ya MV Nyerere mseme lakini sio kupandisha gharama za vifurushi vya chuo kimya kimya,mnatuumiza bure