Voda watoa 4G LTE

Voda watoa 4G LTE

kwa sasa mitandao iliyo launch 4G ni tigo ttcl voda na airtel ila kwa sasa tigo ndio inayojulikana sana ttcl sio sana voda wao hawana wiki mbili ndio maana haijulikani sana na airtel ipo kwenye kwenye majaribio kuna watu wanatumia ila bado haijawa rasmi.
 
c2adf78b412a18f024e7e7d7536fd3b8.jpg
wangetoa halotel sipati picha 10GB za usiku
Tumia tu kiswahili ndugu yangu achana na lugha za watu hizi. Wana lunch ndo nini? Sema wana LAUNCH. nasisitiza tumia kiswahili.sema wanazindua.
 
Mkuuu simu yangu mim ni tecno f5 ambayo niliwahi kuwaconsult tigo kwa ajili ya 4G wakaniambia haisupport wakati kwenye setting zake ipo hiyo kitu ya LTE nashindwa waelewa hawa hebu nisaidie inakuwaje hii
 
unatumia tu mkuu.

Huwezi kutumia modem ya kawaida kupata 4G.Kuna modem maalum zinzotumia 4G.Nakushauri utafute universal Mobile wifi mfano Huawei E5377s-32 ambayo inasupport 4G itakuwezesha kutumia mtandao wowote kama band zake ni compatible.Kwa kutumia hiki kifaa hata kama simu yako haina 4G itapata 4G kwa kutumia wifi kutoka kwenye hiki kifaa
 
Mkuuu simu yangu mim ni tecno f5 ambayo niliwahi kuwaconsult tigo kwa ajili ya 4G wakaniambia haisupport wakati kwenye setting zake ipo hiyo kitu ya LTE nashindwa waelewa hawa hebu nisaidie inakuwaje hii
Simu inaweza ikawa ina support 4G lakini isikubali ya tigo ila ikakubali ya ttcl au smart ina tegemeana na frequency ya 4G ya simu yako kama inaendana naya mtandao husika basi utaenjo.
Cha msingi fuatilia simu yako inashiga 4G katika frequency gani?
 
Jamani hiyo MB 67 per sec ni kweli
kama wewe sio mtumiaji wa muda mrefu wa Vodacom unaweza usiamini, kwa kujiridhisha tu wewe mwenyewe jaribu kustream youtube video kwa kutumia EDGE ya Vodacom kisha njoo kwenye 3G,H, H+ kisha umalizie na LTE 4G ndio utajua kama ni kweli au uwongo
 
Mkuuu simu yangu mim ni tecno f5 ambayo niliwahi kuwaconsult tigo kwa ajili ya 4G wakaniambia haisupport wakati kwenye setting zake ipo hiyo kitu ya LTE nashindwa waelewa hawa hebu nisaidie inakuwaje hii

Tecno ni simu ya kichina
 
Hizi 4G haya makampuni ya simu hayajajipanga ninayo ya Tigo haina tofauti ile ya kawaida network mbovu jana nikasema niende kuulizia ya voda nione kama naweza kuswap hii ya sasa naambiwa niswap nitapoteza huduma zangu za mobile bank hivyo itanibidi nianze upya nimeona ni kusumbuana tu Hamna kipya
 
Mi simu yangu inasapoti "E" lakini kwa speed ya ku-browse nawaacha mbali sana wenye 3G, kwangu hili ni moja ya maajabu hadi nashangaa.
Halafu huwa nakuwa na mb 3 natumia masaa matatu Jamii Forums, mpaka nashangaa, mb 20 huwa nadownload nyimbo zaidi ya 8.
 
Mi simu yangu inasapoti "E" lakini kwa speed ya ku-browse nawaacha mbali sana wenye 3G, kwangu hili ni moja ya maajabu hadi nashangaa.
Halafu huwa nakuwa na mb 3 natumia masaa matatu Jamii Forums, mpaka nashangaa, mb 20 huwa nadownload nyimbo zaidi ya 8.
vyote vinawezekana lakini kwa masharti

1. unaweza mpita mtu wa 3g kama unatumia browser ambazo zinacompress data kama vile opera na ucweb hilo linawezekana ila kwenye full browser kama firefox, chrome, safari etc sahau 2g ni kimeo utasubiria dakika kibao kuload page moja tu

2. jamiiforums hasa version ya simu haili sana data inawezekana kabisa lakini usitegemee kila website iwe hivyo nna uhakika ukiingia site ya michuzi kabla yale matangazo hayajamaliza kuload unatumiwa msg kifurushi kimeisha.

3.na nyimbo unaweza kuwa na mb 10 ki thoery ukadownload nyimbo zaidi ya 100 lakini lazima ziwe na bitrate ndogo. usitegemee nyimbo yenye quality kubwa iwe na mb chache.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom