Linachimbwa kabuli, unavikwa sanda na unawekwa ktk jeneza, kisha unaombewa kama anavyoombewa maiti, then unazikwa na kufukiwa kabisa. Ukifukuliwa hapo kivuli kinakuwa kimefitwa, kwa hiyo unakuwa kama maiti fulani hivi ktk ulimwengu wa kichawi. Maiti hailogeki, kwa hiyo wachawi wakikutafuta inaonekana ulishafariki kitambo tu ma kuzikwa. Kuna mtu aliniambua alifanyiwa hii kitu. Ila tuendelee kutafuta maarifa kutoka kwa wajuzi zaidi
Hapo sawa ,,tukio kama hilo nilishuhudia kwa macho yangu
Miaka mingi iliopita nikiwa mdogo
Lkn skuelewa maana yake lkn nilipouliza nikaambiwa hivyo kua mtu huyu anakingwa,,nilipuuzia
Sasa mwaka 2012 nilienda kijijini kusalimia kufika nikamkuta yule mama ni mlemavu wa mguu hlf mwanae mmoja wa kiume amekua kichaa
Nikauliza kwa mzee mmoja hv wa busara ambae miaka ile ya 90+ nilimuona ktk tukio lile la yule mama
Ndo akaniambia kua yule mama alikingwa na viapo vilivyotumika ni kua yeyote atakae jaribu kumuondoa kwenye uso wa dunia basi aharibikiwe...
Sasa mwanae alienda kwa mganga kutafuta utajiri ndo akaambiwa mama yako ndo utajiri wako,,
Basi wakafanya yao na mganga
Kilichotokea yule mama aligongwa na gari akiwa nje ya nyumba hlf ukuta ukamfunika,,,
Aliumia mguu tuu na mbavu,
Baada ya hapo ndo mwanae akaanza kuropoka kila kitu alichofanya ,,
Mpk sasa jamaa kichaa
Mama yake maisha yanaenda
Haya mambo yapo