View attachment 365412Naandika nikiamini Ulishawahi kujiuliza kuhusu kivuli chako ama la kusikia walau kuhusu ushirikina unaohusisha kivuli. ...Lakini naamini kabisa hukuwahi kudhani kuwa unavyo vivuli vitatu
Vivuli hivi vitatu havionekani muda wote bali wakati wa jioni jua linapozama au usiku kwenye mbalimwezi angavu
Kivuli kidogo kabisa
Kivuli cha kati
Kivuli cha nje
Hiki kidogo kabisa ni kivuli cha ndani ni nafsi (roho + mwili )hiki ndio kinabeba utu au uhai kwa maana nyingine. Ni kupitia kivuli hiki ndio mambo yote ya kudhuru mwili hufanyika, ndio mzizi wa vivuli vyote
Kivuli cha kati ni daraja kati ya kivuli kidogo na kile kikubwa, yani ni kiunganishi kati ya roho na mwili. ndio hiki ambacho hutumika kuleta uhai tiba au marekebisho kwa kivuli kidogo kilichotekwa kufungwa au kuharibiwa kwa namna yoyote ile
Kivuli kikubwa hiki ni kivuli mwili kivuli cha kawaida kivuli kinachoonekana muda wote...hiki ni kivuli kinachobeba mwili uharibikao na kupotea ni kivuli jumba cha vivuli vingine vyote
View attachment 365413Kama ulivyo huu mchoro hapa haukamiliki ukitoa kipande kimoja ndani yake. hivyo hivyo na vivuli hivyo huwezi kuvitenga kawaida bali katika ulimwengu wa roho tuu
Kama ilivyo nafsi tatu katika mwili mmoja (me myselfand I)ndio hivyo hivyo ilivyo hata kwenye vivuli vya mwili wako
NB: mada hii ni kwa msaada mkubwa wa dada divine...