Vivuko vya Azam pale feri Dar es salaam kuna dalili za Ufisadi

Kuna Watanzania hawajali kabisa pale nchi yao inapofisadiwa. Wao kwa kuwa wanapata manufaa mawili matatu baasi, hawana mpango na manufaa mapana ya Taifa.
Hawana tofauti na Wale watu wanaowashangilia majambazi kea kupora pesa kisha wakamwaga chache barabarani watu wazigombanie ili wao wasepe kiulaini!
 
Nawaza tu hapa kwa nini wasiweke hata route nyingine ya hizo sea taxi ili watu wanufaike zaidi?
 
Nawaza tu hapa kwa nini wasiweke hata route nyingine ya hizo sea taxi ili watu wanufaike zaidi?
Umesema kitu cha maana sana..waanzishe route za kuja mbezi nk..itasaidia wengi kupunguza garama za mafuta ya magari na kuleta unafuu wakati huu mgumu
 
Mbona mie naona wako sawa tu. Vinapishana vizuri tu, halafu vya Azam havipakii magari...
Kuna watu hawana shukurani na watalalamika kwa lolote lile. Ndiyo hawa wanaolalamika kuhusu Azam.

Siamini kuwa vivuko vinawekwa kwa makusudi kwa muda mrefu ili kupisha vya Azam vifanye kazi. Shaurini aondoke halafu muje kulalamika tena kuwa vivuko ni vibovu.
 
Kabisa, watu wanahonga sana pale ili aweze kupata nafasi ya kuvusha gari, kusubiri kwenye foleni zaidi ya masaa 8 ni kitu cha kawaida sana kama una Kigari chako.
Mumewekewa daraja bado munalalamika kukaa foleni na gari kwa muda wa masaa 8, kwa lipi?

Hayo masaa ungeshavuka kwenye daraja kwa kulipia 2000 ukaendelea na safari zako kwa buheri na afya. Watz mumerogwa na nani?
 
Nimepita maeneo ya feri Dar es Salaam kwa ajili ya kuvuka kwenda upande wa Kigamboni. Nilichokiona pale kwa kweli kimenifikirisha na kunitafakarisha sana na kunifanya niwaze sana juu ya mustakbali wa nchi hii.

1. Kuna dalili kampuni ya Azam imepewa dili kinyemela kufanya kazi ya kuvusha watu feri

Mwanzoni, walitupiga changa la macho eti kuna tatizo la hali ya hewa, na hivyo kivuko cha Azam kimeletwa ili kusaidiasaidia. Cha ajabu mpaka leo hii hivyo vivuko vinaendelea kufanya kazi, wakati vile vivuko vya MV Kigamboni na MV Magogoni ni vizima.

2. Vivuko vya MV Magogoni na MV vipo na vinaendeshwa polepole Makusudi ili kuvipa nafasi vivuko vya Azam
Inaelekea kuna mpango mkakati wa kuwafanya watu wavizoee vivuko vya Azam pale feri. Nilichokishuhudia, Pale kuna vivuko vinne, Viwili ni vya Azam na viwili ni vya serikali(MV Magogoni na MV Kigamboni), Cha ajabu, Vivuko vya serikali vinaendeshwa polepole kuliko ilivyokuwa zamani.

Yaani nimeshuhudia MV Kigamboni ikikaa upande wa feri kwa takriban dakika 40, bila kuondoka huku Kivuko cha Azam kikiwa kimepiga trip mbili kwenda na kurudi kigamboni. Hii kama siyo hujuma kwa Vivuko vya serikali ni nini?.

3. Maisha ya wananchi yanawekwa hatarini kwa jinsi wanavyotolewa ndani ya sehemu ya kusubiria vivuko na kupangwa nje karibu na ukingo wa maji kusubiri vivuko vya Azam

Kikawaida watu huwekwa ndani ya hall la kusubiria kivuko, kikishafika geti linafunguliwa na kivuko kikishashusha watu na Magari ndo geti linafunguliwa na watu kuruhusiwa kuingia. Cha ajabu nilichokishuhudia leo, kwa kuwa vivuko vya Azam ni vidogo basi askari anawatoa watu nje ya hall ya kusubiria watu mapema kabisa kabla watu wanaoshuka hawajaisha. Maana yake ni iwamba Ujio wa kivuko cha Azam umeondoa hata kusudio la yale mahall ya kusubirisha abiria. Na hata usalama wa Abiria.

4. Ninachokiona
Huenda Kampuni ya Azam, inapewa dili na wakubwa wachache serikalini ili itoe huduma ya kuvusha watu licha ya kuwa vivuko vya serikali vipo pale.
Kampuni ya Azam kupewa kandarasi ya kutoa huduma siyo tatizo iwapo

1. Tenda inatangazwa kwa uwazi
2. Usalama wa wanajchi unazingatiwa ipasavyo
3. Serikali inapata faida

Kilicho dhahiri inaelekea Azam ya Mzee Bakhressa inapigiwa pande kinyemela ktk hii ishu, ambayo dhahiri shahiri kuna harufu za watu kuwa na 10% zao pale.

Hapa Chini ni picha ambayo wananchi wametolewa kwenye hall ya kusubiria kivuko, wamepangwa nje foleni wakisubirie kwa nje. Hii ni hatari sana, na ni very localView attachment 2468085

Hapa Chini, Kivuko cha MV kigamboni kimekalishwa zaidi ya dakika 40, huku kikiwa na watu ndani na magari huku Kivuko cha Azam kikipiga trip tu kwenda na kurudi, Sijui hawa Azam wanalipwa kwa idadi ya Trips wanazopiga?

View attachment 2468089
Hongera sana kaka, umefanya kazi ya TISS, wenye kazi yao wamelala.
 
Its like watu mnaoishi dar MNA shida sana sema mnajifanya mko sawa. Malalamiko hayaishi kila Siku ni mayowe,miano na makelele.
Hameni hamtachekwa.....kutwa kucha mnafarijiana tu kama wajawazito....maisha yenu yamejaa manung'uniko. Yaani vichwa vyenu vimejaa nywele badala ya akili.

Mnavojiona watu wa dili sasa hadi huruma.....kumbe kila MTU anamvizia mwenzake amtapeli.
 
Mumewekewa daraja bado munalalamika kukaa foleni na gari kwa muda wa masaa 8, kwa lipi?

Hayo masaa ungeshavuka kwenye daraja kwa kulipia 2000 ukaendelea na safari zako kwa buheri na afya. Watz mumerogwa na uliishawahi kufika hapo,na Daraja uliwahi kuliona limefikia wapi au unatumia hisia zako boga ulilobega mabegani mwako ,Tanzania hii kuna wazimu wa hali ya juu.

Mumewekewa daraja bado munalalamika kukaa foleni na gari kwa muda wa masaa 8, kwa lipi?

Hayo masaa ungeshavuka kwenye daraja kwa kulipia 2000 ukaendelea na safari zako kwa buheri na afya. Watz mumerogwa na nani?
Daraja halijakamilika, bado lipo kwenye ujenzi na hayo malipo uliyasikia wapi au unatumia hisia zako tu kuleta maneno ya jeuri wakati watu wanateseka .Maamae kabisa
 
Mv magogoni na vyezake haviko salama mtakuja zama mkakumbuka mwaka 1985 baada ya kivuko kuzama na kuua woooote
Haviko salama, ila hivyo viboti ndiyo salama?
Hizo taasisi zinazosimamia usala wa vyombo hivyo hawajui kazi yao, ila wewe ndiye unayejua usalama wa vyombo hivyo?
Basi nenda kaviondoe kabisa, ili kuokoa maisha ya watu kama wewe unajua havina usalama.
 
Hujaelewa nini? Amesema kuwa kuna hujuma ya kufifisha vivuko vya umma na kuachia Azam achume kilaini. Hili jambo linaweza kuwa na ukweli ndani yake kwani hii serikali ya sasa kila mtu anashindana kupiga deal.
Nimejibu vizuri kabisa, wewe ndie hujaelewa kwasababu sioni pointi yenu ya msingi hapa, mmejawa na hisia tu zisizo na uthibitisho..

Mkisema kuna hujuma ya kufifisha, hiyo hujuma imeanza lini? kwani hivyo vyombo vya serikali havifanyi kazi sasa hivi, kama vinafanya hiyo hujuma yenu inatoka wapi? na kama vinafanya kwa kusua sua kwanini isiwe kwa sababu ya uchakavu wa miaka yote, iwe hujuma mnayoilazimisha nyie?

Mmetawaliwa na mawazo ya kupigwa ndio maana sasa kwenu kila kitu mnakichukulia kwa hofu tu, wote mnaomuunga mkono mleta mada hamna uthibitisho wa uhakika wa madai yenu, zaidi ya kuhukumu kwa hisia tu.
 
Nimejibu vizuri kabisa, wewe ndie hujaelewa kwasababu sioni pointi yenu ya msingi hapa, mmejawa na hisia tu zisizo na uthibitisho..

Mkisema kuna hujuma ya kufifisha, hiyo hujuma imeanza lini? kwani hivyo vyombo vya serikali havifanyi kazi sasa hivi, kama vinafanya hiyo hujuma yenu inatoka wapi? na kama vinafanya kwa kusua sua kwanini isiwe kwa sababu ya uchakavu wa miaka yote, iwe hujuma mnayoilazimisha nyie?

Mmetawaliwa na mawazo ya kupigwa ndio maana sasa kwenu kila kitu mnakichukulia kwa hofu tu, wote mnaomuunga mkono mleta mada hamna uthibitisho wa uhakika wa madai yenu, zaidi ya kuhukumu kwa hisia tu.

Kama vyombo vya serikali vipo na vinafanya kazi, hivi vya Azam vya kazi gani wakati siku hizi vivuko vyetu vinatumiwa below capacity?
 
Daraja halijakamilika, bado lipo kwenye ujenzi na hayo malipo uliyasikia wapi au unatumia hisia zako tu kuleta maneno ya jeuri wakati watu wanateseka .Maamae kabisa
daraja la kurasini la Nyerere halijakamilika ujenzi wake, umelala usingizi wa aina gani?

Unadhani matusi ndiyo sifa? Mjinga mkubwa wee
 
daraja la kurasini la Nyerere halijakamilika ujenzi wake, umelala usingizi wa aina gani?

Unadhani matusi ndiyo sifa? Mjinga mkubwa wee
Nahangaika na mbeba boga Fala wa kukurupuka, mi naongelea kivuko cha busisi Kigongo Mwanza na pale daraja linalojengwa ni Daraja la Magufuli liko Mwanza. wewe uko kurasini,ndo nikasema kuna uhuni wa uliopindukia kuliko hata hapo Kigamboni, watu wanahangaika kuhonga mgambo wa Suma JKT wanaolinda pale ili wavushe magari, siku ukipita hiyo njia ndo utaelewa ninachokiandika, usome comment kwa utulivu na kuelewa sio kukurupuka na mimavi yako huko
 
Nimepita maeneo ya feri Dar es Salaam kwa ajili ya kuvuka kwenda upande wa Kigamboni. Nilichokiona pale kwa kweli kimenifikirisha na kunitafakarisha sana na kunifanya niwaze sana juu ya mustakbali wa nchi hii.

1. Kuna dalili kampuni ya Azam imepewa dili kinyemela kufanya kazi ya kuvusha watu feri

Mwanzoni, walitupiga changa la macho eti kuna tatizo la hali ya hewa, na hivyo kivuko cha Azam kimeletwa ili kusaidiasaidia. Cha ajabu mpaka leo hii hivyo vivuko vinaendelea kufanya kazi, wakati vile vivuko vya MV Kigamboni na MV Magogoni ni vizima.

2. Vivuko vya MV Magogoni na MV vipo na vinaendeshwa polepole Makusudi ili kuvipa nafasi vivuko vya Azam
Inaelekea kuna mpango mkakati wa kuwafanya watu wavizoee vivuko vya Azam pale feri. Nilichokishuhudia, Pale kuna vivuko vinne, Viwili ni vya Azam na viwili ni vya serikali(MV Magogoni na MV Kigamboni), Cha ajabu, Vivuko vya serikali vinaendeshwa polepole kuliko ilivyokuwa zamani.

Yaani nimeshuhudia MV Kigamboni ikikaa upande wa feri kwa takriban dakika 40, bila kuondoka huku Kivuko cha Azam kikiwa kimepiga trip mbili kwenda na kurudi kigamboni. Hii kama siyo hujuma kwa Vivuko vya serikali ni nini?.

3. Maisha ya wananchi yanawekwa hatarini kwa jinsi wanavyotolewa ndani ya sehemu ya kusubiria vivuko na kupangwa nje karibu na ukingo wa maji kusubiri vivuko vya Azam

Kikawaida watu huwekwa ndani ya hall la kusubiria kivuko, kikishafika geti linafunguliwa na kivuko kikishashusha watu na Magari ndo geti linafunguliwa na watu kuruhusiwa kuingia. Cha ajabu nilichokishuhudia leo, kwa kuwa vivuko vya Azam ni vidogo basi askari anawatoa watu nje ya hall ya kusubiria watu mapema kabisa kabla watu wanaoshuka hawajaisha. Maana yake ni iwamba Ujio wa kivuko cha Azam umeondoa hata kusudio la yale mahall ya kusubirisha abiria. Na hata usalama wa Abiria.

4. Ninachokiona
Huenda Kampuni ya Azam, inapewa dili na wakubwa wachache serikalini ili itoe huduma ya kuvusha watu licha ya kuwa vivuko vya serikali vipo pale.
Kampuni ya Azam kupewa kandarasi ya kutoa huduma siyo tatizo iwapo

1. Tenda inatangazwa kwa uwazi
2. Usalama wa wanajchi unazingatiwa ipasavyo
3. Serikali inapata faida

Kilicho dhahiri inaelekea Azam ya Mzee Bakhressa inapigiwa pande kinyemela ktk hii ishu, ambayo dhahiri shahiri kuna harufu za watu kuwa na 10% zao pale.

Hapa Chini ni picha ambayo wananchi wametolewa kwenye hall ya kusubiria kivuko, wamepangwa nje foleni wakisubirie kwa nje. Hii ni hatari sana, na ni very localView attachment 2468085

Hapa Chini, Kivuko cha MV kigamboni kimekalishwa zaidi ya dakika 40, huku kikiwa na watu ndani na magari huku Kivuko cha Azam kikipiga trip tu kwenda na kurudi, Sijui hawa Azam wanalipwa kwa idadi ya Trips wanazopiga?

View attachment 2468089
Mikutano ya hadhara inaenda kufumua kila uchafu na kila aliyehusika
 
Hata mimi ninashangaa watu humu JF wanaotetea mambo ya upigaji na ufisadi serikalini.

Azam amepewa hii tenda kinyemela, kimyakimya na kuna dalili za 10% za wakubwa katika hii huduma wanayotoa.

Ukifika pale Feri na Kigamboni, utaiona hujuma ya wazi ambayo vivuko vya serikali vinafanyiwa ili Vivuko vya Azam vipige kazi.

Yaani, Vivuko vya serikali vinakalishwa muda mrefu bila kuondoka, ili vya Azam vipige trip nyinginyingi maana abiria wanahaulishwa kwenye vivuko vya AZAM.

Kwa kuwa wenye magari hawana namna isipokuwa kuvuka kwa kutumia vivuko vya serikali basi wanapotezewa muda sana maana vivuko vya serikali vinakalishwa mno.

Pale feri kipindi kuna vivuko vya serikali peke yake hakukuwa na kuchelewa kuvuka, ulikuwa ukifika unakaa dakika chache tu za kusubiri. Kulikuwa na vivuko vikubwa viwili, vya Mv Kigamboni na MV Magogoni. Na vyote vilikuwa vinapiga kazi simulteneously, Kila kimoja kikienda upande mmoja kinakuta abiria wa kutosha wameshakusanyika, hakikai sana. Lakini leo vinasubirishwa ili Azam abebe abiria waliokusanyika huku vyenyewe vikikaa sana.

Hapa cha kujiuliza Azam analipwa sh ngapi kila tripu?

Tenda ilitangazwa lini?

Au wanamlipa kinyemela mzee Bakhressa aliwapa nini?

Kwa sasa uhitaji wa vivuko vya AZAM unatokana na nini wakati vivuko vya serikali vipo na vinafanya kazi vizuri?
Kweli kabisa Mkuu
Vivuko vya serikali vimekuwa mzigo..haviondoki kwa wakati hadi inalazimu abiria waliokuwa wamepanda kuanza kushuka kwenda kwenye kile kidogo Cha Azam.

Yaani Cha Azam kipo ng'ambo ya pili,Cha serikali kipo tu linasubiri abiria,
Cha Azam kinafika,Cha serikali hakijaondoka tu,
Cha Azam kinapakia,Cha serikali kipo tu hakijaondoka,
Cha Azam kinaondoka,Cha serikali bado kipo kimetia nanga.
Kwanini watu tusishuke?


Imefika kipindi kugombania kile Cha Azam imekuwa kawaida na ni risk maana watu wanadondoka.

Muda mwingine kunageuka bila abiria ili tu kuwahi upande mwingine,hivyo huwalazimu walinzi wafungue mlango watu wakakae pembezoni mwa maji kusubiri kuingia mara tu kikimaliza kushusha..kwa kweli kimepewa nguvu sana hivi vivuko kiasi kwamba wanafanya wanachojisikia.

All in all ,wanaoteseka ni watu wenye magari.


Hii nchi upumbavu ni mwingi sana.
 
Mv magogoni na vyezake haviko salama mtakuja zama mkakumbuka mwaka 1985 baada ya kivuko kuzama na kuua woooote
Kwamba hicho kidogo chenyewe kina guarantee ya kutokuzama?



Ambacho mara kadhaa kinanasa katikati ya maji kwa abiria kujazana mbele

Boti Kampuni moja ya Azam ikishapita na kutibua maji,basi mawimbi yake ya yanakiyumbisha sana na hakiwi stable wakati wa kutia nanga.


Ajali ni ajali.
 
Nina wasiwasi na ulichoandika hapo.

Nachokumbuka vivuko vya Azam vilipewa kazi baada ya vivuko vingine kuwa matengenezoni, hivyo pakawa na uhaba wa vyombo vya usafiri, ukawepo usumbufu kwa abiria, ndipo Azam wakaombwa kutoa hiyo huduma.

Kama kwa sasa pametokea hali isiyo ya kawaida, sioni kama hilo litakuwa ni tatizo la Azam, huo ni uzembe tu wa wasimamizi wa mamlaka ya usafiri huko bandarini.

Walichotakiwa kufanya kama vivuko vingine vilishapona, ni kusitisha mkataba na Azam, lakini kuwaacha Azam waendelee ni sawa na kukaribisha vurugu, japo pia, uwepo wa Azam unasaidia kuondoa adha ya usafiri inayokuwepo eneo hilo mara kwa mara.
Sasa wasiwasi wako uko wapi mkuu? Maana umeeleza vilevile alivyoeleza mtoa hoja
 
Back
Top Bottom