Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,086
- 6,568
Pesa za umma zinaliwa huku wananchi wakiteswa na tozo.
==
Ujenzi wa kivuko cha Mv Kazi uligharimu Sh7.3 bilioni na kina uwezo wa kubeba abiria 800 na magari 22 sawa na jumla ya tani 170.
Kupitia Ukurasa wa twitter wa TEMESA wamesema Kivuko cha MV. KAZI kimerejea rasmi katika eneo la Magogoni Kigamboni kwa ajili ya kutoa huduma baada ya kukamilika kwa ukarabati wake mkubwa uliogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 4.4. Kivuko hicho kiliondolewa kwenye maji baada ya kufikia muda wake wa ukarabati mkubwa.
Kilianza rasmi kukarabatiwa mwezi Juni mwaka 2022 na mkandarasi Songoro Marine Transport Boatyard katika Yadi yake iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam. Katika Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (5) 2020-2025,
Serikali inayoongozwa na Rais Dr. Samia Suluhu Hassan ilitoa ahadi mbalimbali kwa wananchi ikiwemo kuboresha huduma za vivuko hapa nchini ili kuwapunguzia wananchi kero za usafiri wanazopata katika maeneo mbalimbali kupitia Wizara mbalimbalina kupitia Wizara ya Ujenzi, Serikali imeanza kutekeleza ahadi hizo kwa kuanza kuvifanyia ukarabati vivuko hivyo.
==
Ujenzi wa kivuko cha Mv Kazi uligharimu Sh7.3 bilioni na kina uwezo wa kubeba abiria 800 na magari 22 sawa na jumla ya tani 170.
Kupitia Ukurasa wa twitter wa TEMESA wamesema Kivuko cha MV. KAZI kimerejea rasmi katika eneo la Magogoni Kigamboni kwa ajili ya kutoa huduma baada ya kukamilika kwa ukarabati wake mkubwa uliogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 4.4. Kivuko hicho kiliondolewa kwenye maji baada ya kufikia muda wake wa ukarabati mkubwa.
Kilianza rasmi kukarabatiwa mwezi Juni mwaka 2022 na mkandarasi Songoro Marine Transport Boatyard katika Yadi yake iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam. Katika Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (5) 2020-2025,
Serikali inayoongozwa na Rais Dr. Samia Suluhu Hassan ilitoa ahadi mbalimbali kwa wananchi ikiwemo kuboresha huduma za vivuko hapa nchini ili kuwapunguzia wananchi kero za usafiri wanazopata katika maeneo mbalimbali kupitia Wizara mbalimbalina kupitia Wizara ya Ujenzi, Serikali imeanza kutekeleza ahadi hizo kwa kuanza kuvifanyia ukarabati vivuko hivyo.