Vituko vya Maisha ya Boarding, Tukumbushane Tuliosoma Huko

Vituko vya Maisha ya Boarding, Tukumbushane Tuliosoma Huko

sisi tuliosoma Boarding za miaka ya warrant za Govt ndio tulifaidi
mnakutana na watoto wa Tabora girls, Jangwani, Weruweru, Korogwe nk
na mawasiliano ni barua unachora na moyo uliochomwa na mkuki.
Umenikumbusha mbali. Wanafunzi wa Korogwe, Tanga School, Galanos na Magamba kutoka Dodoma, Tabora, Mwanza, Bukoba n.k. tulikutana Ruvu baada ya kushuka tokaa train ya bara na kusubiti train ya kutoka Dar. Hapo ndio watu wanapata watu wao.. Ukirudi shuleni tegemea barua yenye picha ya moyo uliotungwa mshale na picha. Kuna kuandikiana kwenye autograph.
 
Siku ya kuondoka baada ya mtihani wa mwosho ndo kasheshe. Watu wamelia. Tanga Tech
 
Changanyikeni watoto wa o level walikua wanatoroka wanakwenda UDSM wanachukua msosi uliobaki cafeterias wanaleta tunakula
Tulikua tunapiga mchango lilikua linaitwa ZIGO
KUNA SIKU NIKAKUTA TOOTHPICK na KISODA ulikua mwanzo na mwisho kula zigo
 
Umenikumbusha mbali sana kiongozi,namshukuru mwl.Mwakasege kwa kutuunganisha na Loleza angalau mara mbili kwa disco kali kwa mwaka.Wenyewe wakija disco Iyunga wanakuwa wamejiandaa yaani kufuli wanakuwa wameziacha kwao
Team iyunga na loleza now days inakaribia bond kufa
 
Ticha mmoja hivi kupenda kutuamsha kwa kutuchapa,tukamwaga ulezi chini alikula mweleka mpaka kukosa fahamu,aliacha mtindo huo.😱😱😱😱
 
Ifunda the Glorious! Choo cha Mabanzi (Karume). Watoto wa Kaguo, Nkondokaya. Rip Masala, Per Time T.
 
Nilikutana na mchizi wangu baraka anapenda kuangalia video si mchezo, ikawa ni kutoroka kila night hakuna cha prepo wala nini tunazama kibanda umiza.

cheki movie mpaka ngoma 6 inawekwa pilau aseeh, siku moja ma njagu wakatuotea kibanda umiza tunacheki pilau wakatudaka watu kama 8.

hapo tukilala kituoni ni msala skuli, kufukuzwa nje nje ilibidi tuwaambie ukweli sie wanafunzi tuwape mkwanja flani watuachie wakakubali ikawa pona pona yetu.

Matukio ni mengi sana, niliweka wali kwenye tranka mjinga flani akalitingisha juu chini chini juu daaa! nguo zilitapakaa wali si kidogo
Daah mkuu umeniua mbavu
 
Wazee wa lubala sec kulikua na msosi flani tulikua tunauita wakumchinja ulikua unapigwa ngoma nne usiku ukitoka prepo Mzee ulikuaga ni mtamu ukitia muungo alafu ulikua wa bariiiiiiidi kudadeki ukitoka hapo tumbo limejaa gesi ni kuachia yusuph kwa kwenda mbele usiku kucha na mabweni yenyewe yalikua kama wodi ya wazazi usiku wa saa 8 ukibahatika kuamka utadhani kuna mashindano ya kujamba yani ni kupokezana akiachia huyu linapokelewa na yule
Wakumchinja ule msosi sirudii kuula asee

Bording ni shidah
 
Unakula domwork na uji asubuhi kama huna hela ya kununua andazi (domwork ni ugali maharage/kande za Jana ake)!
Wale wenzangu wa kutumia simu tulikua na lugha yetu vocha tunaiita maunjanja so unauliza mwenye maunjanja aniuzie au ukienda duka la shule unamwambia muuzaji nipe maunjanja ya jero anakua ashaelewa! Sitasahau siku teacher kaja kutuamsha week end tuende prepo wakati week end ilikua free acha mwalimu achezeee!! Nmepamisi Rungwe boys
 
Aisee mzee umenikumbusha mbali sana , maana maisha ya boarding yalikua yenye raha na noma. Sintasahau siku ya mtoto wa form one alivyokwenda kunishatakia kwa second master kama huwa nawachapa viboko na kuwalaza nje ya bweni, siku ilipofata niliitwa mbele ya wanafunzi wenzangu kipindi tupo mstarini na kuamuriwa nirudi nyumban na kurudi na mzazi ili hapo nilikua napiga push up mpaka walipotawanyika....aisee sintosahau
 
Ukweli Boarding lazima uikumbuke tu hataiweje, Miaka ya 87 jamaa yangu yeye hali ilivyokua ngumu siunajua nyama haionekani mpa siku maalumu?nakumbuka ilikua weekend alisikia mbuzi wanalia maeneo ya shamba la shule,,hakuaga mtu akaanza kunyata tariiitiiiibuuu hamadi mbuzi,akajitahidi akamkamata mmoja akafikiria sasa mbona mzimamzima hii itakua soo,mbuzi akaanza kupiga kalele mmmmeeeeeee akasema sasahiibalaaa akamziba mdomo aaaaa wapi mvuzi anaendeleaa tu,ikamjia akili yaharka alifikiria kumchinja,akaona hapana siaka mkata paja moja la kulia kisha akamuachia,akalificha juu yamti kisha akarudi bwenini,akatusitua oyaa chukuen chumvi mnifuate(huwezi amini tumefika akashusha mzigo ukachomwa fasta ukapigwa kimya kimya)ukweli mbaya sanaaaa
 
Back
Top Bottom