Vituko vya Maisha ya Boarding, Tukumbushane Tuliosoma Huko

Vituko vya Maisha ya Boarding, Tukumbushane Tuliosoma Huko

Nilikutana na mchizi wangu baraka anapenda kuangalia video si mchezo, ikawa ni kutoroka kila night hakuna cha prepo wala nini tunazama kibanda umiza.

cheki movie mpaka ngoma 6 inawekwa pilau aseeh, siku moja ma njagu wakatuotea kibanda umiza tunacheki pilau wakatudaka watu kama 8.

hapo tukilala kituoni ni msala skuli, kufukuzwa nje nje ilibidi tuwaambie ukweli sie wanafunzi tuwape mkwanja flani watuachie wakakubali ikawa pona pona yetu.

Matukio ni mengi sana, niliweka wali kwenye tranka mjinga flani akalitingisha juu chini chini juu daaa! nguo zilitapakaa wali si kidogo
ahahahahahaha ahahaha ahaha nimecheka sana alivyotingisha tranka
 
kupiga simu chooni, kuvuta mjani, kugonja walimu wa kikeni waliokuwa wakija field, kuuza biskuti, kuvunja makontena ya vilaza, watu tulikuwa na funguo zaid ya 500 hizi ni za kupampu makufuli, wakati tuko shule, tunamiliki shamba bondeni, la nyanya na miwa, kupiga walimu wanoko mida ya prep, kutoroka usiku tunaenda mlima zinaa, kulala ktk mabweni ya wasichana na wasichana kujichanganya ktk mabweni ya masela, kuingia class na vi bom, kupiga simu chooni, disko vumbi, kuwekeana mafta ya taa ktk chakula, kuchambia godoro, kulamba sahani baada ya kula, kupiga passpot size, njuka mnyonge alibanduliwa au kunyonya rungu, kufunga mawe ktk mataulo kisha taa inazimwa dakika tano, muda wa kufunzana adabu, hii kila siku saa tano usiku, kupakana losheni, au kuvunjiwa yai ukilala kisha wanasingiziwa vibwengo, kuuza magodoro ya walioingia darasani wiki dume, godoro linabadilishwa na sahani ya wali maharage, mchaka mchaka saa kumi za usiku kisha mnafuata maji ya kuoga chini ya mlima..na mwisho tukachoma shule moto kisa hawakutupikia wali wiki mbili mfululizo....nilikuwa waziri wa chakula, kampani yangu walijaziwa kuliko maadui zetu, sisi chakula tulikuwa tukiweka katika ndoo ya lita 20 watu watano, tulikuwa wanafunzi 1200 lakini nyama inapikwa kilo kumi na tano tuu, hapo waziri wa msosi nachoma kilo moja na ikiiva najaza kisado, wengine wanakunywa supu...tulibadilishana wali kwa penzi....pamoja na yoote, darasani tulikuwa vizuri....mvua ikinyesha woote tulitoka nje uchi tukioga...kutokana na utukutu niliokuwa nao, pesa ya matumizi nilipewa buku na panadol tu, lakini nikirudi rikizo nilikuwa na zaidi ya laki tatu...
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nakumbuka sana maisha ya boarding pale Minaki High School tuliacha madarasa na mabweni na kwenda kutia msuli forest ambako tulihisi hatusumbuliwi na mtu yeyote yule ila mwisho siku kilieleweka.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]hukuwah kwenda kisarawe kuchek mpira ucku?
 
Boarding school(boys) ya advance ndio imenifundisha puny....E t 0...
Kuna kipindi tulikuwa tunaweka mashindano kabisa ya kurusha sperm kwa umbali mrefu mshindi anapata hela ya maandazi ili asipulize(asinywe uji mkavu) dah yale maisha ya kijinga sana sasa sijui kwann tulikuwa tunafanya vile
====
Mtwara Tech tulikuwa na mashindano bweni la Mwongozo nani anaweza kuclick kwa haraka. Nilishindwa na jamaa mmoja yaani akijigusa tu zimetoka kama mwehu vile.
 
Sikumoja ilifanyika especion ya nguvu lengo kutafuta simu uzuri kulikua na walim wetu vijana hua wanatutonya, istoshe mimi ndo nilikua fundi simu ilibidi nikafukie vifaa vyote shimoni kusubir hali itulie.
Na ma~spay nao hawakua nyuma

Inspection?
Spy?
 
Now uzio kila kona...
Pale mashineni pamewekwa uzio na gate dogo.... Na uongozi WA sasa hatari.....
Hahaha.....duuh kweli maisha yamekwenda Kasi sana,nikipata nafasi nitakwenda mbeya angalau kusalimia.
 
1.tulikua tuna dodge prepo ,kusoma mpk paper ikaribie
2.jioni kwenda kula migahawani (nyumba ya mtu ila ni mgahawa)
3.kupiga stori usiku kucha (walikuepo ma chairmen)
4.kuna watu kufua soksi mpka siku ana kipindi computer lab,au anaenda library
5.tukitoka class saa 9 tunaenda kula wali ambao ki msingi tunatakiwa kuula jioni saa 12,ila sisi kwa kua tulijiita ma staff tuliula tu ,ukiwa wa motooo
6.siku za sherehe tunaiba nyama ,unakula kama nusu nzma peke yako
7.ijumaa tunaenda kula nguruwe ,
8.ku diss walimu
9.kuweka sukari nyingi kweny chai ili kuikomoa shule
10.kuwasha feni za darasani mchana kutwa ili kufidia ada
Dah so much memory ahlulbayt islamic
 
ahahahahahaha ahahaha ahaha nimecheka sna alivyotingisha tranka
yule bwana ni mpuuzi sana alijua kasha tingisha tranka hakuna wali tena mule basi mie mchana nikakataa ugali nikijua nitaenda kula wali mida.

akawa anacheka sana akiniangalia, anasema "utalala na viatu, utaula wa chini" asa mie sielewi naona anazingua tu.

kwenda kufunua tranka daaaaah!!! mpumbavu sana yule jamaa
 
nimesoma shule ya kanisa kila siku saa 11 kuamka kujiandaa na misa, nikawa mvivu flani kila siku napanda darini kutega kwenda misa ya asubuhi

siku moja mlezi kanikurupua nikapanda darini fasta, badala ya kukanyaga mbao nikakanyaga ceiling board. nikashukanalo mpaka chini.

mlezi akaanza piga kelele mchawiiiiii, mchawiiii hahhah alinipiga sana na adhabu ikawa kukaa bench la mwanzo kila siku kwenye misa.
 
Kuna jamaa alikua na ki nokia tochi wenzie wana smartphone bwenini,sas watu wny smart full kupg miziki,jamaa akaona sio tabu akawa anapiga miziki ile ya nokia torch ,
 
nilimwagiwa yai takoni wakasahau kuondoa maganda......niliwapa kisago member wa room mpaka sasa wananikumbuka...!!!
Hahahahaaah khakha ,kwahiyo mkuu wewe kilicho kuuma ni hayo maganda ya yai kuachwa matakoni ? Lakini kitendo cha kumwagiwa yai takoni fresh tu huja mind ?
I wonder mpka wanakuvua ilikua ni katika mazingira gani,all in all pole sna mkuu
 
Unakula domwork na uji asubuhi kama huna hela ya kununua andazi (domwork ni ugali maharage/kande za Jana ake)!
Wale wenzangu wa kutumia simu tulikua na lugha yetu vocha tunaiita maunjanja so unauliza mwenye maunjanja aniuzie au ukienda duka la shule unamwambia muuzaji nipe maunjanja ya jero anakua ashaelewa! Sitasahau siku teacher kaja kutuamsha week end tuende prepo wakati week end ilikua free acha mwalimu achezeee!! Nmepamisi Rungwe boys
Mkuu rungwe boys mwaka gani hyo!!?
 
Nakumbuka pale Mpwapwa sekondari siku naingia tu nikapelekwa Laundry hall nikapewa redio flani hivi ya kukoroga ndio ipate nishati mana haitumii betri.

Wakongwe wanacheza mie nakoroga. Nikichoka wanakuja kunitia vibao na kusema Nyoka hachoki.
 
Kuna kiranja mnoko,mimi na group langu tulipanga mpango wa kumwagia maji usiku akiwa amelala kupitia dirishani kwake,mimi nlipewa jukumu la kutekeleza,basi nikabeba maji ndoo nzima nikamwagia kupitia dirishani lakini lo kumbe jamaa hakulala pale kitandani alikuwa amempisha mwanafunzi mwingine aliyekuwa hoi anaugua malaria,kitendo hicho kinaniumiza mpaka leo.
 
Maisha ya shule za Bweni ama Boarding kwa lugha ya kiingereza, ni sehemu ambayo imewajenga ama kuwabomoa watu wengi waliowahi kuyaishi.

Katika Thread hii ningependa tukumbushane visa,mikasa na moments za kukumbukwa katika maisha ya board

Hapa tunaongelea shule za boarding kabla ya ujio wa shule katika kila kata.

ELIMU
Wakati huo miaka kabla ya miaka ya 2002`s shule za serikali ndio zilikuwa zinaongoza kwa ubora na shule za vipaji maalumu zilitikisa haswaa kwa ubora wake,shule kama Mzumbe,Ilboru,Kibaha,Bwiru Boys,Malangali,kilakala,ndanda,Moshi Tech, na nk,zilikuwa bora sana.kwa hivyo ilikuwa fahari kubwa sana kusoma katika shule hizo maana elimu ilikuwa bora sana.

UTEMI,
Nyakati hizo watu walikuwa wanaanza darasa la kwanza kwa kupitisha mkono katika sikio upande wa pili,hivyo mpaka kufika sekondari watu walienda wakiwa na umri mkubwa na miili mikubwa.Wanafunzi wa kidato cha kwanza walikuwa wakikumbana na utemi,kama kupigishwa simu kwenye matundu ya vyoo,kufua na mikwara Mingi iliyowapa usugu.Haikuwa ajabu watoto wakifunga shule wakirudi nyumbani wakiwa manunda,vyote vilikuwa nyakati hizo.

MAHUSIANO
Wapo wengi Leo hii wameoana lakini mapenzi yao yalianzia toka shuleni.Njia ya mawasiliano zilikuwa ni barua,watu wametumiana sana barua zilizotiwa nakshi ya nyimbo za kiingereza za kimahaba za enzi hizo,ilikuwa sifa na ukidume kuitiwa barua yako mkiwa assemble.Nyakati hizo madisco ya shule,michezo vilizalisha mapenzi mengi sana.

MAADILI,
Wapo walioenda kujifunza tabia njema kama namna ya kuishi na watu,wapo pia waliojifunza tabia mbaya zinazowagharimu mpaka kesho.
Michezo ya kupiga punyeto ilikuwa common sana mashuleni,wapo waliokuwa wataalamu wa kutumia sabuni,mafuta ya kupaka na kutoboa magodoro katika kujichua.
Wengine walidumbukia katika ulevi,Wizi hata ushoga na usagaji katika maisha ya shule.

Ya kale ni dhahabu na hakuna awezaye kuzirudisha nyakati nyuma lakini tujikumbushe enzi hizo,nyakati ambazo maisha ya boarding yalimfanya jay moe ayatungie wimbo akimshirikisha Dully.Nyakati hizo boarding life ilikuwa boarding life,

Tuzirurudishe hisia zetu nyuma
 
Back
Top Bottom