Vituko vya Maisha ya Boarding, Tukumbushane Tuliosoma Huko

Vituko vya Maisha ya Boarding, Tukumbushane Tuliosoma Huko

Kujitumia barua mwenyewe na kisha kwenda kuifungua na kuisoma mbele ya wenzako yenye maelezo demu wa loleza amekupenda sana.IYUNGA TECH,PCM
Umenikumbusha mbali sana kiongozi,namshukuru mwl. Mwakasege kwa kutuunganisha na Loleza angalau mara mbili kwa disco kali kwa mwaka.Wenyewe wakija disco Iyunga wanakuwa wamejiandaa yaani kufuli wanakuwa wameziacha kwao
 
Magodoro ya bwenini yalikusanyika na kuuzwa kijiji cha jirani siku ya kuondoka shule pesa yote heshima baaa kesi waliachiwa njuka wakubwa wamesepa kwi kwi kwi
 
Hahah jamani lile baridi la asb mchaka mchaka dah. Maisha ya boarding yalinifanya nikachangamka hadi leo.
 
Umbwe secondary uji wa saa 12 asubuhi tulikuwa tunaita ''fongo'' ukiwa hauna sukari tulikuwa tunasema ''fongo chuma''..ukikamatwa unarudia(pepa two) msosi adhabu unadeki jikoni wiki nzima..
Hahaha yaan umenikumbusha mbali, mambo ya pepa 2 hahaha.
Mimi nilisoma girls tupu ila kulikuwa na mamdada maoneaji aisee halafu mabaunsa kama wanaume basi siku ya wali mtashangaa tu taa za dining zinazima zote zikija kuwaka masahani yote yako tupu. Wenye nguvu zao walikuwa wanajaza wali hadi kwenye ndoo na wali unalika hata siku tatu bila kupashwa.
 
Shy Bush pale msituni, nilijifanya mjuaji nilivokwenda form five vijana wa O-level wakaiba chaga halafu wakaegesha godoro nilivorudi kutoka mess nikajiachia kitandani.
Nilichokutana nacho ni ngumu kusimulia.
Duh mkuu pole sana
 
Sumve kulikuwaga na shida ya maji, mweh! Yaan ilikuwa maji yakikatika shuleni mnatumia siku nzima kufuata maji tu.
Mpishi sasa mama Yunge(rip) alikuwaga mkali sitakaa nimsahau.
Kuibiana sare za shule, sahani, mashuka ilikuwa kawaida sana.
 
Hahaha yaan umenikumbusha mbali, mambo ya pepa 2 hahaha.
Mm nilisoma girls tupu ila kulikuwa na mamdada maoneaji aisee halafu mabaunsa km wanaume basi siku ya wali mtashangaa tu taa za dining zinazima zote zikija kuwaka masahani yote yako tupu. Wenye nguvu zao walikuwa wanajaza wali hadi kwenye ndoo na wali unalika ht siku tatu bila kupashwa.
iyo ya wali kukaa siku tatu bila kuharibika hapo ndipo paliponishangaza mno
 
Kuna siku kichaa aliingia ndani ya uzio wa shule akagonga kengele saa nane usiku weeee watu waliamka na vyupi, nightdress na wengine wamevaa kabisa uniform ilikua kichekesho cha mwaka. Hahhaahaahh
 
Boarding ngumu ni zile za boys tupu, mi nimesoma Bwiru boys kipindi hicho.
Nakumbuka nina siku 3 toka niingie form 1 akaja 4m4 mmoja pande la mtu ananmbia dogo hebu njoo hapa nikaenda akaanza kunambia eti dogo nina notes zangu counter 3 nataka uje bweni fulan uniandikie, nikamwambia bro niko busy siwezi sahivi eti anauliza form one uko busy, nikamwambia bas ntakuja kuchukua, basi kuanzia hapo ikawa kila nikimuona nakula winga mwishowe akiniona anacheka tukawa washkaji

Watu tulokua na vipaji kama vya kucheza mpira hatukupata shida kiviile maana zikitaka kuanza ligi za mabweni kila dom prefect anataka uamie kwenye bweni lake. Japo boarding ni kama kambi ya jeshi
 
Kuna jamaa lilikuwa jizi la ugali noma sijui sikuhizi liko wapi? Ila wale wenyeviti wetu wa starehe walishakufa wote sijui walipataga laana gani!
 
Umbwe secondary uji wa saa 12 asubuhi tulikuwa tunaita ''fongo'' ukiwa hauna sukari tulikuwa tunasema ''fongo chuma''..ukikamatwa unarudia(pepa two) msosi adhabu unadeki jikoni wiki nzima..
Umbwe mlikua wanoko kama dada zenu wa weruweru
 
Back
Top Bottom