Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

Pole!
IMG_20220706_155127_217.jpg
 
Update: Pichani wanandoa hao ambao mume amepitwa miaka 37 na mke wake huyo wametangaza kutaka kupata mtoto ambapo watatumia shilingi milioni 333.7 na tayari wamempata mwanamke wa kumuajiri awabebee mimba

Mke huyo anaitwa Cheryl ana miaka si chini ya 61 wakati mume wake huyo anaitwa Quran McCain(24) ambapo kwasasa wanaishi Rome, Italia baada ya kufunga ndoa mwaka 2021

Cheryl tayari alishazaa watoto 7 na ana wajukuu 17 katika mahusiano yake ya mwanzo, lakini Quran yeye bado hana mtoto kwahiyo wameamua ili kulinogesha zaidi penzi na ndoa yao basi wapate mtoto ambapo mbegu tayari wameshapata mwanamke wa kumuajiri awabebee hiyo mimba na watatumia jumla ya gharama £120,000 ambazo si chini ya milioni 333.7 za Kitanzania

Wamesema wanapendana sana kila mmoja anamfurahia mwenzie ambapo penzi lao lilianza kipindi cha nyuma baada ya mwanamama huyo kuachia video mtandaoni akicheza muziki kisha watu kuanza kumchamba na kukosa furaha ambapo Quran alianza kumfariji na baadaye penzi kuchanua na hatimaye kufunga ndoaView attachment 2283164
Yaani tukio moja lakini vituko vipo vingi ndani yake

1.mpishano wa umri (mume alifaa awe mjukuu na mke awe nyanya)
2.mpishano wa mshkaji na jina lake (anaonekana bishoo lakini jina lake "Quran" ni maneno matukufu yanayoongoza waislamu)
3.mpishano wa umri na sura ya mwanamama (umri unaonesha ni mzee ila sura anaonekana kikongwe)
4.wanataka mtoto (huku wakijua kabisa hawezi kuzaa)
5.wametafuta mtu wa kubeba mimba (duh...)
Na kadhalika
 
Back
Top Bottom