Hawa jamaa walikuwa ni wanariadha huko marekani miaka hiyo 1968 walishiriki mashindano ya Olimpic mji wa Mexico city,mmoja alimaliza wa tatu mwengine wa kwanza.hii picha iliingia kwenye kumbukumbu ya wamarekani weusi kwa kunyenyua kila mmoja mkono huku amekunja ngumu huku wamevaa soksi za mkononi kama ishara ya kupinga uonevu wa watu weusi huko America kama tuonavyo leo Black Lives Matter.mmoja alonyoosha mkono kushoto mwengine mkono wa kulia.kwa sasa sijajua wanaendesha vipi maisha yao ila waliungwa mkono na jumuiya za wanaotetea haki za watu weusi marekani.Pia walicheza American footbal .japo waliporudi marekani walitishiwa sana maisha kwa kitendo chao cha Kuinua ngumi juu kama dharau ya wimbo wa taifa ila kwa wamarekani weusi kilikuwa kama kitendo cha kishujaa.