Vitu sita ambavyo si viumbe vya Mungu

Vitu sita ambavyo si viumbe vya Mungu

"Tunaambiwa Mungu ni mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote."

Unless na wewe ni mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, ndiyo unaweza ukawa kwenye nafasi ya kuhoji juu ya qualities hizo za Mungu, vinginevyo much far huwezi. Na kama basi hauko hivyo, hakuna namna ambayo unaweza ukajua ni wapi unakosea na wapi uko sahihi katika kutoa hoja zako juu yake. Zaidi ni kuwa Mungu ni Roho, hana mwili na haonekani kwa macho, na hivyo sikuwa namaanisha kuwa ulitaka athibitishwe kwako physically. Pamoja na hayo, kuna emperical evidence nyingi tu zinazoweza kuthibitisha kuwa Mungu yupo lakini zinakuwa ni za kiroho zaidi na ni unique experiences ambazo ukimdai mmoja azithibitishe kwako, inakuwa ni kazi ngumu kidogo unless na wewe uwe kwenye line sawa na yeye katika ulimwengu wa roho. Kwa hiyo mambo ya kiroho si ya kuibuka tu halafu unamwambia mtu akuthibitishie wakati hata hauko aligned naye kiroho au hauko kwenye imani moja naye. Kama wewe ni atheist au non believer, hakuna namna NZURI zaidi ambayo mtu ambaye anamwamini Mungu anaweza akamthibitisha Mungu kwako. Wanaomwamini Mungu wanatumia standards zao ambazo zinatokana na Maandiko Matakatifu, wewe usiyemwamini, hutumii hayo na wala haukubaliani nayo. Hii tayari ni discrepancy kubwa kabisa ambayo haiwezi kuwafanya arguments zenu zikaja kukubaliana mbele ya safari hata siku moja.

Mfano wa emperical evidence ambayo ni ya kiroho ni ndoto. Kuna watu wengi tu huwa wanaongea na Mungu kupitia kwenye ndoto au hata maono mengine yanayofanana na hayo. Sasa mtu kama huyu akikupa shuhuda zake juu ya uwepo wa Mungu, kwa mtu kama wewe ukimwambia kuwa anakudanganya utakuwa uko sahihi 100%, ila hata ukimkubalia pia utakuwa uko sahihi 100%.

Still, uelewa wangu wa siku nyingi tangu huko nyuma, nilikuwa najua kuwa wewe huamini kama Mungu yupo kwa sababu wanaomini kuwa yupo, hawajaweza kukuthibitishia hilo!

Mwisho, je kutokana na maelezo yako hapo juu, unataka sasa wanaomwamini Mungu wamthibitishije kwako? Watumie standards zipi, za kwao za kwako? Kumbuka kuwa hapa lazima standard mojawapo tu ndiyo inatakiwa itumike, ya kwako au ya kwao ila si zote mbili. Nauliza maswali haya kwa sababu leo nimegundua kuwa wanaomwamini Mungu wanao uwezo huo wa kukuthibitishia kuwa Mungu yupo isipokuwa tu walikuwa hawajawahi kulielewa swali lako la siku nyingi!

NB: Kumbuka pia kuwa hoja yangu kubwa hapa ni kwamba, arguments za uwepo wa Mungu kuwa illogical kwako, bado hakumfanyi Mungu asiwepo
Ili kitu kiwe kweli, na si uongo, inabidi kikidhi vigezo gani?
 
mkuu point kubwa kwanza ni kujua na kukubali kwamba kila kitu kimeumbwa na kiumbe chenye nguvu nyingi na akili nyingi sana kuzipitia hizi akili zetu duni za kibinadamu,

kuna kiumbe ambacho kina uwezo mkubwa sana kuweza kututokeza sisi wenye akili za kutengeza complicated machines like hizo ndege,submarines,na vingine vingi

Mungu katoka wapi hilo ni swala jengine mkuu
Ni lazima kilicho complex kiwe na muumba? Au si lazima?
 
Ujinga na umasikini tu. Mtu hajapata kipande cha muhogo kutia tumboni unafikiri anaweza kuwa na muda wa kuchambua "the problem of evil"? Anataka kuambiwa piga magoti uombe mungu atakujaalia. Ndiyo maana Northern Europe watu walikoelimika Zaidi na kuweza kutatua matatizo ya msingi makanisa yako empty na huku kwetu Africa ambako bado tuna ujinga na umasikini watu wanajazana.
Hivi ni vitu viwili msingi kwa mtu katika kujua ukweli, navyo ni Elimu na Maarifa.

Hatahivyo, kusoma yaani kuwa na elimu sio kuwa na maarifa. Lakini kuwa na maarifa ni kuwa na elimu.

Ukifanikiwa kuwa na maarifa utaelewa, hasa kwa upande mmoja "ukweli" na kwa upande mwingine "ukweli wa elimu".

Ni kweli kuwa Afrika kuna umasikini pia kuna ujinga. Lakini, je, vitu hivi: yaani "umasikini" upo Afrika kwa sababu Waafrika hawafikiri au hawana elimu? Na "ujinga" upo Afrika kwa sababu Waafrika ni wavivu kujifunza?

Umesema, Northern Europe, ukataja watu walioelimika... makanisa yako empty... Fikiri kwa mfano, Kanisa Katoliki au madhehebu mengine viongozi wake ni watu gani?

Hoja kama hii haina ukweli wowote. Kwa sababu kanisa lisifafanuliwe na kueleweka kuwa ni jengo au mahali pekee, bali Kanisa ni "mwili".

Kuhusu " the problem of evil", ni vema kujua kuwa Kanisa linashughulika na "dhambi" 'sin'. Kama kuna evil, basi ni kwa sababu ya dhambi. Hivyo hoja kwamba, Kanisa (dini) ni kwa ajili ya social functions, the problem of evil ni madai yalishindwa kuelewa ukweli. Hivyo ni opotoshaji na uzushi.
 
mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote aumbe ulimwengu ambaobmabaya yanawezek
Taarifa kwamba haya ni mabaya, yaani kujua kwamba haya ni mabaya inasikika kutoka kwa nani?

Na utambuzi huu au sauti inayokuambia huu au hiki ni kibaya au ubaya huja baada ya nini na nani kufanya nini?
 
VITU VIKUU SITA AMBAVYO MUNGU HAKUVIUMBA.

1. MUNGU
Ukisoma misahafu yote mikuu miwili quran na biblia hakuna ushahidi hata mmoja unaonesha kuwa Mungu kaumba Mungu(namaanisha Mungu kujiumba).

Kubwa zaidi katika misahafu hiyo ambayo imeandikwa kwa matakwa yake MUNGU, inaonesha ukuu wa Mungu, uwezo wake, mamlaka yake, utukufu wake, usafi wake na kila aina ya sifa nzuri na tukufu, lakini hatuoni chanzo chake kikiandikwa humo na hatuoni mwisho wake ukiandikwa humo, zaidi ya vitabu hivyo kusema ufalme wa MUNGU na Nguvu zake hazina mwanzo wala mwisho.

"Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi" Ufunuo 1:8

"Na Mola wako Mlezi anayajua yaliyo ficha vifua vyao, na wanayo yatangaza. Naye ni Mwenyezi Mungu ambaye hapana mungu isipo kuwa Yeye. Sifa zote njema ni zake Yeye, mwanzo na mwisho...." Quran 28:69-70

Kwa aya hizi, na mafundisho mengine ya kinabii kama haya, yanathibitisha bila shaka kuwa ni kweli kuna mambo au vitu ambavyo Mungu hakuviumba na kwasababu hiyo vitu hivyo haviwezi kuitwa viumbe na ingawa viko. Kitu cha kwanza MUNGU, kipo na hakija umbwa.

Wanaosema kuwa MUNGU ameumba kila kitu waje hapa watuambie "MUNGU" kaumbwa na nani? Wakishindwa kututajia basi waishie kusema Mungu kaumba viumbe vyote lakini si vitu vyote.

2. KIZA
Ukisoma hiyo quran 28:69-70 na ukisoma vizuri ufunuo 1:8 utagundua mambo yote na habari zote kabla ya uwepo wa MUNGU hayajulikani na huenda anayajua Mungu mwenyewe, lakini kwetu sisi tunaona mambo hayo kwetu ni KIZA.

Kwa hivyo tunaweza kusema kabla ya Mungu hajaumba chochote alikuwako yeye na Kiza, Kiza ni mwanamke na Mungu ni mwanaume. Kwakuwa kwa kipindi hicho walikuwa wenyewe, na wanajuana wenyewe, jambo jepesi twaweza kusema hivi vitu ni ndugu. Ipo siku inshallah nitakuja kufafanua kwanini nasema Kiza mwanamke na Mungu mwanaume.

"Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. 2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji. 3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. 4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza."
Mwanzo 1:1-4

Katika andika hilo la juu tunajifunza yafuatayo.
Juu ya mambo au vitu unadai havikuumbwa na Mungu kadiri ulivyofafanua na kuweka marejeo ni mawazo, mtazamo na imani inayoweza kuelezwa kama kusoma, kuelewa na kufafanua mambo au vitu nusu nusu au kitoelewa kabisa au kupotoka.

KIZA, ambacho umedai hakikumbwa ni wewe kushindwa kuelewa kwa vipi "nchi" inaweza kutenganishwa na "Kiza". Kama kiza kinasemwa katika biblia au qur'an basi ni baada ya kuumbwa nchi na mbingu. Ni vizuri kuelewa kuwa haiwezekani kusema hiki ni kiza nje ya uwepo wa mbingu na nchi: ulimwengu.

Kwa maana nyingine, kiza ni kabla viumbe. Kabla ya viumbe vingine havijafanyika, nchi na mbingu ndio zilifanyika kwanza. Jinsi hii ya mbingu na nchi kabla ya viumbe ndio huelezwa kama kiza.

Tofauti na viumbe vingine duniani, mtu anachukua daraja la juu kabisa kati yao. " Tumfanya mtu kwa mfano wetu...Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake.

Hii maana yake ni kwamba, mtu amepewa na Mungu "uwezo" wa kuweza kushiriki kazi ya uumbaji ya Mungu.

Mtu anashiriki uumbaji wa Mungu tofauti na Mungu mwenyewe, ambapo yeye anatumia vitu kuumba vitu, huku Mungu aliumba pasipo kutumia vitu. Ukweli huu umebaki hivyo, hata baada ya mtu kutenda "dhambi". Ingawa dhambi imehujeruhi.

" Vita" na "Kifo" haviwezi kufafanuliwa nje ya mtu mwenyewe. Uwepo wake hauchunguziki mahali pengine popote isipokuwa katika "dhambi".

Hivi vyote: vita, njaa, ouvu na kifo, vimepata kuwepo kwa sababu ya mtu mwenyewe kwenda kinyume na sheria ya milele. Tunaweza kuelewa hili kwa kutafiti na kuchunguza mtu kabla ya kutenda dhambi.
 
Tunaambiwa Mungu ni mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.

Sasa imekuwaje Mungu huyo aumbe ulimwengu ambao mabaya, njaa, maafa, ujambazi, majanga ya kiasili etc yanaweza kutokea, wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao hayo hayawezi kutokea?
Kama ni msomaji makini na unaelewa maandiko matakatifu utaona kwamba ulimwengu kabla ya dhambi haukuwa na mabaya: hayo yote uliyoyabainisha hapo juu hayakuwepo kabla ya mtu kutenda dhambi.

Sauti au uelewa kama huu unaoubainisha hapa (mabaya, uovu) mtu ndio anagundua baada ya kutenda dhambi.

Hivyo, Mungu hakuumba dunia yenye mabaya au uovu.

Dunia hii yenye mabaya ni matokeo ya dhambi, ambayo mtu mwenyewe alitenda kwa sababu ya kuelewa na kutumia vibaya uwezo aliopewa na Mungu akitaraji kuwa atakuwa zaidi ya alivyokuwa.

Matokeo ya alichoelewa kama ni "kuwa zaidi" kikawa dhambi. Ndiyo kwa sababu ya dhambi duniani kuna uovu, ubaya na kifo.

Mpaka leo, kwa sababu ya dhambi, mtu ameendelea kupenda mambo fulani fulani akitaraji kwa hayo atafanikiwa na kuwa bora zaidi kuliko wengine katika maisha.

Kama walivyotenda watangulizi wake, mtu huyu huyu amependa mambo fulani, kwayo akaona na kuelewa kuwa atakuwa zaidi pasipo mapendo kwa Mungu.

Mtu akaweka akili na moyo wake katika kupenda mambo hayo fulani fulani, akaacha kumsikiliza Mungu. Akilini mwake akaona ni vema, amefanikiwa na ni bora kuliko wengine.

Ukweli ni kwamba watu wanaopenda mambo fulani fulani, kwayo wakaweka akili, moyo na nguvu zao, wakaacha mapendo ya Mungu: kile Kanisa linafundisha, watu hao na watu wengine wote katika maisha yao kabla au wakati wa kufa hujua ukweli, Mungu. Huona yote waliofanya kama ni mafanikio: uelewa mzuri au mbaya.
 
Katika uzi ambao umenishinda kuchangia ni huu. Maana muandishi wa mada ameandika mambo ya uongo mpaka yamevuka mipaka na amejichanganya sana.
 
Kama ni msomaji makini na unaelewa maandiko matakatifu utaona kwamba ulimwengu kabla ya dhambi haukuwa na mabaya: hayo yote uliyoyabainisha hapo juu hayakuwepo kabla ya mtu kutenda dhambi.

Sauti au uelewa kama huu unaoubainisha hapa (mabaya, uovu) mtu ndio anagundua baada ya kutenda dhambi.

Hivyo, Mungu hakuumba dunia yenye mabaya au uovu.

Dunia hii yenye mabaya ni matokeo ya dhambi, ambayo mtu mwenyewe alitenda kwa sababu ya kuelewa na kutumia vibaya uwezo aliopewa na Mungu akitaraji kuwa atakuwa zaidi ya alivyokuwa.

Matokeo ya alichoelewa kama ni "kuwa zaidi" kikawa dhambi. Ndiyo kwa sababu ya dhambi duniani kuna uovu, ubaya na kifo.

Mpaka leo, kwa sababu ya dhambi, mtu ameendelea kupenda mambo fulani fulani akitaraji kwa hayo atafanikiwa na kuwa bora zaidi kuliko wengine katika maisha.

Kama walivyotenda watangulizi wake, mtu huyu huyu amependa mambo fulani, kwayo akaona na kuelewa kuwa atakuwa zaidi pasipo mapendo kwa Mungu.

Mtu akaweka akili na moyo wake katika kupenda mambo hayo fulani fulani, akaacha kumsikiliza Mungu. Akilini mwake akaona ni vema, amefanikiwa na ni bora kuliko wengine.

Ukweli ni kwamba watu wanaopenda mambo fulani fulani, kwayo wakaweka akili, moyo na nguvu zao, wakaacha mapendo ya Mungu: kile Kanisa linafundisha, watu hao na watu wengine wote katika maisha yao kabla au wakati wa kufa hujua ukweli, Mungu. Huona yote waliofanya kama ni mafanikio: uelewa mzuri au mbaya.
Umeelewa swali langu?
 
Umeelewa swali langu?
Nimeelewa vizuri sana swali lako.

Swali lako kwa maana nyingine ni hivi: kama dhambi ndio chanzo cha mabaya au dunia yenye uwezekano wa mabaya, Mungu mwenye uwezo wote, upendo wote, nguvu zote na mwenye kujua yote alishindwaje kuzuia dhambi isitendeke?

Kufafanua ni kuwa, Mungu baada ya kuumba mbingu na nchi, kisha viumbe vingine alimaliza kazi ya uumbaji kwa kumuumba mtu.

Uumbaji wa mtu ni wa pekee hivi kwamba aliumbwa kwa mfano wa Mungu. Mtu alipata kati ya viumbe vyote vya duniani uwezo au sehemu ya akili ya Mungu, ndio roho.

Swali kwamba, kwanini Mungu aliumba dunia ambamo mabaya yanawezekana kuwepo wakati ana uwezo wa kuumba dunia isio na mabaya, lisifafanuliwe kama linapingana na ukweli kuwa Mungu ana uwezo wote, upendo wote, nguvu zote na anajua yote, lakini lifafanuliwe kama ni kosa dhidi ya "sheria ya milele".

Kinachoeleweka kama kukinzana kwa Mungu kwamba anauwezo wote, upendo wote, nguvu yote na anajua yote, lakini ameumba dunia ambayo mabaya yanatokea au kwa nini ameshindwa kuondoa mabaya duniani. Karne na karne mabaya yameendelea kuwepo duniani, huelezwa kama kosa dhidi ya akili, ukweli na dhamiri safi.

Kosa dhidi ya akili, ukweli na dhamri safi ni kosa dhidi ya sheria ya milele.
 
Ili kitu kiwe kweli, na si uongo, inabidi kikidhi vigezo gani?
Ili kitu kiwe kweli, na si uongo, inabidi kikidhi vigezo gani?

Ili kitu kiwe kweli SIYO LAZIMA kiwe kina-base kwenye empericism, (i.e not necessarily provable by emperical evidence, hata empericism yenyewe haijadai hivyo kwamba everything OUTSIDE ITS DISCIPLINE, should be supported by emperical evidence), except that kinaweza kuwa na ANGALAU mojawapo ya attributes zifuatazo. Aidha kinaweza kuwa:
(i) Illogical
(ii) Logical
(iii) both logical and illogical (e.g. the issue of twin paradox or delusion, where sometimes it happens in reality that the more you chase a thing, the more it deludes from you)

Most important, not also that NOT ALL ILLOGICAL ASSERTIONS are false, and that NOT ALL LOGICAL ASSERTIONS are true!

Ongezea na hiyo pdf attachment nina imani unaweza ukapata kitu kipya kutoka humo.
 

Attachments

Ili kitu kiwe kweli SIYO LAZIMA kiwe kina-base kwenye empericism, (i.e not necessarily provable by emperical evidence, hata empericism yenyewe haijadai hivyo kwamba everything OUTSIDE ITS DISCIPLINE, should be supported by emperical evidence), except that kinaweza kuwa na ANGALAU mojawapo ya attributes zifuatazo. Aidha kinaweza kuwa:
(i) Illogical
(ii) Logical
(iii) both logical and illogical (e.g. the issue of twin paradox or delusion, where sometimes it happens in reality that the more you chase a thing, the more it deludes from you)

Most important, not also that NOT ALL ILLOGICAL ASSERTIONS are false, and that NOT ALL LOGICAL ASSERTIONS are true!

Ongezea na hiyo pdf attachment nina imani unaweza ukapata kitu kipya kutoka humo.
Kwanza kabisa sahihisha spelling. Si "emperical" ni "empirical".

Pili, unajua maana ya empirical evidence ni nini?

Tatu, unajua reason ni nini?

Nne, unajua tofauti ya empirical evidence na reason?

Tano, unaelewa kwamba mimi sijakataa uwepo wa Mungu kwa kutumia empirical evidence, bali kwa reason, na hivyo, criticism yako ya kuhusu empirical evidence hainihusu mimi?

Nakuachia hayo maseali matano kwa sasa, yajibu yote kikamilifu.

Zaidi ya yote. Unaelewa kwamba hujajibu swali langu la msingi?
 
Kwanza kabisa sahihisha spelling. Si "emperical" ni "empirical". Pili, unajua maana ya empirical evidence ni nini? Tatu, unajua reason ni nini? Nne, unajua tofauti ya empirical evidence na reason? Tano, unaelewa kwamba mimi sijakataa uwepo wa Mungu kwa kutumia empirical evidence, bali kwa reason, na hivyo, criticism yako ya kuhusu empirical evidence hainihusu mimi? Nakuachia hayo maseali matano kwa sasa, yajibu yote kikamilifu. Zaidi ya yote. Unaelewa kwamba hujajibu swali langu la msingi?
Kwanza kabisa sahihisha spelling. Si "emperical" ni "empirical". Pili, unajua maana ya empirical evidence ni nini? Tatu, unajua reason ni nini? Nne, unajua tofauti ya empirical evidence na reason? Tano, unaelewa kwamba mimi sijakataa uwepo wa Mungu kwa kutumia empirical evidence, bali kwa reason, na hivyo, criticism yako ya kuhusu empirical evidence hainihusu mimi? Nakuachia hayo maseali matano kwa sasa, yajibu yote kikamilifu. Zaidi ya yote. Unaelewa kwamba hujajibu swali langu la msingi?

Maswali manne uliyouliza, jibu ni kwamba NAJUA. Swali lako la msingi nimeshalijibu, by deductive reasoning. Wewe ulichohitaji ni jibu, siyo njia ya namna ya kujibu swali lako. By the way, umesoma hiyo attachment niliyoweka hapo kwenye post yangu iliyopita, kabla ya hii?
Tathmini yangu ni kwamba post yako inayokuja kama itakuwepo, inaweza kuwa nje kabisa ya mada, unaanza kuondoka kwenye mada, ku-divert kwenye kwenye outliers ambazo si za msingi sana kama kurekebisha spelling wakati hapa hatufanyi mtihani.However, english is my third language
 
Maswali manne uliyouliza, jibu ni kwamba NAJUA. Swali lako la msingi nimeshalijibu, by deductive reasoning. Wewe ulichohitaji ni jibu, siyo njia ya namna ya kujibu swali lako. By the way, umesoma hiyo attachment niliyoweka hapo kwenye post yangu iliyopita, kabla ya hii?
Tathmini yangu ni kwamba post yako inayokuja kama itakuwepo, inaweza kuwa nje kabisa ya mada, unaanza kuondoka kwenye mada, ku-divert kwenye kwenye outliers ambazo si za msingi sana kama kurekebisha spelling wakati hapa hatufanyi mtihani.However, english is my third language
Ushaanza kitabiri nitakachojibu kabla sijajibu.

Una majibu yako unayoniwekea kujibu kabla sijajibu.

Hatuwezi kujadikiana kwa kubadikishana mawazo.

Una bias kubwa sana tayari.
 
Nadhani hoja ya uwepo au kutowepo Mungu,ni hoja yenye changamoto,na ni rahisi zaidi,na pia labda sahihi zaidi ikielezwa kwa kupitia imani zetu,kwani,anayeongelewa ni wa kiroho,kipimo ambacho sisi wenye miili,na kwa kutumia vipimo na vigezo vya kimwili,si rahisi sana kuthibitisha kwa hoja ya kumridhisha sana asiyeamini.

Kama tungezaliwa mara moja tu wote kwa mkupuo na pasiwepo kuzaliwa watoto wengine baada ya hapo,nadhani si ajabu ingekuwa shida sana kumshawishi kwa hoja mtoto anayebisha kuwa,sio mama na baba fulani ndio walimzaa labda akiamini amezuka tu ama kuwepo tu kama hao wazazi wake.Japo hata yeye binafsi,kumbukumbu zake za maisha yake kurudi udogoni zingeenda nyuma na zingeishia na kutokomea kizani tu.

Lakini,bahati mda wote tunapokuwa,twaona watoto wakizaliwa.Na kubwa zaidi,hatimae nasi hushiriki uzazi na kuleta viumbe duniani (kimwili) hatimae hata ubishi dhidi ya wazazi kutuzaa,hauwezi kuwepo tena,labda mengine tu.

Ulimwengu wa kiroho,naamini ni wa vipimo(dimension?) tofauti sana na huu wetu wa nyama tunaoishi.Ili kuweza kudodosa ulimwengu wa kiroho,yahitaji 'vipimo' vya kiroho na ambavyo,katika vionjo na vigezo vya maisha haya ya kimwili,nadhani hatuna,ila maelezo,mafundisho na imani za kidini tu zaidi,japo nadhani wapo waliokwisha hama toka kwenye imani na kuingia kwenye ufahamu na uhakika zaidi kupitia imani zilizokomaa na experience zao na Mungu wao moja kwa moja.

Kutumia vipimo vya kimwili ama vinavyoeleweka katika utashi wa kawaida kibinadamu,mwenye imani tu,hata kama ni ndogo sana ndiye aweza kuongezewa imani kwa maelezo na mafundisho ya kiimani.Ila inaweza kuwa changamoto kwa namna fulani kumwelewesha ama asiyeamini au anayehitaji vigezo na ushahidi dhahiri. Mtu kutoamini mambo ya imani au hata uwepo wa Mungu,nadhani sio lazima kuwa ni ubishi au utata,bali ndio mtazamo wake na kushindwa kwa walio na uwezo kumshawishi kwa hoja zinaoweza kuikuna na kuiamsha imani kwa mantiki za kibinadamu.
 
Ni lazima kilicho complex kiwe na muumba? Au si lazima?
mkuu Kiranga ni lazima kila kitu unachokiona wewe hapa duniani kiwe na muumba,na nadhani hata wewe kuna mahali ulikubaliana na mimi kwamba hata kama kila kitu kina muumba wake not necessarily awe Mungu,nikakwambia lets say nimekubaliana na wewe sasa kwamba okay kila kitu kina muumba wake yes ila sio Mungu,then ni nani muumba wa kila kitu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom