Marekani, nchi inayotamka haitaki vita wakati inaanzisha vita hivyo!

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
1710916936030.png

Hivi karibuni, Marekani ilitangaza kwamba imefanya mashambulio ya anga katika maeneo 85 nchini Iraq na Syria, dhidi ya Kikosi cha Mapinduzi ya Kiislamu cha Iran na makundi ya silaha yenye uhusiano na Kikosi hicho. Mashambulio haya yameharibu zaidi uhusiano kati ya Marekani na Iran, ambao tayari ulikuwa si mzuri, na kuufanya kuwa na utata zaidi.

Nchi zote mbili zimedai kuwa hazina nia ya kuanzisha vita kati yao, na kuna kila sababu ya kuamini kuwa kauli hii ni ya kweli, lakini ukweli ni kwamba, kila upande unazidi kukaribia kuwa na mvutano na hata vita. Nini hasa kinasababisha hali hii?

Baada ya mashambulio ya anga ya Marekani, nchi tatu, ambazo ni Iraq, Iran na Syria, ziliweka wazi hasira yao na kulaani vikali mashambulio hayo. Hapa inapaswa kukumbuka kuwa, kitendo cha Marekani ni ukiukaji wa wazi wa mamlaka halali ya Iraq na Syria, na ni kinyime cha malengo na kanuni za Mkataba wa Umoja wa Mataifa. Marekani imedai kuwa inashambulia vikosi vinavyoungwa mkono na Iran, lakini imesababisha vifo vya raia wa kawaida nchini Iraq na Syria. Kutokuwa na umakini kulikoonyeshwa na Marekani katika kudhihirisha umwamba wake kunahitaji jamii ya kimataifa kutafuta njia za kuudhibiti.

China daima imekuwa na msimamo wa kumaliza tofauti kwa njia za amani na inapinga matumizi ama vitisho vya kimabavu katika uhusiano wa kimataifa. China imependekeza pande zote zinazohusika kufuata kwa ufanisi malengo na kanuni za Mkataba wa Umoja wa Mataifa na kanuni za kimsingi za uhusiano wa kimataifa.

Pia imesisitiza kuwa, mamlaka halali, uhuri na ukamilifu wa ardhi ya Iraq na Syria vinapaswa kuheshimiwa na kulindwa. Hii inaonyesha wazi kuwa, China inapinga na kulaani vitendo kama hivyo vya Marekani.

Katika miongo michache iliyopita, Marekani na Iran zimekuwa katika mvutano ambao umekuwa sehemu kubwa ya mambo yanayoendelea katika Mashariki ya Kati. Inapaswa kufahamu kuwa, Marekani na Iran zote zina uzoefu mkubwa wa siasa za kijiografia, lakini hali ilivyo sasa inaelekea moja kwa moja kwenye mgogoro wa wazi, na kama hii ikiruhusiwa kutokea, hali katika kanda hiyo itakuwa mbaya zaidi.

Kama hilo likitokea, si Marekani wala Iran itakayokuwa na uwezo wa kudhibiti hali hiyo, na hakuna upande utakaoweza kuelekeza mwelekeo kama unavyotaka. Zaidi, ukubwa wa athari ya hali hiyo kama ikitokea, hautakuwa kati ya Iran na Marekani pekee, kwa sababu mapigano yoyote katika kanda ya Mashariki ya Kati yana uwezekano mkubwa wa kuenea katika sehemu nyingine.

Marekani imeweka vikwazo vya pande zote dhidi ya Iran kwa miaka mingi. Sasa, inafanya mashambulio ya moja kwa moja dhidi ya kile inachodai kuwa ni ‘makundi yanayoungwa mkono na Iran,’ hatua ambayo, kwa kiasi fulani, pia inaashiria kutofanikiwa kwa vikwazo hivyo. Matokeo ya matumizi ya jeshi yanazidi hata hivyo vikwazo, na Marekani huenda tayari imegundua hili.

Badala ya kupunguza utegemezi wa vikwazo na matumizi ya jeshi, Marekani huenda imeongeza utegemezi wa hatua hizo. Tunalazimika kusema kwamba, mvutano wa kimkakati unaiokabili Marekani umekuwa ni suala kubwa la kikanda na dunia!
 
Back
Top Bottom