Ngoja niweke mkasa wangu mwingine ulitokea 2004, Jamaa zangu walitoka mgodini wana hela ya maana wamekuja na mshikaji wao watupambanishe kunywa pombe wanajua mimi kichwa ngumu kwenye bia. Nikawapa masharti kuwa nakunywa bia na si pombe kali. Wakaleta kreti moja ya Tusker na jamaa akapewa yakwake hiyo ni saa mbili asubuhi tumeshakula ugali kwa supu ya samaki. Kufika saa saba nimemaliza kreti jamaa kachemsha. Nikaaga nikaenda kulala, nakuja kushtuka kesho yake mchana majirani wanabomoa mlango wakijua nimekufa. Walichungulia dirishani wanaona mtu kalala chini wakajua nishaenda kwa Sir God. Niliugua siku 3 sijiwezi kabisa.