Visa gani pombe ilikufanyia hutasahau?

Visa gani pombe ilikufanyia hutasahau?

Usipokunywa pombe hiyo digestion hifanyi kazi vizuri? Nini madhara ya kutokunywa?
Kutokunywa pombe hakuna madhara, ila kiwango fulani kina rahisisha kazi zingine mwilini kama hiyo moja niliyosema. Kwa wale ambao walishakunywa alafu wakaacha, mpangilio wa digestive system huvurugika na hata kiwango cha kuka hupungua
 
Visa vyangu ni lukuki, miaka ya 2000 nilisafiri toka mkoa niliokuwepo nikaenda Mkoa wa mara (Musoma mjini). Rafiki yangu wa karibu sana alikuwa anafunga ndoa, sherehe ikafanyika pale Musoma hotel. Nilikunywa pombe nazinduka nimelala ufukweni mwa ziwa victoria tena asubuhi kabisa vitu vyangu vyote ninavyo. Usiku baada ya sherehe wamenitafuta wakashindwa kujua nilikokwenda. Nikarudi nilikofikia bila kuwasimulia kilichonikuta
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Pombe ina gharama!
Kununua pombe mpaka ulewe inahitaji pesa ndefu!
Labda uwe mnywa pombe chafu Kama mabanana na gongo ambayo yanazeesha haraka

Kutibu hangover ni gharama masupu,energy drinks,matango nk na ikikuzidi hapo utajisalimisha zahanati ule dripu za maji na glucose

Hapo bado utashindwa kufanya kazi uingize kipato!
Utadhahaurika halafu Amna kitu Cha faida ulichopata

Najutaga kuijua pombe nilivyoianza nikiwa na miaka 12 kwa mbege huko Moshi

Ila now mi ndio naimiliki
 
Baada ya kuutwika kwenye sherehe ya kazini nilimtongoza mama mmoja mwenye cheo chake, nae akawa anacheka tu. Mimi ndio nazidi kumpa maneno mbele ya watu. Party iliisha kila mtu akaenda zake. Jumaatatu yule mama akaniita na kuniambia Ni mwambie yale maneno niliyo muambia siku ya party halafu alikua serious.
Ikawaje
 
Nilifakamia nyagi pale taifa usiku wa fiesta kufikia kwenye saa nane sielewi ilikuaje nashtuka saa kumi na mbili kasoro hivi nimelala katikati na wana wengine kibao watoto wa kike ndo usiseme, kuna sister flan nlkua naye hata sikufanikiwa kujua alisepa saa ngapi ila kuna dogo tulikutana pale tulikua wote before alikua na mtu wake nikampigia simu tukaonana nikazuga nilikua naruka pale kati....cha kushukuru ulinzi ulikua imara ile siku
 
Mkuu heko kwako[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]

Makofi jamani eeh, umedadavua kiutamu mpaka nimerudia mara mbili mbili kusoma

Ila kama mambo yenyewe ni hayo, sitaki na wala sitamani ulabu tena

Kwaheri gambe[emoji119][emoji119][emoji2772]
Thanks for your appreciations. Kuna hatua flani ukifikia pombe haiachiki bila maelekezo kutoka kwa daktari baada ya kuwa na health complications.

Na kama hujafikia huko si mbaya ukinywa kwaajili ya kuchangamsha mwili (Uwe na personal limits zako mwenyewe).

Ila wengi wanasema wanaacha lakini naadae wanajikuta wamepumzika kwa muda tu hahaha😄😄 so I wish you all the best on your quitting process.
 
Kuna siku nilimkamata demu mmoja mkali sana wa Chuo fulani, Huyo demu alinisumbuwa sn siku nyingi, Siku moja nikamchombeza tukutane sehemu,,,nimpe ofer ya nyama choma, basi tukatafuta sehemu tulivu safi kabisa,,,,,yule mrembo akaagiza henken na mm sikuagiza chochote zaidi ya maji.

Basi yule mrembo akaanza kuponda,,kwamba anakuwa comfortable sana kama akiwa na boyfriend mnywaji kama yeye. Duu!! Mimi sijawahi kunywa pombe hata siku moja. Ikabidi kwa kujikaza na mm niagize henkeni nikaanza kupiga moja moja.

Aisee nilijikaza sn kunywa kama chupa mbili tu,,nikaanza kuona watu wanatembea kichwa chini miguu juu, Basi nikalazimisha tuingie ndani lodge chumbani tuendelee kunywa tukiwa chumbani.

Maana ile sehemu ilikuwa na lodge ,,,basi sikumbuki vzr ilikuwaje ,,ila nakumbuka nilizidiwa na pombe na hakuna kilichofanyika siku ile,,
Nililala fofofo bila kumgusa yule demu,,kushtuka sauti ya muhudumu wa lodge ikituamsha kuchek out..na ni saa nne asubuhi..
Duu...tuliposhtuka nililazimisha kupiga japo tako 3 kwa yule demu,,nipate kimoja cha Jogoo ikashindikana.,,maana mtoto na yeye pia kachelewa Chuo.

Duuh nilimlaani sana aliyegunduwa pombe.

Mtoto yule nimemkosa hadi Leo.

Pombe nuksi sana,,,naichukia hadi leo.
Haha yaani kuzima kwako ndio unailaumu pombe mkuu? Kwani ungemwambia kwamba you'd never tasted alcohol before angekubania? Ugwadu wako ndio uliokupelekea kukosa utamu wa vyote yaani raha ya pombe na raha ile😂😂😂
 
Haha yaani kuzima kwako ndio unailaumu pombe mkuu? Kwani ungemwambia kwamba you'd never tasted alcohol before angekubania? Ugwadu wako ndio uliokupelekea kukosa utamu wa vyote yaani raha ya pombe na raha ile[emoji23][emoji23][emoji23]
Nilitaka nionekane ni really gentleman kwa mrembo.
Maana anapenda mwanaume mnywaji kama yeye.
 
Nilitaka nionekane ni really gentleman kwa mrembo.
Maana anapenda mwanaume mnywaji kama yeye.
Haha bhasi pombe haina makosa mkuu, ni wewe tu ulishindwa kuibalance na hali yako ya ugeni kwenye pombe. Chakushangaza umezima kwa Heineken mbili?!😂😂
 
Siku moja tulienda goa, nlikuwa bangarole chuoni. Basi bwana mdada mmoja kutoka syshelly alikuwa nazo balaa. Tuko kwenye boat inatuzungusha baharini.

Goa ni mji wa kitalii kama huku kwetu bagamoyo. Basi bwana kuna kitu inaitwa kingfisher ina alcohol8.6 kama sikosei. Akatoa ofaer kwa wanachuo wote katika darasa letu tulikuwa kama 20 hivi wanywe tani yao mpaka boati ikirudi nchikavu. Kila mzunguko ulikuwa 15 minutes.

Alituxhukulia poa, mi mbongo nikasema hapa ndo pa kuchukulia sifa. Acha nipige tarumbeta, walikuwa wanacheza mziki mi nagida tu. Mpaka dk 15 nishatia damage kama kopo 5 hivi. Halafu ikumbukwe tulitembea usiku kucha kutoka bangarole hadi goa.

Ni kama dar mwanza, na mabasi huanza safari saa 2 usiku. Tulikuwa na beer zinafleva ya soda za fanta orange na fanta black current tulizinywa sana.hadi tunafika nlkuwa hoi. Mpaka boti inafika nchikavu nlikuwa hoi walifanya kunibeba hata kusimama ni kwa shida.

Nlirudisha chenj ndo hali ikawa ovyo kabisa. Utalio wangu ukaharibikia hapo. Ikabidi nikatalie kwenye buss. Naambatanisha picha nliyopiga mwenyewe nikiwa ndani ya boati

IMG_20160902_113452.jpg
 
Mimi wala pombe sina memory nayo maishani ila UGORO jamani,sijui mimi nani aligundua UGORO.

nili test ONCE ila kumbukumbuku ninayo mpaka na kesho kutwa,watumiaji Ugoro heshima yenu wakuu.
Ulikufanyaje mkuu?

Mimi nina historia na Kubeli miaka zaidi ya 16 iliyopita. Nikikumbuka tumbo lilivyoninyonga jioni ile baada ya kupewa na room mate wangu na kuitafuna na kumeza mate 😰😰😭
Nilivyotapika na njaa iliyoniuma baada ya hapo alafu tuko shule boarding wakati wa prepo chakula tulishakula hapo hakuna kitu kingine mpaka asubuhi warm up (kahawa kavu) sitaki kukumbuka😂😂

Kuanzia tukio hilo sijui kubeli yenyewe, tambul wala ugoro haujawahi kuingia kwenye hiki kinywa tena
 
Mimi wala pombe sina memory nayo maishani ila UGORO jamani,sijui mimi nani aligundua UGORO.

nili test ONCE ila kumbukumbuku ninayo mpaka na kesho kutwa,watumiaji Ugoro heshima yenu wakuu.
Ulikufanyaje mkuu?

Mimi nina historia na Kubeli nikikumbuka tumbo lilivyoninyonga jioni ile baada ya kupewa na kuitafuna na kumeza mate 😰😰😭

Nilivyotapika na njaa iliyoniuma baada ya hapo alafu tuko shule boarding wakati wa prepo chakula tulishakula hapo hakuna kitu kingine mpaka asubuhi warm up (kahawa kavu) sitaki kukumbuka😂😂

Kuanzia tukio hilo sijui kubeli yenyewe, tambul wala ugoro haujawahi kuingia kwenye hiki kinywa tena
 
Sita sahau siku hiyo nimekunywa pombe badala ya kwenda Lumumba aisee nikaelekea pale ufipa tena nakumbuka nilimkuta mwenyekiti wao na makamu wake.

Ila kwa bahati nzuri sijui mbaya nao walikuwa washazitwika tani yao.
 
Back
Top Bottom