Wamekujibu mengi mpaka nimeshindwa kuyasoma yote. Kama kuna aliyeandika haya yangu, basi yapotezee.
Back to the point;
Ni sheria isiyo badilika. Mama mkwe kamwe hakosei wala hawezi kuambiwa ati kakosea. Ikae hivyo na uikubali, ndipo wewe utajulikana kuwa unamheshimu.
Mawifi; Usiwanenee mabaya yeyote mbele yao au mama yao. Utazusha zogo litakushinda kumaliza.
Tatu na mwisho;
Nyumba yako itakuwa imara kama mumeo akiweka paamba masikioni na kuwaambia wote, mamake na dadaze kuwa yeye ndiye kaoa wala si wao waliooa.
Awaambie kuwa, kampenda mchafu wake, mvivu wake na timbwatimbwa lake. Full Stop. Hahitaji kusaidiwa kukupenda. Akisimama na hilo, umepona. Akiungana nao, hiyo nyumba hukai. Hata kwa ndumba