Vipaji maalum si lolote, si chochote

Vipaji maalum si lolote, si chochote

fuatilia tamasha la young scientist lililofanyika dsm mshindi alikuwa nani na alitoka shule gani kwa ku present nini....Nyani ulisoma school gani ? Tatizo mnafuatilia matokeo ya Necta tu.....matamasha ya Malihai na uhifadhi wa mazingira watoto wa.afanya makubwa kule.

Lol@ vipaji maalum vya NECTA.

Mi nilisoma Kinondoni Muslim
 
mbona chuo wamedisco,sup kibao,poor performance,poor presentaion.G PA 1 .9 ad 2.4.me nimetoka shule ya jesh ila mwanzo mwisho nakimbiza G.PA,4.1.kusoma kuamua 2 hakuna kipaji wala nini we ukiamua kukomaa mbona unawaficha walioenda mzumbe,tabora,kibaha kipind hicho me nilifel la 7.me nikaenda seminary nashangaaa vipagi wapo mitani nimewaacha,nimeanini bongo elimu kukomaaa 2 hakuna chochote.aliyekuwa mbulula shule ya msingi amepiga 1.10 kipindi hicho ye huwa wa mwisho kwenye mitihani.
 
Lol@ vipaji maalum vya NECTA.

Mi nilisoma Kinondoni Muslim

Hongera mkuu hata kino pia naamini wanachukua majembe, wakati nipo chuga kuna jamaa yangu alikuwa anapga shule hapo jamaa kitaa tulimhanya sijui maeneo hayo hali ilikuwaje bt kiujumla naikubali sana hiyo shule, na vipi suala imani hapo mkuu?
 
Hapa hakuna cha kipaji maalum wala nini....kwani mtu akifaulu kwa ndondokela au akiiba mitihani akafaulu vizuri hicho kitakuwa ni "kipaji maalum"? Kipaji maalum cha kuiba mitihani au nini? Hii dhana ya "ukipaji maalum" inapaswa kutazamwa upya...haina mashiko tena siku hizi. Tafakari, chukua hatua!
 
Hapa hakuna cha kipaji maalum wala nini....kwani mtu akifaulu kwa ndondokela au akiiba mitihani akafaulu vizuri hicho kitakuwa ni "kipaji maalum"? Kipaji maalum cha kuiba mitihani au nini? Hii dhana ya "ukipaji maalum" inapaswa kutazamwa upya...haina mashiko tena siku hizi. Tafakari, chukua hatua!

wivu wa ki....
 
kamwe ntasimamia msimamo wangu!!! TANZANIA HAKUNA SHULE YA KIPAJI AU VIPAJI MAALUM!!!!! fulusutopu
 
Tanzania ina Shule sita zinazojulikana kama Vipaji Maalum. Zipo nne za wavulana na mbili za wasichana. Shule hizo ni Mzumbe,Tabora Boys,Ilboru,na Kibaha(kwa wavulana). Kwa wasichana ni Kilakala na Msalato.

Katika matokeo ya Kidato cha Nne ya 2012 yaliyotangazwa leo,Shule hizo za vipaji maalum zimeboronga. Hakuna hata moja iliyo kwenye kumi bora. Zimeshindwa kujidhihirishia utofauti wao. Vipaji maalum sasa hakuna lolote,hakuna chochote.

Nafasi zao ni kama ifuatavyo: Mzumbe(17),Kibaha(18),Ilboru(31),Tabora Boys(44),Msalato(59) na Kilakala(63).

NOTE: Shule mpya ya Marian Boys ambayo ndio kwanza imeanza kutoa wahitimu wa kidato cha nne imeshika nafasi ya pili kitaifa. Hii ni Shule pacha ya Marian Girls (zote ziko Bagamoyo).Marian Girls imekamata nafasi ya nne nyuma ya Feza Boys(3) na vinara St. Francis Girls ya Mbeya.

Kwaheri vipaji maalum!



Kwa sasa tunaweza kusema kuwa hatuna vizazi vijavyo kwani ukiangalia kwa makini wanafunzi wengi siku hizi hawajali shule kama zamani maana kila mmoja anataka kumiliki gari haraka hata kabla ya kumaliza shule ama kufanya kazi, hivyo wengi hujikita kwenye haya matamasha ya kijinga ya Bongo star search ama epic search ili ajishindie gari na hatimaye kupata mkataba wa kurekodi nyimbo za fleva na kuvaa makata ku.ndu kujifananisha na Lil Wayne wa Marekani ama msanii wa Kimarekani. Kwa kifupi, naweza sema Bongo fleva na Clouds media zinawaharibu sana wanafunz wetu. Hii pia ni furaha ya viongozi wetu kwani wanafunzi wengi wakijikita kwenye gemu la muziki ni unafuu kwao kwani wao wataweza kuiba na kusomesha watoto wao nje ya nchi huku wanafunzi wakiwa bize kuandika mistari ya fleva isiyo na maana.
 
Bottom line ni kwamba hayo mambo ya vipaji maalum ni hogwash!

Hizo shule si za vipaji maalum. At least mimi sijaona umaalum wala kipaji chochote kwa wanafunzi waliosoma kwenye hizo shule.

Kama wapo kweli na wanacho cha kuonyesha kuthibitisha umaalum wa vipaji vyao basi naomba mwenye hayo majina na accomplishments zao anipatie hapa.
Wanachukua cream ya taifa one ya 14 na AAA
 
tabora girls pia ni special school nahisi mtoa mada umeisahau. Shule zile ni vipaji sababu zinachukua best students, ila shida iko pale pe kwa shule zetu za serikali, walimu na zana za kufundishia ni duni. Mie nilisoma moja ya hizo shule, form V yote hatukuwa na mwalimu wa chemistry sasa hapo huwez kufananisha na hizi shule za private ambazo walimu wamakuwa utilized at maximum level. Ila kama wanafunzi wa hizo shule wakapewa magement ya kama marian schools nahisi wangepitiliza kufaulu sababu wako vizur sana
 
Tanzania ina Shule sita zinazojulikana kama Vipaji Maalum. Zipo nne za wavulana na mbili za wasichana. Shule hizo ni Mzumbe,Tabora Boys,Ilboru,na Kibaha(kwa wavulana). Kwa wasichana ni Kilakala na Msalato.

Katika matokeo ya Kidato cha Nne ya 2012 yaliyotangazwa leo,Shule hizo za vipaji maalum zimeboronga. Hakuna hata moja iliyo kwenye kumi bora. Zimeshindwa kujidhihirishia utofauti wao. Vipaji maalum sasa hakuna lolote,hakuna chochote.

Nafasi zao ni kama ifuatavyo: Mzumbe(17),Kibaha(18),Ilboru(31),Tabora Boys(44),Msalato(59) na Kilakala(63).

NOTE: Shule mpya ya Marian Boys ambayo ndio kwanza imeanza kutoa wahitimu wa kidato cha nne imeshika nafasi ya pili kitaifa. Hii ni Shule pacha ya Marian Girls (zote ziko Bagamoyo).Marian Girls imekamata nafasi ya nne nyuma ya Feza Boys(3) na vinara St. Francis Girls ya Mbeya

Kwaheri vipaji maalum!

.........kwanza kwa sasa hakuna hiko kinaitwa kipaji maalumu,hilo kwanza ulitambue,pili....hizi shule zilizokuwa zinaongoza kipindi hiko sasa hivi hakuna mkazo wa elimu kutokana na sababu mbalimbali zilizoko katika tafiti zilizofanywa
 
Nchi kukosa kuzipalilia shule maalum za vijana wake wenye vipaji maalum ni muendelezo wa MAJANGA. Na ukiona wananchi wa nchi hiyo wanachekelea hali hiyo kama mazuzu, basi ndio kabsaaaaa "majanga+"
Lakini tusikate tamaa, tuendelee kukesha tukiomba.
 
Mpaka leo sijapata jibu la swali langu!

Vipaji maalum maana yake nini na ni vigezo gani ambavyo waliamua kutumia kuamua huyu ana kipaji maalum na huyu hana?

Kwa sababu kupata alama za juu tu kwenye masomo haimaanishi kwamba una kipaji maalum.

Hao wanafunzi waliosoma kwenye hizo shule kuna hata mmoja aliyevumbua chochote cha kuboresha maisha ya mwanadamu?

Halafu, hao wanafunzi waliosoma kwenye hizo shule za vipaji maalum mbona tunawakimbiza sana huku uraiani.

Vipaji maalum maana yake nini?

mkuu, mimi naomba tu kufahamu aliyeleta hilo wazo la vipaji maalum ni nani hasa na lengo lake lilikuwa ni nini?
 
Mkuu kuna vipaji maalum serikali na vipaji maalum binafsi. Na kutokana na ufundishaji mzuri wa vipaji maalum binafsi wanafunzi wengi "cream" wanaishia huko kwa akina St. Francis, Marian, etc. Wale ambao wazazi wao hawana uwezo wa kuwalipia hizo karo kubwa ndo wanaenda huko Mzumbe, Ilboru na kwingineko. Kwahiyo na matokeo lazima yawe mazuri zaidi kwa vipaji maalum binafsi kwasababu pia huwa wanawachuja kila muhula.

umenena vema maisha ya marian na tbr boys hayafanani kabisa
 
Kwa nini unakimbilia kunyoosha kidole cha wivu badala ya kujibu swali lililoulizwa?

Vipaji maalum maana yake nini na ni vigezo gani wanatumia kuamua huyu mwanafunzi ana kipaji maalum na huyu hana?
mfumo wa elimu haivitambui vipaji vya uvumbuzi kwenye ngazi ya chini hivyo wanatumia kigezo cha ufaulu kama kipaji hebu niambie ni mtoto gani tanzania kavumbua kitu at std7
 
Back
Top Bottom