Viongozi wa kisiasa msitake sifa kwenye mambo ya Usalama kwa misafara ya viongozi!!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,320
33,940
Kuratibu na kulinda misafara ya viongozi si jambo jepesi kama watu wengi wanavyodhani. Kuwa na mazingira wezeshi ya kulinda misafara hiyo pia si jambo la Polimi lai!!

Naona watu wengi pamoja na wanasiasa wenyewe wanachanganya kati ya kuwa na misafara mirefu na muda unaotumika kupitisha misafara kutokana na uhitaji wa huyo aliyemo kwenye msafara husika.

Leo mnataka misafara ilindwe kisiasa kuwafurahisha wanaosubirishwa bila ya kuangalia chanzo cha kusubirishwa huko. Kwa mfano misafara ya Dar toka Ikulu mpaka uwanja ndege hutumia kati ya Dakika 7 mpaka 10 kwa muda wa kawaida ama dakika 10 hadi 12 kama kuna dosari za mwendo na mpangiilio wa magari.

Lakini kama msafara huo huo toka Uwanja wa ndege kwenda Ikulu ukiwa na Mgeni unaweza kuchukua mpaka dakika 30. Sasa waliomo kwenye msafara siyo waliomo kwenye vituo (Point) vya kuongozea magari yapitayo msafara unapopita. Na Mwelekeo wa gari haudhibitiwi toka kwenye Pointi bali kule linakoelekea.

Kwa mfano kwenye Point tata ya Gerezani, wale wanaotaka Magari yazuiuwe dakika 10 kabla ya msafara kupita wanaelewa wanachokisema? Kwa mfano Magari yaruhusiwe kuelekea njia ya Kurasini, na ya kurasini yaruhusiwe kuelekea Posta. Nani atakuwa anasimamia mwendo kasi wa magari hayo??

Maana watu wanadhani kwamba ni kitu rahisi kuwafanya madereva wote wa Magari wafikirie kwa kufanana kwamba wanatakiwa waharakishe ili msafara upite. Matokeo yake kukiwa na kukwama basi lawama tena watatupiwa watu wa Usalama barabarani.

Wanasiasa wanaowalaumu Polisi leo ndiyo hao hao huwa wanawalaumu misafara inapoingiliwa. Na mikoani ndiyo Karipio huwa kubwa sana na Ma -RPC huwa kwenye changamoto kubwa sana kwenye kusimamia misafara hiyo.
 
Wasiojua tu ndio wanapiga kelele nilishangaa hata kauli ya Mpango!!

Kumbe mpango pamoja na kuwa Makamu bado kuna vitu havijui!!

Usalama wa rais, makamu na waziri mkuu na mawaziri na wabunge upo katika miongozo kabisa kisheria!!

Imagine mbunge analindwa na watu wawili mpaka watatu wasioonekana je itakuwaje kwa Rais au makamu?

Maana wanajua hasara itakayotokea ya kwenda kwenye uchaguzi kama watafanya mzaha akafa kwa uzembe!!

Angalia hasara taifa lilioingia baada ya kifo cha Magufuli!!

Tuache siasa kwenye kila jambo!!
 
Allen umepoa sana ckuiz,

Badala ya kuanzisha thread kuwasha moto Bunge lijadili Ripoti ya CAG Kwa dharura, unakuja na hoja nyepesi zilizojaa propaganda.

Yaani Leo unaanzisha HOJA kuwajibia polisi?

Mmepatwa na nini hapo ufipa?
Bungeni si mmejijaza wenyewe!! Waambieni UVCCM na chawa wenu wawahimize wabunge wenu wajadili ripoti ya CAG waache Polimi Lai!!
 
Yaani wananchi wanaichukia hiyo misafara!
Wanatamani hata iwe inatozwa Kodi!!
Hoja si misafara ila jinsi inavyoshauriwa iendeshwe. Kwa kweli watu wanaojua yaliomo kwenye mambo ya Misafara, hizo hoja za dakika kumi hawawezi kuzikubali!!
 
Hoja si misafara ila jinsi inavyoshauriwa iendeshwe. Kwa kweli watu wanaojua yaliomo kwenye mambo ya Misafara, hizo hoja za dakika kumi hawawezi kuzikubali!!
Inavyoendeshwa ni medani...
Wananchi wanaumizwa na utitiri wa magari ya kifahari na gharama kubwa kwenye hiyo misafara!

Usikwepeshe tatizo lilipo!
 
Inavyoendeshwa ni medani...
Wananchi wanaumizwa na utitiri wa magari ya kifahari na gharama kubwa kwenye hiyo misafara!

Usikwepeshe tatizo lilipo!
Wewe ndiyo unataka kujadili mada ambayo si hoja ya bandiko langu. Msafara kuwa na Magari ya kifahari na watu kusimamishwa muda mrefu ili msafara upite ni mambo mawili yasiyofanana kabisa. Misafaraa mingi inatumia muda mwingi kutokana na tabia isiyotabirika ya wanasiasa wenyewe!1

Umesema kwamba kuendesha misafara ni medani, na kama ni medani basi bila ya shaka kuna kanuni ya kuiiongoza inayotokana na tafiti zilizowahi kufanyika. Na ndiyo maana nimetoa mfano wa muda unaotumika kupitisha msafara toka Ikulu ya Magogoni mpaka uwanja wa ndege Kipawa.
 
Kuratibu na kulinda misafara ya viongozi si jambo jepesi kama watu wengi wanavyodhani. Kuwa na mazingira wezeshi ya kulinda misafara hiyo pia si jambo la Polimi lai!!

Naona watu wengi pamoja na wanasiasa wenyewe wanachanganya kati ya kuwa na misafara mirefu na muda unaotumika kupitisha misafara kutokana na uhitaji wa huyo aliyemo kwenye msafara husika.

Leo mnataka misafara ilindwe kisiasa kuwafurahisha wanaosubirishwa bila ya kuangalia chanzo cha kusubirishwa huko. Kwa mfano misafara ya Dar toka Ikulu mpaka uwanja ndege hutumia kati ya Dakika 7 mpaka 10 kwa muda wa kawaida ama dakika 10 hadi 12 kama kuna dosari za mwendo na mpangiilio wa magari.

Lakini kama msafara huo huo toka Uwanja wa ndege kwenda Ikulu ukiwa na Mgeni unaweza kuchukua mpaka dakika 30. Sasa waliomo kwenye msafara siyo waliomo kwenye vituo (Point) vya kuongozea magari yapitayo msafara unapopita. Na Mwelekeo wa gari haudhibitiwi toka kwenye Pointi bali kule linakoelekea.

Kwa mfano kwenye Point tata ya Gerezani, wale wanaotaka Magari yazuiuwe dakika 10 kabla ya msafara kupita wanaelewa wanachokisema? Kwa mfano Magari yaruhusiwe kuelekea njia ya Kurasini, na ya kurasini yaruhusiwe kuelekea Posta. Nani atakuwa anasimamia mwendo kasi wa magari hayo??

Maana watu wanadhani kwamba ni kitu rahisi kuwafanya madereva wote wa Magari wafikirie kwa kufanana kwamba wanatakiwa waharakishe ili msafara upite. Matokeo yake kukiwa na kukwama basi lawama tena watatupiwa watu wa Usalama barabarani.

Wanasiasa wanaowalaumu Polisi leo ndiyo hao hao huwa wanawalaumu misafara inapoingiliwa. Na mikoani ndiyo Karipio huwa kubwa sana na Ma -RPC huwa kwenye changamoto kubwa sana kwenye kusimamia misafara hiyo.
Huo ni utumbo wa kujitakia kazi zisizo na tija.
Mwalimu miaka hiyo alikuwa na msafara wa magari yasiyozidi sita.
Taratibu wapambe wa kiusalama wanaoji overate wanaingiza vitu ambavyo si nadharia tu,bali kujipatia kazi ambazo hazina tija.

Watanzania ni ni watu peaceful na hayo wanaojidai wana usalama yanaweza kutokea, hayajawahi kutokea.

Mwalimu alikuwa anatembelea hadi ile Rolls Royce akipokea wageni, na niliona hilo live akimpokea Nelson Mandela, na nilikuwa maeneo ya Posta ya zamani.

Mtoa mada nikuulize,kwa fujo mnazoonyesha na kusumbua wananchi, how many assasination attempts mmeweza kuzuia?

Wanausalama wanasumbua wananchi, na naungana na Mh Phillip Mpango kwa hili.
 
Ungetolea mfano wa Dodoma kwa sababu makao makuu ya nchi yako huko. Halafu pia nafikiri wanawweza kuwa wanatumia Helicopter.
Kuratibu na kulinda misafara ya viongozi si jambo jepesi kama watu wengi wanavyodhani. Kuwa na mazingira wezeshi ya kulinda misafara hiyo pia si jambo la Polimi lai!!

Naona watu wengi pamoja na wanasiasa wenyewe wanachanganya kati ya kuwa na misafara mirefu na muda unaotumika kupitisha misafara kutokana na uhitaji wa huyo aliyemo kwenye msafara husika.

Leo mnataka misafara ilindwe kisiasa kuwafurahisha wanaosubirishwa bila ya kuangalia chanzo cha kusubirishwa huko. Kwa mfano misafara ya Dar toka Ikulu mpaka uwanja ndege hutumia kati ya Dakika 7 mpaka 10 kwa muda wa kawaida ama dakika 10 hadi 12 kama kuna dosari za mwendo na mpangiilio wa magari.

Lakini kama msafara huo huo toka Uwanja wa ndege kwenda Ikulu ukiwa na Mgeni unaweza kuchukua mpaka dakika 30. Sasa waliomo kwenye msafara siyo waliomo kwenye vituo (Point) vya kuongozea magari yapitayo msafara unapopita. Na Mwelekeo wa gari haudhibitiwi toka kwenye Pointi bali kule linakoelekea.

Kwa mfano kwenye Point tata ya Gerezani, wale wanaotaka Magari yazuiuwe dakika 10 kabla ya msafara kupita wanaelewa wanachokisema? Kwa mfano Magari yaruhusiwe kuelekea njia ya Kurasini, na ya kurasini yaruhusiwe kuelekea Posta. Nani atakuwa anasimamia mwendo kasi wa magari hayo??

Maana watu wanadhani kwamba ni kitu rahisi kuwafanya madereva wote wa Magari wafikirie kwa kufanana kwamba wanatakiwa waharakishe ili msafara upite. Matokeo yake kukiwa na kukwama basi lawama tena watatupiwa watu wa Usalama barabarani.

Wanasiasa wanaowalaumu Polisi leo ndiyo hao hao huwa wanawalaumu misafara inapoingiliwa. Na mikoani ndiyo Karipio huwa kubwa sana na Ma -RPC huwa kwenye changamoto kubwa sana kwenye kusimamia misafara hiyo.
 
4 hours is too much!
Kwanza ni muda usio na sababu. Lakini nikwambie kitu. Msafara huanza pale mwenye msafara anapoanza Msafara.

Nikupe "Scenario" moja ya jinsi misafara inavyoanza. Anayesafirishwa huwa anaelekezwa kutoa ishara ya kufikia mwisho wa ama hotuba au ukaaji wake sehemu anayotakiwa kutoka kwenda kwingine. Hiyo Ishara ndiyo husaidia wapanga msafara kuweka mazingira ya Msafara kuanza.

Ndiyo maana Kiongozi wa kisiasa anapohutubia anapokaribia mwisho wa hutoba yake ni lazima aoneshe kwamba anafikia mwisho wa hotuba kwa kutoa aina fulani ya maneno. Sasa wakati waongoza msafara wanatafsiri Kiongozi kafikia mwisho wa hotuba, kumbe yeye ghafla anaona aanzishe hadhiti nyingine ya kutamatisha hotuba yake.

Wakati Kiongozi huyo anachomekea mambo mapya mwishoni mwa hotuba yake, huku waongoza msafara tayari wanakuwa wametoa ishara na maelekezo kwa watu wao kuwa msafara unakaribia kuanza hivyo wazuie magari. hiyo nimetoa mfano wa mijini ambako msafara huwa hautumii zaidi ya dakika 30 kufika unakoelekea.

Lakini hebu fikiria barabara ambayo kiongozi anatoka mkoa mmoja kwenda mwingine yenye upana wa mita 3.25 na kwa uhimilivu wa mwendokasi wa Magari ya misafara ni lazima magari yapite katikati ya Barabara, sasa hapo Polisi wanawezaje kudhibiti usalama toka kwenye point zao mpaka msafara ulipo na unakoelekea??

Kwa mfano Point ya Polisi iko Kilomita 60 msafara unapotoka ama kuelekea, akiruhusu magari, hapo katikati nani atakayekuwa anayadhibiti hayo Magari??
 
Wasiojua tu ndio wanapiga kelele nilishangaa hata kauli ya Mpango!!

Kumbe mpango pamoja na kuwa Makamu bado kuna vitu havijui!!

Usalama wa rais, makamu na waziri mkuu na mawaziri na wabunge upo katika miongozo kabisa kisheria!!

Imagine mbunge analindwa na watu wawili mpaka watatu wasioonekana je itakuwaje kwa Rais au makamu?

Maana wanajua hasara itakayotokea ya kwenda kwenye uchaguzi kama watafanya mzaha akafa kwa uzembe!!

Angalia hasara taifa lilioingia baada ya kifo cha Magufuli!!

Tuache siasa kwenye kila jambo!!

Usumbufu waliopata watu wa Mwanza siku Mpango yupo na jiografia ya miundo mbinu, hoja yako ni nyepesi mno.
 
Mwalimu miaka hiyo alikuwa na msafara wa magari yasiyozidi sita.

Watanzania ni ni watu peaceful na hayo wanaojidai wana usalama yanaweza kutokea, hayajawahi kutokea.

Mwalimu alikuwa anatembelea hadi ile Rolls Royce akipokea wageni, na niliona hilo live akimpokea Nelson Mandela, na nilikuwa maeneo ya Posta ya zamani.

Mtoa mada nikuulize,kwa fujo mnazoonyesha na kusumbua wananchi, how many assasination attempts mmeweza kuzuia?

Wanausalama wanasumbua wananchi, na naungana na Mh Phillip Mpango kwa hili.
Hiyo Idadi ya Magari ya Mwalimu ni ya Mwaka Gani? Halafu wakati Mandela anakuja Tanzania Mwalimu hakuwa Rais wa nchi hii.

Halafu kusema watu wa Usalama wana Overrate hatari zilizopo ni kutokuwatendea haki. Misafara inaongozwa na Polisi na siyo watu wa Usalama.

Wengi wenu hamjui tu, kuongoza hiyo misafara ni polisi ndiyo wanaoteseka na kama wangekuwa na uwezo bila ya shaka, wangetaka hiyo misafara isitumie hata dakika tatu iwe imepita. Ukichunguza ni polisi ndiyo wanaoshinda mabarabarani kusubiri hiyo misafara ipite. Unadhani na wao wanapenda kukaa masaa kwa masaa kusubiri msafara upite?? Yaani Polisi wanafaidika na nini kuzuia watu kwa muda wote huo?

0837536101e6bdc31e7022f5aa262f79.jpeg


Kwenye hii picha Makamu wa Rais kasimamisha msafara wake kati kati ya barabara anahutubia. Kwa mazingira kama hayo Polisi wanaweza kuruhusu magari yaelekee alipo Makamu wa Rais??
 
Kuratibu na kulinda misafara ya viongozi si jambo jepesi kama watu wengi wanavyodhani. Kuwa na mazingira wezeshi ya kulinda misafara hiyo pia si jambo la Polimi lai!!

Naona watu wengi pamoja na wanasiasa wenyewe wanachanganya kati ya kuwa na misafara mirefu na muda unaotumika kupitisha misafara kutokana na uhitaji wa huyo aliyemo kwenye msafara husika.

Leo mnataka misafara ilindwe kisiasa kuwafurahisha wanaosubirishwa bila ya kuangalia chanzo cha kusubirishwa huko. Kwa mfano misafara ya Dar toka Ikulu mpaka uwanja ndege hutumia kati ya Dakika 7 mpaka 10 kwa muda wa kawaida ama dakika 10 hadi 12 kama kuna dosari za mwendo na mpangiilio wa magari.

Lakini kama msafara huo huo toka Uwanja wa ndege kwenda Ikulu ukiwa na Mgeni unaweza kuchukua mpaka dakika 30. Sasa waliomo kwenye msafara siyo waliomo kwenye vituo (Point) vya kuongozea magari yapitayo msafara unapopita. Na Mwelekeo wa gari haudhibitiwi toka kwenye Pointi bali kule linakoelekea.

Kwa mfano kwenye Point tata ya Gerezani, wale wanaotaka Magari yazuiuwe dakika 10 kabla ya msafara kupita wanaelewa wanachokisema? Kwa mfano Magari yaruhusiwe kuelekea njia ya Kurasini, na ya kurasini yaruhusiwe kuelekea Posta. Nani atakuwa anasimamia mwendo kasi wa magari hayo??

Maana watu wanadhani kwamba ni kitu rahisi kuwafanya madereva wote wa Magari wafikirie kwa kufanana kwamba wanatakiwa waharakishe ili msafara upite. Matokeo yake kukiwa na kukwama basi lawama tena watatupiwa watu wa Usalama barabarani.

Wanasiasa wanaowalaumu Polisi leo ndiyo hao hao huwa wanawalaumu misafara inapoingiliwa. Na mikoani ndiyo Karipio huwa kubwa sana na Ma -RPC huwa kwenye changamoto kubwa sana kwenye kusimamia misafara hiyo.
Msituchoshe bwana , inaonekana umeandika jambo la msingi basi kwa kua inaonesha una uzoefu basi ulitakiwa kutafuta watafuta wastani tujue kama ni dakika 20,au 30, sio watu wanagandisha wenzao barabarani masaa na masaa.

Hoja ya Makam Rais inamashiko hoja ni kuiborsha tu
 
Kwa hiyo una unga mkono kufunga barabara ya highway mfano ya kwenda Aiport kwa masaa zaidi ya mawili kupisha tu kiongozi ????
Sijui kama unafahamu gharama/ usumbufu wanaopata watu mfano Abiria wa Ndege za kimataifa Kuachwa na ndege kwa sababu eti barabara ilifungwa?
Hapo sijaongelea wagonjwa, mama wajawazito; watu wanaotaka kuwahi makazini/kwenye Biashara nk nk nk
Mimi nimewahi kuwa Muhanga wa hii kitu hivyo najua madhara yake.....Usijitoe ufahamu!
Soma basi angalau nilichoandika ili uelewe. Hoja hapa ni nani anafunga barabara na ni nani anayesababisha barabara ifungwe kwa muda wote huo. Hayo mambo yenu ya kusiasisha mambo ya usalama siyo sawa.
 
Back
Top Bottom