Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,336
- 24,232
Msafara wa magari ya serikali, kuna ushamba wa maspidi kupindukia.
Ajali msafara wa wabunge, watu 6 walifariki
Polisi watatu walifariki ajali msafara wa Magufuli
Ajali msafara wa Mkonda huko kusini
Tuibue hoja moja inayomuelezea mwanasiasa au kiongozi anayejitutumua hadharani bila aibu wakati hastahili.
Sasa hivi kuna tabia ya viongozi, ukiacha Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na Wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama, wanaopenda kujikweza katika jamii kwa kupenda misafara na vurugu ya vimuli muli.
Ukiacha hao pao niliowata hapo juu, wengine wote ni washamba wa kisiasa. Wanajitutumua mbele ya wananchi, kwa magari ya wananchi na kwa kodi za wananchi. Wanajiweka kimbelembele wakati kwa kweli hawastahili.
Ajali ya kishamba iliyomtokea Makonda na msafara wake huko mikoa ya Kusini inatakiwa kuwa somo kwa viongozi washamba.
Mbaya zaidi hata kwa hao viongozi wanano stahili, Polisi husimamisha matumizi ya barabara kwa muda mrefu li viongozi wakuu wapite. Huo vile vile ni ushamba wa madaraka.
Huko mikoani Polisi washamba wa kujipepenea kwa mamlaka wanaweza zuia njia kwa muda mrefu huku shughuli za kiuchumi za wananchi wa kawaida zikisimama.
Makamu wa Rais, Dk Phillip Mpango aliwahi kukemea tabia hii ya kishamba, lakini pengine akakosa mamlaka ya kusimamia hili.
TUBADILIKE!