Vincent Laswai wa Kibo Palace na Trust Bureau de changes yuko matatani?

Vincent Laswai wa Kibo Palace na Trust Bureau de changes yuko matatani?

Mzigo wa sabuni za jamaa ushaanza kuwa adimu sokoni (ukitaka in bulking)
Alikuwa anaingiza bidhaa nyingi sana. Haswa consumer goods. Mfano pia ndo agent wa sukari. Hata pale TPC ni yeye, na juzi juzi wamemuongeza muhindi...Lazima bidhaa zianze kuadimika!
 
Na wewe si ungetajirika kiujanja ujanja mkuu?

Why so much hate?
tumeangalia upande mmoja wa shilingi...mara nyingi hawa matajiri wakubwa hasa waliojitokeza awamu zilizopita walitajirika kiu-kanjanja....

Haya maisha bhana... kila mtu huwa yanamgonga kwa style yake.
 
Hii habari haiko balanced.

Tunatoa shutuma nyingi kwa serikali lkn uhalisia wa tukio lenyewe ni kuwa tunahisi tu. Inawezekana kabisa tajiri huyu alikuwa na michezo michafu ya kukwepa kodi, kumiliki kiasi kikubwa cha fedha in cash etc Yote hayo ni makosa, mlitaka aachiwe kisa tu anatoa ajira kwa wananchi wa kawaida nk.

Nchi haiendeshwi hivyo lazima tufuate sheria wote maskini na matajiri. Tusubir uchunguzi ukamilike.

Nafahamu kabisa awamu hii ina mambo ya kukomoana kisiasa lkn ukiangalia kwa mfano bureau de changes zote zilizofungwa Arusha Dsm je zote zinamsapot Membe? Mwachen jiwe afanye kazi yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi na Palace Hotel ni yake?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mara ya mramba Mara ya shirima.wa precision air... Ninachojua huyu mzee alianzia kwenye ujambazi front line Kuna kipindi alivamiwa na kina mangeu na wadogo za Alex masawe kisa huko Nyuma waliiba Kisha yy. Akawa double cross wenzie walimvamia saa mbili asubuhi baada ya kumwambia awape nyumba wamuache [emoji23][emoji23][emoji23] ila wale jamaa walikamatwa na mavitu kibao ya wizi maana aliwataja .. trust bureau ndo iliyovamiwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huenda ikawa mambo ya kodi aisee.

Maana hata kama ni conspiracy kumhusu jiwe sidhani huyo Laswai anatumia hata email!!

Hivi Bureau De Change yake pale Moshi ndio ile miaka ya 90's alikua anasimama Rasta mmoja hivi nje watu tukadhani ni yake?

Nadhani ni njia ya Double Road mbele ya Panjwani kanjia ka kupanda kulia kama unaelekea msikiti wa Riadha?

Huyu Laswai mwenyewe si alikuaga na maduka ya jumla ya sukari,mafuta,etc?

Ila mkuu kwa biashara hii ya commodities sidhani kama jamaa ni high powered mpaka kumtisha jiwe!

Hata hoteli,asset kama asset itakua owned na bank,yeye anazungusha operations,na sales sio bakora za hatari..

Ila sijui bwana,mambo mengi,kila mtu ana michongo yake,huenda kamgusa jiwe pabaya..!
Jiwe anaogopa kila kitu amefeli kila kitu Sasa anataka kukusanya Kodi Hadi makanisa I[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yes, Kibo Palace ni yake.
Kuna KIBO PALACE na PALACE, Mdau kauliza kama hizo mbili zote ni zake? jibu ni yes, zote mbili anaendesha yeye.

Kibo palace ipo pale mkabala na Aicc Hospital na Palace ipo mkabala na Manispaa, mitaa ya kwa Mkuu wa Mkoa.

Mwanzo baada ya kujenga Kibo Palace walisema yupo share na Basil Mramba, naona sasa wameleta mpya ya Kenyata...Wabongo kwa kuchonga.
 
Kesi ya utakatishaji fedha inasubiri, hii kesi haina dhamana. Ataozea jela.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom