Vincent Laswai wa Kibo Palace na Trust Bureau de changes yuko matatani?

Vincent Laswai wa Kibo Palace na Trust Bureau de changes yuko matatani?

Nchi hii ya hovyo sana,
Kwenye korosho,wameburunda,tumetoka kapa,na mbwembwe zote za jeshi,sifa za kisiasa,hakuna kitu,Tsh,inazidi kuporomoka.
Badala ya kukamata mifisadi,Ana Tibaijuka,Chenge,Ngereja,na majizi yote yalioyoingia mikataba ya gesi,wanasumbua wafanyabiashara Wazalendo,wanaotoa ajira kibao kwa wa TZ.
Wao watuambie wanatoa ajira kwa nani,zaidi ya kuficha pesa yote nje ya nchi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu labda huna ufahamu Wa haya mambo...ukiwabana kina laswai ndio una kuwa umewataiti na kina hao wote uliowataja!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kazi si kidogo mkuu!! Hapo kesi ya money laundering ipo mezani!
Ni noma sana! Let’s wait and see! Lazima Itakuwa hivyo ndo maana wamevamia hadi nyumbani kwake! Na pia kumkamata mtoto wake! Enzi za Sokoine uhujumu uchumi naskia ndivyo walifanya! Lakini naona serikali hii inafanya kazi kimafioso zaidi!
Cc jaji mfawidhi
 
Hebu nionyeshe kwny comment yangu nimetaja neno kabila wapi?

Hujaona wanasema Laswai ni rafikiye Membe.

Na Membe si ndiye anatajwa kama mpinzani wa Magu?

Then huo ukabila unaosema umetoka wapi?
Msamehe atakua tuu ni shemeji yangu Tesha amepanick.
 
Dada sijakuelewa. Suala la yeye kuwa Mtu wa karibu wa Bernard Membe mbona linafahamika? Hilo la kuwa share na Kenyatta Kibo Palace ndo rumours. Inawezekana isiwe kweli. Lakini hiyo siyo hoja. Una makengeza ya akili?
Hivi ni vitoto visivyo kuwa na hoja
 
Vita inayoendelea na wafanya biashara ni vita mbaya sana. Hawaangalii jinsi uchumi unavotetereka kwa kuwafungia biashara zao, wananchi wangapi wanapoteza ajira zao na hao hao wananchi ndo walipa kodi. Tanzania taratibu inakua kama Zimbabwe
 
Yep! Wamemkamata mtoto wake na wamevamia nyumbani anakoishi! Enzi za uhujumu uchumi serikali ya Nyerere ilifanya jambo kama hilo! Lakini ni uonevu. Wanataka kumfilisi!

Ili tuwe fair maana mpaka sasa wengi hatumjui Laswai, wala alijenga kwa staili gani biashara zake, unaweza kutusaidia kidogo kujua Laswai ni nani na kwanini iwe ni yeye kwa nguvu kubwa kiasi hiki?
JF tuliyoizoea ilikuwa na balanced information. Kiasi kwamba ilijijengea heshima kubwa sana.
 
Back
Top Bottom