Vijana wengi wana hasira na Zitto Kabwe

Vijana wengi wana hasira na Zitto Kabwe

Vijana wengi wa Kitanzania Maoni yao hutoa kwenye Masanduku ya kura sio Instagram! Mbowe na Vijakazi wake mnalijua hilo ndio maana 2009 Mkakata Jina la Zitto, Tangu mwaka Jana Mlipiga danadana Uchaguzi wa Mwenyekiti kuogopa 'Chuki ya Vijana kwa Zitto', Leo mnaleta kura za Instagram!

Unajua 'Chuki ya Vijana' dhidi ya Zitto ndio iliyolazimisha Slaa kufuta Uchaguzi wa BAVICHA uliompa ushindi kafulila na kumfukuza Chamani kwa kudai ni Sisimizi?

Zitto kwishney!!!
 
sio siri wacha niwe tu wazi katika vijana niliona bado wanamfuata zito ni wale tu wakiislam lakini mimi binafsi kipindi hiki zito alipotimuliwa chadema sijaona mshabiki wa chadema wakristo wanamshabikia zitto samahani kama kuna watu nimewakwaza
Naona umekiri rasmi kuwa Chadema ni chama cha Wakirsto na tatizo la Zitto ni Uislam wake.

Shukrani kaka kwa kutufumbua macho.
 
hizo hekaya za abunuasi zilizotungwa hapo ufipa na slaa zimepitwa na wakati..zito ni kiongozi makini sana
 
Akili ya zito ni zaidi ya viongozi na wanachama wote wa chadema kwa pamoja
 
unachekesha kweli! Unataka kujaribu kuonyesha kuwa Zitto ni sawa na Mbowe? Mbowe hana doa. Mbowe ni mtetezi wetu. Maturity ya Mbowe imemzidi mwenyekiti mwenza wa ACt Zitto mara 100000000.

Zitto angekuwa na akili asingeasisi chama cha kijinga cha ACT kitakachokufa na kuzikwa hivi karibuni.

Zitto is a disgrace! Zitto is a hooligan

ni kweli mbowe ni mtetezi wa matumbo yenu chadema,, sio mtetezt wa watanzania
 
Zito aliaminiwa na Chama na akakitumia kujitangaza lakini aliwaka tamaa na kushawishiwa na Wapinzani wa chama chake kukihukumu. Haya pia ni maelezo ya wapinzani wa Zitto mwenyewe
Yeye sasa anahusishwa na ACT na hajasema hadharani ataaminiwaje?
 
[/B]Yote haya umeyajua leo Baada ya Zitto kukataa kuwa Sabufa la Wachagga kama alivo Lissu?

Zitto ndiye facilitator wa uhuni na ndie mpangaji wa mipango isiyotekelezeka ya kuimaliza Chadema kwa ufadhili wa CCM
 
zitto kabwe ndo mbunge mwenye ushawii mkubwa zaidi tanzania hata kama cdm wataendelea kumchafua
 
wanachama wa cdm uwa kama kondoo hakimsikia mbowe kasema jamaa msaliti basi nawo wanangangania tupenikuindani kabisa usaliti wa zitto na si upuuzi mliomezeshwa na kamati kuu
 
Unataka vijana wasiwe na hasira dhidi ya mtu aliyeunda kikundi cha kumpindua mwenyekiti wake? PM7?
Unataka vijana wasiwe na hasira juu ya mtu anayejitangaza kuwa mgombea urais awamu inayofuata katikati ya kampeni badala ya kumpigia kampeni mgombea wa chama chake?
Unadhani vijana hawatakuwa na hasira dhidi ya mtu aliyewaengua wagombea ubunga wa chama chake ili kuwapisha wale ccm kupita bila kupingwa?
Unadhani vijana watamvumilia mtu anayejinasibu kutumia uchawi waziwazi dhidi ya mahasimu wake,familia zao pamoja na wanyama wasio na utashi kama panya?
NADHANI VIJANA WANASABABU ZAKUWA NA HASIRA DHIDI YA HUYO MTU.
 
Zitto yuko sahihi kabisa, na watanzania wengi bado tuna imani naye!

CHADEMA wanamtenga kwa ajili ya dini yake na kabila lake, pia kwa ajili ya misimamo yake isiyoyumbishwa!

BAVICHA wengi hawampendi Zitto kwa sababu wanafuata mkumbo wa viongozi wao!

wewe msalani tunakujua ni CCM damu.... sasa tangu lini Zitto akawa mtu mwema kwa CCM??!! Acheni unafiki ninyi CCM maana mmemtumia Zitto vibaya na baada ya kugundulika na chama chake kwamba ni msaliti sasa na ninyi mmeamua kumdampu kama kawaida yenu. Unajua CCM kwa kukosa watu wenye akili ndio wamemfanya Zitto kujulikana kwamba alipewa pesa na serikali ya CCM ili kukihujumu CHADEMA na hata sasa hivi wewe msalani kwa kukosa akili kwako unaendelea kudhihirisha namna ambayo CCM imekasikrika kwa Zitto kushindwa kutimiza malengo aliyopewa na CCM baada ya kuchukua pesa za watanzania masikini toka kwa serikali ya CCM. Siku zote nikuambie sasa kwenye jumuia yeyote rasilimali watu ndio utajiri mkubwa kuliko chochote ila CCM hakuna mwenye akili zaidi ya ujambazi na unyang`anyi.
 
Tatizo ni kwamba bado vijana wengi hatujielewi na hatujui nini tunataka,sisi ni bendera tu na kuendeshwa na emotions.
Zittokabwe hatumuelewi na hatumtumii vizuri,Zittokabwe ni zaidi ya mwanasiasa,he is a whistle blower anafanya siasa kwa uwanja mpana bila kujifungia kwenye maboksi ya vyama.
 
Mwana mapinduzi yeyote hawezi kuwa kigeugeu. Anapaswa kusimama imara bila kuyumbishwayumbishwa. Sasa huyu bwana amekuwa akitumikia mabwana wawili Kwa wakati mmoja; Mara yuko CDM Mara Ana agenda na watu wa CCM. Alipaswa kuamini kuwa CDM ndio Chama ambacho kingemwezesha kufanikisha mapinduzi watakayo watanzania.

Kama kuna mambo ambayo yalikuwa yanamfanya aitilafiane na wenzake ndani ya Chama angepambane Kufa na kupona wafikie muafaka na kazi ya ukombozi iendelee. Sasa Mara yuko huku, Mara kule; Sisi tumweleweje?

Kimsingi ninaona kuwa mwisho wake wa kisiasa Umefika Kwa kutokuwa serious na Yale aliyoaminiwa nayo na hivyo basi ajaribu kutafuta njia mbadala ya kuendesha maisha yake Kwani Kama ni siasa ameshashindwa. Vijana wa kitanzania walimtegemea ashirikiane nao kuusaka ukombozi wa kweli kumbe yeye alikuwa anasaka tonge la muda mfupi. Sasa Sisi vijana wapenda long term results tumemchukia na kumdharau mno. Arudi Kigoma akalime!
 
Wewe si Mtanzania! Hakuna Mtanzania mwenye kuhujumu ukombozi against Ufisadi, Ujangili, Biashara ya Sembe, Ukwapuaji wa Rasilimali za Taifa... Zitto ni mhujumu wa mabadiliko yenye tija kwa Watanzania... imewahi kutamkwa hapa kuwa Zitto si Mtanzania! Pengine na wewe ndo katika wale mamluki wenye kuinajisi nchi yetu... pata muda soma ile taarifa kipelelezi kuhusiana na hujuma za Zitto kwa Chadema; pale kuna evidence ya a/number, amount, wahusika wakuu na hata number zao za simu zilizotumiwa mshiko wa kuihujumu CHADEMA, kuhujumu Watanzania ili Umasikini uendelee kutamalaki...
sisi watanzania hatujasalitiwa na zito. labda ameisaliti familia yako.
 
Back
Top Bottom