Vijana wa Dar na Vibegi mgongoni

Vijana wa Dar na Vibegi mgongoni

Buy your own car
d66bdd6d33527a0cc0d61b15e9fbc052.jpg
 
Hata akinamama mibegi mikubwa utafikiri atakaa huko siku mbili kumbe anarudi jioni, na anajali begi lake kuliko abiria wenzie, anakugonga nalo bila kujali
 
Habari wana JF,

Najua kama mabegi hutumika kuweka vitu mbalimbali ila kero yangu ni kwa wale wanayoyavaa mgongoni kwenye daladala/mwendokasi kama tunavyojua zinavyajaza bora hata uweke mbele au umuombe mtu akushikie kuna wengine wabishi kuyaweka vizuri hata ukimwambia halafu kwanini sikuhizi yamekuwa mengi sana tofauti na zamani?

Sasa usiombe gari lifunge brake ghafla utaipata fresh hata mikoba ya wanawake nayo ni kero kubwa.
Kwanini usinunue garu yako
 
Ndugu zangu wale mnaopenda kubeba mabegi kama mnakwenda shule tambueni kwamba iyo mibegi yenu mnayobeba mgongoni bila sababu za msingi inawakera wenzenu hasa kwenye ule mbanano wa kwenye daladala.

Unakuta mtu kabeba mbegi umetuuuuna utafikiri amebeba kitu gani cha maana kumbe ubishoo tu umemjaa.Sawa hatukatai kuna wengine wamebeba laptop na baadhi ya vitu vya msingi vya kiofisi lakini wengi wanabeba hii mibegi kama urembo ilimradi tu na yeye aonekane kwamba ni mtu wa mishemishe hapa town.

Aisee badirikeni bana mana mfano kwenye mabasi ya mwendokasi ndo mnakera balaa na mbanano ule.Kama huna ulazima wa kubeba begi tafadhali acha nyumbani kwako ili kuepuka kuwakera wengine kwenye huu usafiri wetu wa public.

NI hayo tu,ukitoa povu ujue imekutachi
 
sawa kaka mi mwenyewe nabeba sana ila simkeri mtu nikifika kwenye daladala naangalia utaratibu kama kumpa mtu anishikie au kama kuna sehemu niweke ikishindikana sana naweka kwa mbele

Huwa unabeba nini hadi umpe MTU akushikie!!! Yaan wanaume wa Dasilika iko namna
 
Nonsense unataka watu wote wasafiri kama unavyosafiri wewe...? Mimi bag langu lazima liwe na pc, nguo za kubadili, mswaki na dawa ya meno, vitambulisho, ATM cards, kijiko, sahani, maji, first aid kit, subwoofer ndogo notebook, na coins kama za elfu 10 kwaajili ya nauli...kiukweli siwezi kulieka chini maana linaniweka mjini!

Wewe itakuwa kalubandika
 
Habari wana JF,

Najua kama mabegi hutumika kuweka vitu mbalimbali ila kero yangu ni kwa wale wanayoyavaa mgongoni kwenye daladala/mwendokasi kama tunavyojua zinavyajaza bora hata uweke mbele au umuombe mtu akushikie kuna wengine wabishi kuyaweka vizuri hata ukimwambia halafu kwanini sikuhizi yamekuwa mengi sana tofauti na zamani?

Sasa usiombe gari lifunge brake ghafla utaipata fresh hata mikoba ya wanawake nayo ni kero kubwa.

…patamu pale mwenye begi alikuwa kaliweka mahali chini penye uchafu, halafu kaingia nalo hivyo hivyo kwenye daladala na kakuwekea mgongoni au begani tena ukiwa umevaa shati jeupe..
 
mkuu usiashangae sana hao wote unaowaona na mabegi ni wanafunzi wameamua kurudi shule si unajua jamaa hana maskhara ktk vyeti,so vumilia tu wakihtmu hutowaona na mabegi.
KIYUTIIII? hahahaaaaa mkuu unajua kukisia
 
Back
Top Bottom