Vijana wa Dar na Vibegi mgongoni

Vijana wa Dar na Vibegi mgongoni

Katika siku za karibuni kumeibuka kitu kinachoitwa 'fasheni' ya vijana ya kubeba mabegi ya safari na kuzunguka nayo kwenye vyombo vya usafiri jijini Dar!

Unapowaona hao vijana walivyobeba mabegi yao ya safari unaweza kuhisi wanasafiri kwenda mikoani, kwa hiyo ukadhani wanaenda Ubungo Terminal kwenda kupanda mabasi ya kuelekea mikoani.

Kumbe katika uhalisia hao vijana wameichukulia hiyo hali ya kubeba hayo mabegi kuwa 'fasheni' na kuamua kuzurura nayo jijini Dar!

Hiyo inayoitwa 'fasheni' ya vijana imesababisha kero kubwa sana kwenye usafiri wa Umma hapa jijini Dar, hususani kwenye mabasi ya mwendo kasi, ambapo husababisha mabegi yao hayo wanayoyavaa mabegani, kuchukua nafasi kubwa kwenye hayo mabasi na hivyo kuwakosesha abiria wengi usafiri wa kwenda makazini na wanaporejea toka kwenye shughuli zao.

Nadhani ni muhimu kwa sasa wananchi wote tunaokerwa na hiyo hali inayosababisha kero kubwa sana kwenye usafiri wa Umma kutokana na 'fasheni' hiyo ya kipuuzi ya hao vijana, tuikemee kwa nguvu zote tabia hiyo ili hao vijana wakome kuendelea na hiyo 'fasheni' yao ya kipuuzi.
Sasa ndugu, kazi ninayofanya inahitaji niwe laptop muda wote hivo ni lazima niwe na begi.
Maisha ya sasa yanauhitaji mkubwa sana wa laptop kwa hiyo itakuwa ngumu kulikwepa hilo
 
utajuaje kama ni fasheni au amebeba vitu vyake vya muhimu..au umeingia kwenye public transport kwa bahati mbaya!
 
sio vijana tu sasa hivi mpaka watu wazima.....halafu utakuta dume zima kutwa limebeba begi....sasa sijui na wao wanaweka pedi, poda na chupi kama wanawake
 
Sasa ndugu, kazi ninayofanya inahitaji niwe laptop muda wote hivo ni lazima niwe na begi.
Maisha ya sasa yanauhitaji mkubwa sana wa laptop kwa hiyo itakuwa ngumu kulikwepa hilo
siku hizi simu ina kila kitu kinachohitajika kwenye laptop
 
ila kuna pochi za wanaume siku hizi ,mtu ana simu tatu,wallet japo haina zaidi ya elf 2 ,unataka aweke wapi? mwingine ana laptop plus macharger ya simu.acha uzamani wewe
494df773d0729d1f21d7a93898887677.jpg
stock-photo-men-s-casual-outfits-standing-over-gray-grunge-background-with-space-beauty-and-fashion-concept-507406090.jpg
Mis umeuwa eti hayana zaid ya 2000[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Sasa ndugu, kazi ninayofanya inahitaji niwe laptop muda wote hivo ni lazima niwe na begi.
Maisha ya sasa yanauhitaji mkubwa sana wa laptop kwa hiyo itakuwa ngumu kulikwepa hilo
Lkn haka kamtindo kamezuka hivi karibun swal zaman alikuwa hamtumii hizo laptop mbon hatukumiona na hivyo vibegi
 
Embu weka picha kwa maana mabegi ya safari yapo ya aina nyingi.
 
Kuna mwingine niliona ameweka deki chakavu ya SUMSUNG ili ionekane kama laptop, sasa nikawa naona hiyi laptop kila siku hatoi, kuna siku nilasema ngoja nichungulie, nilichoka!
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
utajuaje kama ni fasheni au amebeba vitu vyake vya muhimu..au umeingia kwenye public transport kwa bahati mbaya!
Hatukatai kuwa wapo wachache ambao wanayatumia hayo mabegi kubebea vitu vyao muhimu kama laptop na vitu vingine vya thamani.

Hata hivyo vijana walio wengi wanaamua tu kuzurura nayo hayo mabegi yao, wakiichukulia hiyo kama fasheni.
 
Hatukatai kuwa wapo wachache ambao wanayatumia hayo mabegi kubebea vitu vyao muhimu kama laptop na vitu lingine vya thamani.

Hata hivyo vijana walio wengi wanaamua tu kuzurura nayo hayo mabegi yao, wakiichukulia hiyo kama fasheni.
How can you distinguish dem nigga?
 
Sijui wanaweka nini humo ndani, maana ni kama fashion kwa sasa.
Juzi wakati nipo Taifa kuna kijana nilikaa nae jirani wakati anafungua nikachungulia, Ajabu katoa headphone ya simu na hamkuemo na kitu kingine cha ziada ndani nilichoka sana.

Binafsi naona kama ni ushamba fulani hivi ambao vijana wanalimbukia bila kujielewa.
Sio Dar tu mkuu, ni Tanzania nzima.Hii ni fashion yao kwa sasa. Kwa kweli kubeba begi tupu eti kisa fashion,ni ujinga wa hali ya juu. Kazi ya begi ni moja tu, kubebea vitu.Vijana acheni ujinga huo.
 
Lkn haka kamtindo kamezuka hivi karibun swal zaman alikuwa hamtumii hizo laptop mbon hatukumiona na hivyo vibegi
Zamani ni watu wachache sana waliokuwa na uwezo wa kumiliki laptop, kwanza miaka hii kwa wanafunzi wa elimu ya juu laptop imekuwa kama moja ya nyenzo muhimu halafu matumizi ya laptop yamekuwa makubwa sana siku hizi.
Pili, zamani ilikuwa ukienda dukani kununua laptop ulikuwa unapata bag za laptop za mkanda kuning'iniza begani huwezi iweka mgongoni na wenye uwezo huo walikuwa wachache. Sasa hivi ukienda kununua laptop mpya ukihitaji na bag lake unapata ya kuvaa mgongoni.
.
.
.
Sasa kwa faida ya ya wote ni kuwa zamani tuliosoma vijjn daftari tulikuwa tunaweka kwenye rambo/marbolo, waliokuwa na uwezo walishonewa mifuko ya vitambaa. Sasa hv maisha yamebadilika hata wanafunzi wanawrka daftari kwenye bag za kuning'iniza mgongoni kutokona na urahisi wa kubeba.
.
.
Anaedhani kwamba mtu utabeba tu mbegi kama chizi eti fasheni sio kweli japokuwa wanaweza kuwepo wachache. Mimi nina miaka 11 kazini shughuli yangu huw inanilazimisha kutumia pc/laptop daily... Zamani nilikuwa nina begi la kuning'iniza lakini ss hivi ninatumia ya mgongoni.
 
Acheni ushamba hilo beg ni personal package ,unaweza weka ipad,gadgets yoyote ile ,vitabu hata condom because its safe
Ndio kwani wavunja sheria? Tumeona hata picha za mababu na baba zetu walivyokuwa wanaiga kuvaa suruali chupa na fupi, bwanga, razioni, vishati vumebana na kola kubwa, afro, jinsi ya kucheza mziki n.k. n.k.
Vijana haya mambo ndio wakati wao, ila mbona mbona hata viongozi kwenye nchi zilizoendelea wanavaa masuti yao, headphones na rucksacks?!
Kwanza kwenye rucksacks waweza beba kila utakacho, kuanzia karanga, viazi, mihogo na kachupa ka chai, kalamu, notebooks, ma files, vitabu, simu, laptops, na vitu kedekede...
Kama wasiopenda haya hawataki basi wabebe mifuko yao waipendayo..
 
sio vijana tu sasa hivi mpaka watu wazima.....halafu utakuta dume zima kutwa limebeba begi....sasa sijui na wao wanaweka pedi, poda na chupi kama wanawake
Hahaha kumbe umewajua wengine wanaweka vipodozi kama mabinti akifika mahali anajinakshi nakshi maana kaka poa nao ndio fashion zao wanakuwa na vibegi kama mabinti
 
Back
Top Bottom