Vijana wa Dar na Vibegi mgongoni

Vijana wa Dar na Vibegi mgongoni

Wengi wenye hayo mabegi hasa mida ya asubuhi na jioni huwa wanaelekea ama kutoka maofisini, darasani na huwa wamebeba laptop, karatasi ama vitabu muhimu kwa siku hiyo. Hivyo kuwaambia wasibebe hayo mabegi ni sawa na kumwambia mkulima aende shambani bila jembe huku ukihimiza afanye kazi.

Tatizo la kumpa mtu akushikie au kuliweka mbele ukizubaa kuna wajanja wengine wanaweza kulifungua na kuchukua vilivyomo ndani au kushuka nalo kabisa, hii hutokea mara nyingi kutokana na msongamano mkubwa kwenye vyombo hivi vya usafiri.

Wengine wanaweza kukuwekea kitu ndani na ukazushiwa kesi ushukapo kituoni.

Tatizo mjini maadili yameshaharibika na hakuna wa kumwamini.
sasa kuweka mbele na kuweka nyuma wapi salama zaidi
 
Kwa hio wewe unataka wabebe mifuko ya rambo?
hapana wabebe tu maana wanaweka vitu tatizo huanza pale kwenye msongamano wa daladala halafu abebe kwa nyuma bora akiweka mbele
 
Kweli mkuu mi juzi nimegombana na jamaa alikuwa kabeba beg mgongoni kumbe ndani kaweka samaki wabichi wanatiririsha mimaji ya barafu alafu na yeye kesha loa kwenye koti alokuwa amewaa hana habari si akanipaka maji!!asee nilimchenchia sana
Duh pole kaka mfano angeweka mbele angeloa mwenyewe
 
Nonsense unataka watu wote wasafiri kama unavyosafiri wewe...? Mimi bag langu lazima liwe na pc, nguo za kubadili, mswaki na dawa ya meno, vitambulisho, ATM cards, kijiko, sahani, maji, first aid kit, subwoofer ndogo notebook, na coins kama za elfu 10 kwaajili ya nauli...kiukweli siwezi kulieka chini maana linaniweka mjini!
 
Nonsense unataka watu wote wasafiri kama unavyosafiri wewe...? Mimi bag langu lazima liwe na pc, nguo za kubadili, mswaki na dawa ya meno, vitambulisho, ATM cards, kijiko, sahani, maji, first aid kit, subwoofer ndogo notebook, na coins kama za elfu 10 kwaajili ya nauli...kiukweli siwezi kulieka chini maana linaniweka mjini!
Kazi kweli kweli.
 
Ndio maana siku hizi vijana wengi mabega yao yamerudi nyuma vifua mbele.
 
Ukichoka hizo kero nunua gari yako mkuu. Huku kila mtu analipa nauli
 
Back
Top Bottom