Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 19
Hakukuwa na majibu yoyote yale, simu ilikuwa ikiita tu lakini haikuwa ikipokelewa. Alishindwa kujua kulikuwa na tatizo gani lakini kila alipofikiria kwamba alikwenda kumpokea Mchungaji Mark, alihisi kwamba mwanaume huyo huyo alikuwa bize katika kufanya mazungumzo na mchungaji.
Muda ulizidi kusogea, mpaka inaingia saa tisa usiku wa manane bado majibu yalikuwa yaleyale. Hilo kidogo likaanza kumtia hofu na kitu kimoja na cha kwanza kilichomjia kichwani mwake ni kwamba Cassian alikuwa amepata ajali mbaya.
Akahisi mwili wake ukipigwa ganzi, hakutaka kuona hilo likitokea, kitu alichokuwa akikihitaji ni kuona akifunga ndoa naye na hata kama angepata ajali na kufa, basi kitu hicho kitokee wakati wakiwa ndani ya ndoa.
“Mpenzi nina wasiwasi,” alisema Evelyne, alikuwa amempigia simu Mwajuma.
“Wasiwasi wa nini tena?”
“Cassian. Aliondoka kwenda kuonana na Mzungu ambaye ndiye atakuwa mchungaji wa kesho. Hajarudi mpaka sasa hivi,” alisema Evelyne.
“Aliondoka saa ngapi?”
“Tangu saa tatu usiku!”
“Mmh! Lakini usijali! Inawezekana kaenda sehemu kunywa. Si unajua wanaume,” alisema Mwajuma.
Maneno ya rafiki yake huyo hayakumuingia kichwani, bado alikuwa na hofu kwa kuhisi kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea upande wa pili.
Muda ulizidi kusogea, hakupata usingizi, ilikuwa ni heri kukosa kitu chochote kile lakini si kuikosa ndoa ambayo iliutesa moyo wake, ndoa ambayo aliamini piga ua ilikuwa ni lazima kuyabadilisha maisha yake.
Ilipofika saa kumi na moja na kuona kimya, hakutaka kuendelea kubaki hospitali, haraka sana akatoka na kuanza kwenda katika hospitali zilizopo karibu, alihisi kwamba mwanaume wae huyo alikuwa huko. Alikwenda kwenye hospitali tatu lakini huko hakufanikiwa na ndipo akapata wazo la kwenda nyumbani kwa Cassian.
Hakukuwa na majibu yoyote yale, simu ilikuwa ikiita tu lakini haikuwa ikipokelewa. Alishindwa kujua kulikuwa na tatizo gani lakini kila alipofikiria kwamba alikwenda kumpokea Mchungaji Mark, alihisi kwamba mwanaume huyo huyo alikuwa bize katika kufanya mazungumzo na mchungaji.
Muda ulizidi kusogea, mpaka inaingia saa tisa usiku wa manane bado majibu yalikuwa yaleyale. Hilo kidogo likaanza kumtia hofu na kitu kimoja na cha kwanza kilichomjia kichwani mwake ni kwamba Cassian alikuwa amepata ajali mbaya.
Akahisi mwili wake ukipigwa ganzi, hakutaka kuona hilo likitokea, kitu alichokuwa akikihitaji ni kuona akifunga ndoa naye na hata kama angepata ajali na kufa, basi kitu hicho kitokee wakati wakiwa ndani ya ndoa.
“Mpenzi nina wasiwasi,” alisema Evelyne, alikuwa amempigia simu Mwajuma.
“Wasiwasi wa nini tena?”
“Cassian. Aliondoka kwenda kuonana na Mzungu ambaye ndiye atakuwa mchungaji wa kesho. Hajarudi mpaka sasa hivi,” alisema Evelyne.
“Aliondoka saa ngapi?”
“Tangu saa tatu usiku!”
“Mmh! Lakini usijali! Inawezekana kaenda sehemu kunywa. Si unajua wanaume,” alisema Mwajuma.
Maneno ya rafiki yake huyo hayakumuingia kichwani, bado alikuwa na hofu kwa kuhisi kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea upande wa pili.
Muda ulizidi kusogea, hakupata usingizi, ilikuwa ni heri kukosa kitu chochote kile lakini si kuikosa ndoa ambayo iliutesa moyo wake, ndoa ambayo aliamini piga ua ilikuwa ni lazima kuyabadilisha maisha yake.
Ilipofika saa kumi na moja na kuona kimya, hakutaka kuendelea kubaki hospitali, haraka sana akatoka na kuanza kwenda katika hospitali zilizopo karibu, alihisi kwamba mwanaume wae huyo alikuwa huko. Alikwenda kwenye hospitali tatu lakini huko hakufanikiwa na ndipo akapata wazo la kwenda nyumbani kwa Cassian.