Viganja Mashavuni Mwangu

Viganja Mashavuni Mwangu

Mkuu sidhani kama mm na ww tumeshawahi kuquotiana ila kama kuna sehem nilikukosea nisamehe mm sijapebda kauli yako sipo hivyo hii jf tu
tumequotiana mara nyingi sana kwa ID tofauti tofauti mwaka wa 2 sasa.
 
SEHEMU YA 13

“Kama ni furaha, muonyeshee, usimfanye ashtukie kitu chochote kile, halafu huo ujumbe wake ulioingia, ufute. Halafu kesho nitakupeleka katika hospitali ya swahiba wangu akakufanyie vipimo tena,” alisema Osman.

“Sawa. Nitashukuru!”
Hicho ndicho alichoambiwa, hakutaka kuonyesha tofauti yoyote ile. Hakutaka kuondoka muda huo, alikaa mpaka ilipofika usiku ambapo akajiandaa na kuelekea nyumbani.

Alipofika, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumkumbatia Evelyne kwa furaha tele, alimletea unafiki, hakuonyesha tofauti yoyote ile machoni mwake, kama ilivyokuwa juzi na jana ndivyo ilivyokuwa siku hiyo kiasi kwamba msichana huyo akahisi hakukuwa na jambo lolote baya na inawezekana ujumbe ule haukuenda, na kama ulienda basi hakuuona.

Wakati Cassian akiwa amekwenda bafuni kuoga, haraka sana Evelyne akachukua simu ya mpenzi wake huyo na kuanza kuangalia. Akaenda sehemu ya meseji na kuangalia katika uwanja wa kuwasiliana naye, hapo, hakukutana na ujumbe wowote mpya kuonyesha kwamba kumbe meseji hakuwa ameipata.

Kidogo moyo wa Evelyne ukarudi kwenye amani, furaha ambayo ilikuwa imepotea ikarudi tena. Cassian alipomaliza kuoga, akarudi chumbani, akamnyanyua Evelyne na kumtupa kitandani ambapo akaanza kumvua nguo moja baada ya nyingine na kuanza kufanya mapenzi.
 
Anachojaribu kufanya Cassian kwa Evelyne ni psychological torture... ni adhabu mbaya sana...

Mtu anajua kuhusu mambo yako lakini anajifanya hajui ili aendelee kukujua zaidi...


Cc: mahondaw
 
SEHEMU YA 14

Mpaka kufikia hatua hiyo msichana huyo hakujua kama mwanaume huyo alijua kila kitu, hali aliyokuwa amemuonyeshea siku hiyo ilikuwa kama siku nyingine, wakalala na siku iliyofuata Cassian kuaga kwamba anaelekea kazini lakini ratiba yake ya kwanza kabisa ni kuwasiliana na Osman ambaye akamwambia hospitali ya kwenda na kuonana huko.

Hawakutaka kuchelewa, moja kwa moja wakaingia ndani ambapo Osman akamwambia tatizo alilokuwa nalo rafiki yake huyo ambapo daktari huyo hakuwa na tatizo lolote lile zaidi ya kuanza vipimo.

“Huna tatizo lolote lile. Mbegu zako zina nguvu za kuzalisha hata watoto uwanja mzima! Wewe tu,” alisema daktari baada ya saa kumi za kusubiri majibu.

“Kweli?”
“Ndiyo! Kwani kuna mtu alikwambia huna uwezo?”
“Ndiyo! Kwa hiyo mambo yapo poa?”
“Kabisa kabisa. Mwanaume ngangari kama chuma,” alisema daktari huyo huku akimpongeza Cassian kwa kumpigapiga mgongoni.

Wakati Cassian akiwa amekwishapata majibu yake, Evelyne akampigia simu Mwajuma na kumwambia kwamba alitaka kuonana naye.

Wakaonana na kuumuhadithia kila kitu kilichokuwa kimetokea, jinsi alivyowaandikia meseji madaktari na kwa bahati mbaya kumtumia mpenzi wake.

“Una hatari sana!”
“Wewe acha tu! Lakini hakushtukia. Angejuaaaa! Nafikiri angenichinja usiku ule,” alisema Evelyne huku akionekana kuwa na furaha tele.

“Mmh! Umecheza kama Pele. Kwa hiyo!”
“Sasa hivi hata kutuma meseji za kijinga siwezi. Nisije kukosea tena. Ile haikwenda, nikirudia tu, inakwenda,” alisema msichana huyo pasipo kugundua kwamba Cassian alijua na alitaka kumfanyia mchezo hatari, kumkataa siku moja kabla ya harusi.

Je, nini kitaendelea?
 
Back
Top Bottom