Viganja Mashavuni Mwangu

Shunie

JF-Expert Member
Aug 14, 2016
152,999
453,892
Nyemo ChilonganiSEHEMU YA 01

Cassian alikuwa kimya, macho yake yalikuwa yakiangalia baharini huku mawazo yake yakiwa mbali kabisa. Moyo wake ulichoka, maumivu aliyokuwa akiyasikia moyoni mwake hayakuweza kuelezeka.

Alikuwa bilionea mkubwa, mwenye makampuni mengi, migodi ya dhahabu na kila kitu ambacho kingemfanya kustahili kuitwa bilionea. Alimshukuru Mungu kwa utajiri aliokuwa nao lakini tatizo lilikuwa moja tu, hakuwa na mtoto.

Hilo lilikuwa pigo kubwa katika maisha yake, wakati mwingine alikuwa akimuuliza Mungu juu ya kilichokuwa kimetokea. Kwa nini alimpa utajiri mkubwa na kumnyima mtoto? Utajiri ungekuwa na maana gani kama tu hakuwa na mtoto ambaye angekuja kuurithi baada ya yeye kufa?

Hakuwa na furaha hata kidogo, kila siku moyo wake ulichoma kama moto kiasi kwamba alimuonea aibu mkewe, hata kukutana naye wakati mwingine aliogopa kutokana na tatizo lililokuwa mwilini mwake.

Hapo ufukweni mawazo yake yalikuwa mbali kabisa. Alitulia ndani ya gari huku akionekana kuwa na mawazo lukuki, alikaa garini kwa dakika kadhaa ndipo akaamua kutoka na kuanza kutembea. Kwa jinsi alivyokuwa akiwaza mpaka wakati mwingine machozi yalikuwa yakimtiririka mashavuni mwake.

Aligombana na dada zake kwa sababu hakuwa na mtoto. Kipindi cha kwanza ndugu hao walifikiri kwamba mwanamke aliyekuwa akiishi naye ndiye alikuwa na matatizo lakini baada ya kupima katika hospitali tatu, zote zilionyesha yeye ndiye alikuwa na matatizo.

Hakutaka kuwaambia ndugu zake ukweli, alikuwa tayari kugombana nao na hata kuchukiana maisha yake yote lakini si kuwaambia ukweli kwamba tatizo la kutokupata mtoto lilisababishwa na yeye na si mpenzi wake kama walivyokuwa wakihisi.

“Kwa nini wanamuonea? Kwa nini hawataki kuniuliza ili wajue ukweli kwamba Evelyne hana tatizo?” alijiuliza huku machozi yakimtiririka mashavuni mwake.

Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake ya kila siku. Moyo wake ulimuuma mno, hakuona thamani ya utajiri, bila kuwa na mtoto maisha yake yangekuwa hivyohivyo mpaka kifo chake na mali kubaki kwa ndugu zake.


Screenshot_20180701-204239.jpeg
 
SEHEMU YA 02

Si kazini, si nyumbani au barabarani, kila alipokuwa Cassian alikuwa myonge, hakuwa muongeaji, wakati mwingine alihisi kabisa mwili wake ukianza kupungua kutokana na matatizo aliyokuwa nayo.

Alipenda kuwa na mtoto, kila alipowaona wanaume wenzake wakiwa na watoto barabarani moyo wake ulimuuma, alitamani kuona kama ingekuwa yeye, alitamani kuona naye akiwabeba watoto wake kama walivyofanya watu wengine.

Mpenzi wake ambaye alimchukulia kama mkewe, Evelyne ndiye aliyekuwa akimfariji kila siku, alimwambia kwamba hakutakiwa kukata tamaa na ipo siku ambayo Mungu angetenda muujiza na hatimaye kupata watoto.

Alimwangalia Evelyne machoni, aliyaona maumivu yake, aliona jinsi msichana huyo alivyokuwa akiumia kwa kuwa tu hakuwa na mtoto. Alimuona kuwa mwanamke mwenye uvumilivu sana, aliyevumilia maneno ya ndugu na wakati hakuwa na tatizo bali tatizo kubwa lilikuwa kwake.
“Pole sana mke wangu,” alisema Cassian huku akimwangalia Evelyne.

“Usijali mume wangu! Maneno ya watu huwa hayanisumbui hata kidogo! Mimi nimekupenda wewe, katika shida na raha hakika tutaendelea kuwa pamoja na kamwe sitokuacha,” alisema Evelyne maneno ambayo kwa Cassian yalionekana kuwa faraja kubwa.

“Ila sina uwezo wa kumpa mimba mwanamke!” alisema Cassian.
“Hata kama! Nimekupenda wewe mpenzi, mtoto ni majaaliwa ya Mungu,” alisema Evelyne huku akimwangalia mpenzi wake huyo machoni mwake.

Japokuwa mkewe alijitahidi sana kumfariji lakini hakufarijika, bado alijiona kuwa na mzigo mkubwa kichwani mwake. Alimuomba Mungu kila siku bila kukoma, maombi yake makubwa yalikuwa ni kupata mtoto.

Ni kama alimuona Mungu akiwa ameziba masikio, alijitahidi kufunga na kuomba lakini matokeo yalikuwa yaleyale kwamba hakupata mtoto.

Hilo lilimuuma mno, alichokifanya ni kwenda kwa madaktari wengi pamoja na mkewe, katika kila hospitali aliyofika, aliambiwa kwamba alikuwa na tatizo kubwa katika mfumo wa utengenezaji mbegu, hazikuwa na nguvu za kumpa mimba mwanamke.
 
SEHEMU YA 03

Kila aliposikia sehemu kuna mikutano ya injili, yeye alikuwa wa kwanza, wakati mwingine alimuacha Evelyne nyumbani na kwenda huko, alitaka kumuona Mungu akimtendea muujiza lakini alimuona Mungu kuchelewa kwani kwenye kila alipofanyiwa maombezi aliambiwa kabisa kwamba angepata mtoto lakini matokeo yalikuwa yaleyale, hakupata mtoto.

Maumivu hayakupungua moyoni mwake, alikuwa mtu wa majonzi na kulia kila siku. Hakuona thamani ya utajiri, wakati mwingine alimwambia Mungu kwamba alikuwa tayari kupoteza kila kitu lakini mwisho wa siku aje kuwa na mtoto lakini maombi yake yote hayo yalionekana kama si kitu mbele za Mungu.

“Mchungaji! Kwa nini Mungu hajibu maombi yangu?’ aliuliza Cassian huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Kuna siku atafanya jambo. Nakwambia kwamba kuna siku utapata uzao wako wa kwanza,” alisema mchungaji huku akimwangalia Cassian.
“Kweli?”

“Unachotakiwa ni kuamini. Uwe na imani hata kama ni ndogo kama mchanga, hakika Mungu atafanya jambo,” alisema mchungaji huku akimwangalia Cassian.

Aliteseka usiku, hakulala vizuri, kila wakati alikuwa akishtuka usiku na alipoyafumbua macho yake kitu cha kwanza kilikuwa ni mtoto tu.

Evelyne alimuonea huruma, wakati mwingine msichana huyo aliinuka kutoka kitandani na kwenda sebuleni, huko alikuwa akilia kama mtoto, hakuamini kama alikuwa akipitia maisha yake, alimpenda sana Cassian, alitamani siku moja wawe na familia yao lakini jambo hilo lilishindikana kabisa.

Cassian alipokuwa akiamka na kumkosa mkewe kitandani, alimfuata sebuleni na kumkumbatia, alimfariji kwa kumwambia kwamba kuna siku wangepata watoto hivyo hakutakiwa kuwa na hofu hata kidogo.

“Kuna siku Mungu atatupa familia yetu! Usilie mpenzi, amini kwamba kuna siku tutakuwa na familia yetu,” alisema Cassian huku akiwa amemkumbatia Evelyne.

“Ninaamini mume wangu!” alisema Evelyne huku akilia kilio cha kwikwi.
 
SEHEMU YA 04

“Shoga mwenzako najuta kwa nini sikuwa nikichoma sindano za kuzuia mimba! Yaani umalaya wangu huu leo unanifanya nikose mtoto!

Nimetoa mimba nyingi, mwisho wa siku leo hii nakosa mtoto! Hivi kweli mimi wa kukosa mtoto?” aliuliza Evelyne huku akimwangalia rafiki yake, Mwajuma.

“Mmh! Shoga ila na wewe ulizidi. Kila ulipopata mimba, kazi ilikuwa ni kutoa tu, ona sasa, unamfanya mume wako akose amani, alie kila siku, kwa nini lakini? Tena hata sindano za kuzuia mimba ulikataa kuchoma, ” aliuliza mwajuma.

“Wewe acha tu. Kwanza hapa ninachokitaka ni kufunga naye ndoa tu ili hata kama kuna siku mambo yataharibika basi yaharibike tukiwa kwenye ndoa ili tugawane mali manake bila hivyo naweza kuachwa kibudu,” alisema Evelyne.

“Hilo kweli Eve! Siku mumeo akigundua kwamba hata tatizo lolote ni lazima atakuacha. Umemdanganya sana! Kila nikimwangalia namuonea huruma bilionea wa watu. Wewe mwanamke mbaya sana,” alisema Mwajuma na wote kuanza kucheka.

Mwajuma alikuwa shoga pekee wa Evelyne aliyejua kilichokuwa kikiendelea. Aliyajua maisha ya Evelyne tangu kitambo, walikua wote utotoni na kusoma pamoja.

Katika maisha ya ujana waliyopitia wasichana hao yalikuwa ni maisha ya kujirusha na kila mwanaume aliyekuwa akipita mbele yao.

Waliendekeza ufuska, walitembea na kila mwanaume aliyeonekana kuwa na pesa. Walipenda maisha ya starehe kiasi kwamba wakati mwingine walikuwa wakijiuza katika mitandao ya kijamii wakitafuta pesa na kwenda nchi mbalimbali kutafuta mabwana.

Maisha yao yaliharibika, wanaume ndiyo waliokuwa wakiyaendesha maisha yao. Kutokana na kujiona mjanja zaidi, Mwajuma aliamua kujichoma sindano za kuzuia mimba ila kwa Evelyne, aliogopa kabisa kufanya hivyo.

Evelyne alipokuwa akipata mimba, kitu cha kwanza kilikuwa ni kutoa. Mpaka anakutana na bilionea kijana, Cassian, alitoa mimba zaidi ya kumi na mbili.
 
SEHEMU YA 05

Wakawa wapenzi, wakaanza kuishi pamoja. Kwa kuwa alimpata mwanaume mwenye pesa, Evelyne akatulia, akataka kujenga maisha na kutengeneza familia yake ila tatizo lilikuja pale alipogundua kwamba hatoweza kushika mimba kwa sababu mfuko wake wa uzazi (uterus) na ukuta uliokuwa ukishikilia mfuko huo (cervix) vyote vililegea na mimba isingeweza kukaa tena.

“Huwezi kushika mimba. Mfuko wako wa uzazi umeharibika vibaya kiasi kwamba hauwezi kuruhusu kijusi kutengenezwa,” alisema daktari kwa sauti ya huruma huku akimwangalia Evelyne aliyekuwa akilia pembeni ya rafiki yake.

Hicho ndicho kitu kilichomuumiza mno, hakuamini kama tabia yake ya kutoa mimba ndiyo ingemfikisha mahali hapo.

Alilia na kujuta sana huku wakati mwingine akitamani muda urudi ili arekebishe pale alipokosea lakini hakuweza kuurudisha muda huo.

Alijua kabisa kwamba kama angemwambia mumewe kuwa tatizo alikuwa nalo yeye angemuacha na kutafuta mwanamke mwingine, hivyo alichokifanya ni kutumia pesa zake, kwa kila hospitali waliyotakiwa kwenda kesho, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumtuma Mwajuma huko, alionana na daktari aliyetakiwa kuwapima siku inayofuata na kumpa kiasi kikubwa cha pesa ili aseme kwamba mwanaume ndiye aliyekuwa na tatizo.

Huo ndiyo ulikuwa mchezo wao, walifanikiwa, Cassian hakujua kilichokuwa kikiendelea, kwenye kila hospitali waliyokuwa wakiingia, majibu yalitoka na kusema kwamba yeye ndiye aliyekuwa na tatizo kitu kilichomnyima furaha katika maisha yake.

Wakati hayo yote yakiendelea, Evelyne hakutaka kuonyesha kitu chochote ndani ya nyumba, alimuonyeshea Cassian mapenzi ya dhati kwamba alikuwa akimpenda hivyohivyo kumbe dhamira yake kubwa ilikuwa ni kufunga ndoa na mwanaume huyo ili hata kama kuna siku wangeachana basi wagawane mali.

“Nakuonea huruma mke wangu,” alisema Cassian huku akimwangalia Evelyne.

“Hutakiwi kunionea huruma mume wangu! Nilikwishakwambia kwamba mimi na wewe mpaka kifo kitutenganishe,” alisema Evelyne huku akimwangalia mwanaume huyo.

“Ila sina uwezo wa kumpa mimba mwanamke!”
 
leo nimekuwahi mapema bibie mpaka lukwili nilimis sana story zako, wewe sikukumisi sababu sikufahamu
 
SEHEMU YA 06

“Hilo hutakiwi kujali! Nilikupenda wewe, nakupenda jinsi ulivyo, unaniheshimu, unanithamini, hivyo ni vitu pekee ambavyo kila msichana huvipenda kutoka kwa mtu wake,” alisema Evelyne, wakati akizungumza hayo, tabasamu lilikuwa likionekana kwa mbali.

Bado Cassian alikuwa na mawazo tele, kila siku alipokuwa akimwangalia msichana huyo alijiona mkosefu katika maisha yote. Msichana mrembo kama Evelyne alitakiwa kuwa na mwanaume mwenye uwezo wa kumpa mimba mwanamke si kama yeye.

Mwanamke huyo alimuonyeshea uvumilivu, hakujua kama yeye ndiye mwenye tatizo na si kama alivyofikiria. Kwa kuwa alikuwa amejitolea kumpenda maisha yake yote, kuishi naye basi akataka kufanya kile alichokihitaji, kufunga naye ndoa pasipo kugundua mbinu za mwanamke huyo zilikuwa ni kugawana mali.

Akamwambia kwamba alikuwa tayari kufunga naye ndoa, hiyo ilimpa furaha Evelyne ambapo baada ya kuwa peke yake, akachukua simu yake na kumpigia rafiki yake kipenzi, Mwajuma kwa lengo la kumpa taarifa hiyo.

“Vipi? Mbona asubuhi asubuhi?” aliuliza Mwajuma kwenye simu.
“Mambo yametiki!”
“Umepata mimba?”

“Hapana bhana! Ameniambia nianze kufanya mipango ya harusi,” alisema Evelyne huku akionekana kuwa na furaha tele.

“Kweli?”
“Kwa nini nikudanganye? Tuanze kufanya mipango shoga kabla huyu mpuuzi hajagundua lengo langu,” alisema Evelyne.

“Eeh! Unamuita mpuuzi tena!”
“Hahah! Sasa nimuiteje? Mwanamke wa kukudanganya tena kizembe namna hii! Huyu ni mpuuzi,” alisema Evelyne na kuanza kucheka.

Mipango ikaanza kusukwa, Evelyne akajitoa vilivyo, akawataarifu marafiki zake wote kwamba alikuwa akijiandaa kufunga ndoa na mwanaume wake wa ndoto. Hakufikiria mapenzi, kichwa chake kilifikiria pesa ambazo aliamini kwamba mara baada ya kuachana na Cassian basi angeweza kuzipata.

Marafiki zake wakampongeza, wengine wakamuonea wivu kwani hawakupenda kumuona akiolewa na mwanaume mwenye pesa kama yeye, kila mtu alitaka kuwa na mwanaume mwenye pesa kama Cassian.
 
SEHEMU YA 07

Akawasiliana na marafiki zake waliokuwa Dubai, akawaambia wamuandalie shela kwani alitaka kuvaa vazi hilo kutoka nchini humo.

Akawapigia simu marubani wake wa ndege ndogo ya mpenzi wake aliyokuwa akiitumia kwenda huku na kule, akawaagiza kwamba wajiandae kwani walitakiwa kuondoka kuelekea katika Visiwa vya Comoro kula fungate yao baada ya kufunga ndoa.

Siku haikuwa imefika lakini Dar es Salaam nzima walikuwa wakifahamu kilichokuwa kikiendelea.

Evelyne alimpa taarifa kila mtu aliyekuwa akimfahamu, alitaka watu wote wajue kwamba alikuwa akienda kufunga ndoa na bilionea mkubwa Afrika Mashariki.

“Tuna wiki mbili tu! Kila kitu kipo tayari kwa upande wako?” aliuliza Cassian huku akimwangalia Evelyne.

“Ndiyo mpenzi! Hofu kwako!”
“Huku kwangu kila kitu kipo poa. Nimewasiliana na Mchungaji Sebastian Mark kutoka nchini Ufaransa, amejitolea kuja kutufungisha ndoa.

Nimeandaa boti nzuri na ya kifahari ambayo tutafungia ndoa huko katikati ya bahari,” alisema Cassian huku akitoa tabasamu, japokuwa alikuwa na moyo wa furaha lakini suala la kukosa mtoto lilimkosesha amani.

“Kwenye boti?”
“Ndiyo!”
“Waooo! Jamani baba watoto...” alisema Evelyne na kumkumbatia mwanaume huyo.
 
Back
Top Bottom