Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,166
- Thread starter
- #321
Sehemu ya 101
Aliteremka, baada ya dakika tano, akafanikiwa kufika chini kabisa huku akiwa hoi. Hakusimama, alichokifanya ni kuanza kupiga hatua kuelekea sehemu iliyokuwa na parking ya magari ambapo hapo akaliona gari kubwa la takataka likiwa limefika hapo kwa kuondoa taka usiku huo.
"Nitakwenda nalo hilihili," alisema Edmund na kuingia ndani ya gari hilo ambapo kulikuwa na mifuko mingi myeusi, akaichambua na kujificha katikati ya mifuko hiyo na kutulia.
"Nahisi nitaondoka salama mahali hapa," alijisemea huku akiendelea kujichimbia zaidi.
*** Watu walijaa katika Uwanja wa Ndege wa JFK uliokuwa jijini New York nchini Marekani.
Watu wote waliokuwa mahali hapo walitaka kuwaona mapacha walioungana ambao walikuwa na vipaji vya aina yake, Walter na Walker waliokuwa wameiteka dunia kwa kipindi hicho.
Watu waliwaona sana kwenye televisheni, walitaka kuwaona tena na tena. Walijua kwamba siku chache zilizopita walikuwa nchini humo kabla ya kwenda nchini Tanzania, siku hiyo walitaka kuwaona zaidi, kwa wale ambao hawakuwahi hata kuwagusa, walitaka kuwagusa na hata wale ambao hawakuwa wamesainiwa vitabu vyao, walitaka kuona hilo likitokea.
Muda wote watu hao walikuwa wakiangalia saa zao, waliambiwa kwamba ndege hiyo ingewasili mahali hapo majira ya saa tisa jioni lakini cha ajabu, kila mmoja aliona kama muda ulikuwa umefika ila watu hao hawakuwa wameingia nchini humo.
“Jamani! Mbona wanachelewa hivi?” aliuliza msichana mmoja huku akiangalia saa yake, ndiyo kwanza ilikuwa saa 8:17 mchana lakini waliona kama saa tisa ilikuwa imekwishafika.
Uwanjani hapo hawakuwa peke yao, walikuwa na Waziri Mkuu, Bwana Gordon na mkewe ambao nao walitaka kuwaona mapacha hao ambapo kila kona duniani walikuwa wakizungumziwa wao tu.
Aliteremka, baada ya dakika tano, akafanikiwa kufika chini kabisa huku akiwa hoi. Hakusimama, alichokifanya ni kuanza kupiga hatua kuelekea sehemu iliyokuwa na parking ya magari ambapo hapo akaliona gari kubwa la takataka likiwa limefika hapo kwa kuondoa taka usiku huo.
"Nitakwenda nalo hilihili," alisema Edmund na kuingia ndani ya gari hilo ambapo kulikuwa na mifuko mingi myeusi, akaichambua na kujificha katikati ya mifuko hiyo na kutulia.
"Nahisi nitaondoka salama mahali hapa," alijisemea huku akiendelea kujichimbia zaidi.
*** Watu walijaa katika Uwanja wa Ndege wa JFK uliokuwa jijini New York nchini Marekani.
Watu wote waliokuwa mahali hapo walitaka kuwaona mapacha walioungana ambao walikuwa na vipaji vya aina yake, Walter na Walker waliokuwa wameiteka dunia kwa kipindi hicho.
Watu waliwaona sana kwenye televisheni, walitaka kuwaona tena na tena. Walijua kwamba siku chache zilizopita walikuwa nchini humo kabla ya kwenda nchini Tanzania, siku hiyo walitaka kuwaona zaidi, kwa wale ambao hawakuwahi hata kuwagusa, walitaka kuwagusa na hata wale ambao hawakuwa wamesainiwa vitabu vyao, walitaka kuona hilo likitokea.
Muda wote watu hao walikuwa wakiangalia saa zao, waliambiwa kwamba ndege hiyo ingewasili mahali hapo majira ya saa tisa jioni lakini cha ajabu, kila mmoja aliona kama muda ulikuwa umefika ila watu hao hawakuwa wameingia nchini humo.
“Jamani! Mbona wanachelewa hivi?” aliuliza msichana mmoja huku akiangalia saa yake, ndiyo kwanza ilikuwa saa 8:17 mchana lakini waliona kama saa tisa ilikuwa imekwishafika.
Uwanjani hapo hawakuwa peke yao, walikuwa na Waziri Mkuu, Bwana Gordon na mkewe ambao nao walitaka kuwaona mapacha hao ambapo kila kona duniani walikuwa wakizungumziwa wao tu.