Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #381
Sehemu ya 127
Madaktari hawakuacha kuhangaika, walifanya kila liwezekanalo kuokoa maisha ya mapacha hao.
Kila mtu aliwatumainia, wao ndiyo ulikuwa msaada wa mwisho waliokuwanao kipindi hicho, yaani wao ndiyo waliokuwa wameshililia uhai wa mapacha hao, wao ndyo wangeamua kama watu hao walitakiwa kufa au kuendelea kuishi.
Hawakuwa na mategemeo yoyote ya mapacha hao kupona, damu zilizokuwa zikiwatoka baada ya mishipa kuchanika ziliendelea kusambaa miilini mwao na hivyo kuwafanya kuwa kwenye hali mbaya zaidi.
Ilipofika tarehe 2/09/2016 majira ya saa 2:36 usiku ndiyo muda ambao Walter na Walker wakafariki dunia katika kitanda walichokuwepo.
Hiyo ilikuwa habari ya mshtuko, madaktari ambao walilitambua hilo wakaishiwa nguvu, hawakujua ni kwa namna gani wangeweza kuwaambia wazazi wao juu ya kile kilichokuwa kimetokea kwani kwa kipindi chote ambacho watoto hao walikuwa mahututi nyuso zao zilionekana kuwa kwenye maumivu makali, ingekuwaje kama wangewaambia kuwa walifariki dunia?
“Tutaitoaje miili hii na wakati wazazi wao wapo hapo nje?” aliuliza daktari mmoja.
“Labda tukawatoe!” “Tukawatoe? Tutaanzaje?” “Subiri! Nakwenda kuwachukua na kuwaambia twende kwa daktari kuongea nao. Wakati nimetoka nao, nyie watoeni haraka sana muwapeleke katika chumba maalumu kwanza,” alisema daktari mwingine.
“Sawa.”
Wakakubaliana, hakukuwa na muda wa kupoteza, hapohapo daktari yule akatoka, akaanza kuzungumza nao na kuwaambia kwamba walitakiwa kuzungumza nao katika ofisi yake hivyo awafuate. “Wanaendeleaje?’ aliuliza Naseku huku akimwangalia daktari.
“Wanaendelea salama! Twendeni,” alisema daktari.
Wakasimama na kuanza kuondoka, walipiga hatua fupifupi huku kila mmoja akiwa na mawazo tele.
Daktari alikuwa akiwaza ni kwa namna gani angeweza kuwaambia wazazi hao kile kilichokuwa kikiendelea kwani kwa jinsi walivyokuwa wakionekana, hawakuwa radhi kupokea taarifa kwamba watoto wao walikuwa wamefariki dunia.
Wakaondoka katika korido ile, haraka sana madaktari wale waliokuwa wamebaki ndani ya chumba kile walipoona wameondoka, wakaanza kuitoa miili ile iliyokuwa kitandani na kuipeleka katika chumba kingine.
Madaktari hawakuacha kuhangaika, walifanya kila liwezekanalo kuokoa maisha ya mapacha hao.
Kila mtu aliwatumainia, wao ndiyo ulikuwa msaada wa mwisho waliokuwanao kipindi hicho, yaani wao ndiyo waliokuwa wameshililia uhai wa mapacha hao, wao ndyo wangeamua kama watu hao walitakiwa kufa au kuendelea kuishi.
Hawakuwa na mategemeo yoyote ya mapacha hao kupona, damu zilizokuwa zikiwatoka baada ya mishipa kuchanika ziliendelea kusambaa miilini mwao na hivyo kuwafanya kuwa kwenye hali mbaya zaidi.
Ilipofika tarehe 2/09/2016 majira ya saa 2:36 usiku ndiyo muda ambao Walter na Walker wakafariki dunia katika kitanda walichokuwepo.
Hiyo ilikuwa habari ya mshtuko, madaktari ambao walilitambua hilo wakaishiwa nguvu, hawakujua ni kwa namna gani wangeweza kuwaambia wazazi wao juu ya kile kilichokuwa kimetokea kwani kwa kipindi chote ambacho watoto hao walikuwa mahututi nyuso zao zilionekana kuwa kwenye maumivu makali, ingekuwaje kama wangewaambia kuwa walifariki dunia?
“Tutaitoaje miili hii na wakati wazazi wao wapo hapo nje?” aliuliza daktari mmoja.
“Labda tukawatoe!” “Tukawatoe? Tutaanzaje?” “Subiri! Nakwenda kuwachukua na kuwaambia twende kwa daktari kuongea nao. Wakati nimetoka nao, nyie watoeni haraka sana muwapeleke katika chumba maalumu kwanza,” alisema daktari mwingine.
“Sawa.”
Wakakubaliana, hakukuwa na muda wa kupoteza, hapohapo daktari yule akatoka, akaanza kuzungumza nao na kuwaambia kwamba walitakiwa kuzungumza nao katika ofisi yake hivyo awafuate. “Wanaendeleaje?’ aliuliza Naseku huku akimwangalia daktari.
“Wanaendelea salama! Twendeni,” alisema daktari.
Wakasimama na kuanza kuondoka, walipiga hatua fupifupi huku kila mmoja akiwa na mawazo tele.
Daktari alikuwa akiwaza ni kwa namna gani angeweza kuwaambia wazazi hao kile kilichokuwa kikiendelea kwani kwa jinsi walivyokuwa wakionekana, hawakuwa radhi kupokea taarifa kwamba watoto wao walikuwa wamefariki dunia.
Wakaondoka katika korido ile, haraka sana madaktari wale waliokuwa wamebaki ndani ya chumba kile walipoona wameondoka, wakaanza kuitoa miili ile iliyokuwa kitandani na kuipeleka katika chumba kingine.